Maneno ya hekima ya kutafakari

wa stendi

JF-Expert Member
Jul 7, 2016
24,688
26,796
*Nyati wanaua watu 7 kila mwaka.*
*Simba wanaua watu 500 kila mwaka.*
*Kiboko wanaua watu 800 kila mwaka.*
*Mabuibui wanaua watu 5000 kila mwaka.*
*Nnge wanaua watu 7000 kila mwaka.*
*Nyoka wanaua watu 10000 kila mwaka.*

*Kisha cha kushangaza,*

*Mbu wanaua watu milioni 2.7 kila mwaka...! Ndio... Walio wadogo kabisa ndio wanaoua sana..!!*

*Dhambi ndogo ndogo, ambazo wengi hawazioni au hawazitambui, ndio zenye kuua zaidi maisha yako ya kiroho (imani).*

*Epuka kutosali kutenga muda mchache wa siku yako kwa ajili ya Mungu wako.*

*Dhambi za upungufu zinaua kama dhambi za uamuzi tu..!*

*Kusengenya na uongo mdogo mdogo, kunafanywa mara kwa mara na ndio mauti.*

*Chunga yale madogo madogo unayoyafanya kila siku, ndio yatakayo kuangusha.*

*Watu wa kufanikiwa wana mambo mawili midomoni mwao: _Tabasamu na Kimya_.*

*Tabasamu inaweza kutatua matatizo, na kimya kinaweza kuepusha matatizo.*

*Sukari inaweza kuchanganywa na chumvi, lakini siafu wanaikataa chumvi na wanaibeba sukari pekee.*

*Chagua watu wa sawa katika maisha, uyafanye maisha yako yawe bora na matamu.*

*Ukishindwa kufikia ndoto zako, badilisha mbinu wala sio Mungu wako*

*Kumbuka miti hubadilisha majani yake, wala sio mizizi yake.*

*Hutafikia unakokwenda (lengo lako) ikiwa utasimama kurushia mawe kila mbwa anaye kubwekea.*

*Wapinzani wakikuona unatembea kwenye maji, watasema ni kwasababu huwezi kuogelea.*

*Hata ukicheza kwenye maji, maadui wako watalalamika unarusha vumbi.*

*Fanya hamu yako iwe kuishi maisha ya utulivu, kutizama yako, na kufanya kazi kwa mikono yako.*

*Kumbuka usishindane hata na nguruwe... Mutachafuka nyote lakini nguruwe atafurahia..!*


*KUWA MWENYE HEKIMA*
Kosa mahali popote ila kwa Mungu usikose.

Tafadhali usidharau dhambi ndogo ndogo ili tuuone ufalme wa mbinguni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom