Maombi ya LUKU, TANESCO mnanitesa

Maombi ya LUKU, TANESCO mnanitesa

topr

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2014
Posts
700
Reaction score
654
Jamani naombeni msaada wa mawazo!

Nilituma maombi ya LUKU TANESCO mwaka jana mwezi wa kumi na mbili, Nikalipia kila kitu, mwezi wa kwanza wakanambia ndani ya wiki watakuja kufunga Umeme! Nimekaa naona kimya,wiki iliyopita kwenda wananambia TANESCO zote Dar hazina LUKU wala vifaa vya kufungia Umeme, wanatarajia kupata mwezi wa nne mwishoni, so mpaka waje nifungia itakua mwezi wa tano!

Nikaondoka kichwa chini fulu kuwaza mpaka mwezi wa tano na hili joto la mjini yataka moyo basi Leo mshkaji wangu ananambia hata yeye alienda wakamwambia hivyo ila kuna mfanyakazi mmoja kamwambia ampe 150,000/= atamfungia LUKU hizo zipo ofisini!

Sasa jamani, haya mashirika ya umma kwanini yanatutesa hivi?

 
We hujui TANESCO walivyo, we toa rushwa kidogo unakuja kufungiwa umeme,bila hivyo unaweza ukasubiri hata huo mwezi wa 5 na wasije wakaendelea kukuzungusha.

Hii ndio Tanzania yetu.
 
Hii haikubaliki ina maanisha vifaa vipo. Peleka malalamiko yako ngazi ya juu. Kiujumla TANESCO imekithiri kwa rushwa. Inachukulia rushwa kama mtindo wa maisha. Hii haikubaliki hata kidogo nenda ngazi za juu kwani inabidi kukomesha ni si ku-encourage.
 
Back
Top Bottom