Habari za leo ndugu zangu. Poleni kwa majukumu ya kila siku, naimani mungu yu pamoja nasi katika mihangaiko ya kila siku na kutupatia riziki sisi sote.
Ndugu zangu naomba kufahamishwa kuhusu manunuzi ya bidhaa kupitia application ya AliExpress. Application hii nimeipata nikiwa katika kuangalia bidha mbalimbali mtandaoni. Nimevutiwa na bidhaa zao. Lakini ningependa kupata uzoefu kwa yoyote aliyewahi kufanya order kupitia AliExpress.
Lakini pia jinsi gani naweza kufanya malipo mpaka pale mzigo utakaponifikia. Pia ni njia gani wanayoitumia kufikisha mzigo mana kwenye Application yao nimeona wameandika (free shipingi via China Post Registered Office Mail). Na je kwa waliowahi kutumia njia hii ya manunuzi uhakika wa kupata bidhaa uliyoagiza ni wa kiasi gani.
Ningependa kujua zaidi kwa wale wenye taharifa zaidi juu ya hili. Natanguliza shukrani zangu za dhati na nitashukuru kwa msaada wenu.
Ndugu zangu naomba kufahamishwa kuhusu manunuzi ya bidhaa kupitia application ya AliExpress. Application hii nimeipata nikiwa katika kuangalia bidha mbalimbali mtandaoni. Nimevutiwa na bidhaa zao. Lakini ningependa kupata uzoefu kwa yoyote aliyewahi kufanya order kupitia AliExpress.
Lakini pia jinsi gani naweza kufanya malipo mpaka pale mzigo utakaponifikia. Pia ni njia gani wanayoitumia kufikisha mzigo mana kwenye Application yao nimeona wameandika (free shipingi via China Post Registered Office Mail). Na je kwa waliowahi kutumia njia hii ya manunuzi uhakika wa kupata bidhaa uliyoagiza ni wa kiasi gani.
Ningependa kujua zaidi kwa wale wenye taharifa zaidi juu ya hili. Natanguliza shukrani zangu za dhati na nitashukuru kwa msaada wenu.