We utakuwa shahidi wa yehova sio bure
hakuna mkatoliki mwenye imani hiyo_usitudanganye
Mkuu, mimi ni Mkatoliki kimsingi.
Lakini kuwa Mkatoliki hainifanyi nisijifunze ama kusoma makala pamoja na maandiko kadhaa yanayo muhusisha Mungu na kifo.
Kwamfano nilipo soma kitabu cha
Death—kinasema The Final Stage of Growth. Maneno hayo yanadhihirisha ile imani kwamba kifo ni tukio la kawaida, mwisho wa viumbe wote walio hai. Imani hiyo imefanya watu wawe na tabia ya kutumia fursa yoyote inayotokea ili kujinufaisha.
Lakini je, kwa kweli kifo ni mwisho wa uhai? Si watafiti wote wanaoamini jambo hilo. Kwa mfano, Calvin Harley, mwanabiolojia anayechunguza hali ya kuzeeka kwa binadamu, alisema katika mahojiano fulani kwamba yeye haamini kwamba wanadamu “wamekusudiwa wafe.” Mtaalamu wa kinga ya mwili, William Clark alisema: ‘Si lazima tufe.’ Naye Seymour Benzer kutoka Chuo cha Tekinolojia cha California anasema, ‘hatuwezi kusema kwamba kuzeeka ni jambo lisiloweza kuzuiwa, bali ni mfululizo wa matukio tunayoweza kubadilisha.’
Wanasayansi hushangaa wanapochunguza maumbile ya wanadamu. Wanakuta kwamba tumeumbwa tukiwa na uwezo mwingi sana wa kufanya mambo. Tunatumia tu kiasi kidogo sana cha uwezo huo katika kipindi cha miaka 70 hadi 80 ambacho tunatazamia kuishi. Kwa mfano, wanasayansi wamegundua kwamba ubongo wa binadamu una uwezo mkubwa sana wa kukumbuka mambo. Mtafiti mmoja alikadiria kwamba ubongo wetu unaweza kuhifadhi habari ambazo “zingejaza mabuku milioni ishirini yanayoweza kutoshea mojawapo ya maktaba kubwa zaidi ulimwenguni.” Wataalamu fulani wa mfumo wa neva wanaamini kwamba mwanadamu hutumia sehemu ndogo sana ya ubongo wake katika maisha yake yote. Inafaa kuuliza, ‘Kwa nini tuna ubongo wenye uwezo mkubwa hivyo ilhali sisi hutumia sehemu ndogo sana katika maisha yetu?’
Pia fikiria jinsi ambavyo wanadamu hutenda kwa njia isiyo ya kawaida wanapokabiliwa na kifo! Kwa wengi, kifo cha mke, mume, au mtoto kinaweza kusababisha majonzi makubwa maishani. Mara nyingi, hali ya watu ya kihisia-moyo huvurugika kwa muda mrefu baada ya kifo cha mpendwa. Hata wale ambao hudai kwamba kifo ni tukio la kawaida kwa binadamu hushindwa kukubali wazo la kwamba kifo chao wenyewe kitamaanisha mwisho wa mambo yote. Gazeti British Medical Journal lilitaja ‘maoni ya kitaalamu kwamba kila mtu hutaka kuishi muda mrefu iwezekanavyo.’
Tunapofikiria jinsi mwanadamu anavyokiona kifo, uwezo wake wa pekee wa kukumbuka na kujifunza, na tamaa yake ya moyoni ya kuishi milele, je, si wazi kwamba aliumbwa aishi? Kwa kweli, Mungu aliwaumba wanadamu wakiwa na taraja la kuishi milele, bali si wafe. Ona wakati ujao ambao Mungu aliwaandalia wenzi wawili wa kwanza wa kibinadamu: “Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.” (Mwanzo 1:28) Huo ulikuwa wakati ujao wa kudumu ulio mzuri kama nini!