Mangula amkosoa Ole Sendeka

Mangula amkosoa Ole Sendeka

Anguko lap ni.marekebisho ya katiba ujanja wao ndio upo hapo basi...
 
watu wanashindwa kutofautisha kati ya siasa na kampeni ya uchaguzi,siasa haiwezi kuwa na mwisho kampeni ndio ina mwisho ,kuisha kwa siasa ni kufutwa kwa vyama vya siasa.
 
Na hii ni ishara kuwa ccm wanakwenda kupasuka mapande ya kikanda kwani hawa wazee waling'ang'ania madaraka wakasahau kuwajenga vijana. Na hivi wengi wa vijana waliopo kwenye vijinafasi ni wanaharakati zaidi ya kuwa wanasiasa. Nao wapo kimaslahi zaidi. Hivyo kwa makosa ya hawa wazee ccm itazidi kupwaya na kupasuka mara dufu na hatimaye kufa kabisa. Siku hawa wazee wakiziwahi namba kwa muumba ndipo mtawaona hawa kina ole watakavyokikimbia chama. Hakuna ujenzi wa chama kwa sasa bali kuna ujenzi wa nchi. Ccm na viongozi mababu.
 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bara, Philip Mangula, amekosoa kauli ya Msemaji wa chama hicho, Christopher ole Sendeka ya kupambana na vyama vya upinzani kwenye majukwaa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Tamasha la Kigoda cha Mwalimu Nyerere lililofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema siasa ina wakati na mahali pake.

“Hata msemaji wetu alikosea kusema CCM ingeenda kupambana nao huko huko barabarani. Hatuwezi kufanya kitu kama hicho kwa sababu haijengi badala yake inabomoa, wakati huu ni wakati wa kujenga nchi.

“Siasa ina muda na wakati wake…tulifanya siasa za majukwaani wakati wa kampeni na uchaguzi na ule ulikua wakati wake lakini hivi sasa kuna Bunge ambalo linajadili suala muhimu la bajeti ya Serikali halafu mtu badala ya kukaa bungeni atoe mchango wa kujenga na kuboresha anataka kwenda kusimama kwenye majukwaa, suala ambalo halitasaidia kitu,” alisema Mangula.

Hivi karibuni, Sendeka alizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam akilaani operesheni okoa demokrasia iliyoanzishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Akizungumzia kuhusu uongozi wa Mwalimu Nyerere na ule wa sasa, alisema tatizo linalosumbua ni watu kununua uongozi huku wapiga kura wakiomba kununuliwa.

Alisema CCM imekuwa ikijitahidi kupambana na tatizo hilo kwa kuwaondoa wale wanaobainika kununua uongozi.

“Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000 katika majimbo manne tuliwaondoa wagombea wa ubunge waliokuwa wameshinda nafasi ya kwanza na ya pili na kuteua walioshika nafasi ya tatu kwa sababu ya rushwa.

“Pia katika majimbo 10 tuliteua wagombea walioshika nafasi ya pili na kuwaacha waliokuwa wameshinda baada ya kubaini kuwapo vitendo vya rushwa,” alisema.

Alisema watu wasiojua nini kinachoendelea wamekuwa wakilalamika kuwa chama hicho hakina demokrasia suala ambalo si kweli.

Chanzo: Mtanzania
Mh mang'ula Mbona umetoa mifano ya zamani SANA ? Hiyo ya 2000 is irrelevant, why not 2010 Na 2015?
 
CCM ingekuwa inataka hata wapinzani washiriki kujenga nchi kupitia bunge wangeacha lugha za kuudhi Na ngonjera zao
 
Hakika nalisubiri anguko kuu la CCM, na siku ikitoka madarakani nitatembea kwa mguu kutoka Kingolwira hadi Lumumba kuwazodoa hao
Naona kama ikitokea utakuwa mzee sana na hutoweza kutembea. Nakushauri weka nadhiri ya mafanikio katika shughuli za kukuingizia pesa.

Unadhani kwa watu wa UKAWA wanaweza kuleta ukombozi zaidi ya kushibisha matumbo yao? Bado sana.
 
big up mzee M. bishara ya kucopy na kupest ya wapinzani huku hujajifunza malengo yao marfuku!!
 
Back
Top Bottom