Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,230
Mgombea Udiwani wa Kata ya Kariakoo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Haji Sunday Manara, ameahidi kuwafikia wapiga kura wote wa kata hiyo ili kuwaomba kura, akisisitiza kuwa bado ana nguvu na ari ya kufanya kazi hiyo kikamilifu.
Soma Pia: Mgombea Udiwani kata ya Kariakoo Haji Manara akiomba kura ndani ya Daladala
Manara alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha ndani cha Kamati ya Siasa ya CCM Kata ya Kariakoo, kilichoitishwa kwa lengo la kujadili na kupanga mikakati ya kampeni kwa ajili ya kuwaombea kura wagombea wa chama hicho. Kikao hicho kilijadili mikakati ya kumsaidia mgombea urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na mgombea ubunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azzan Zungu.
Soma Pia: Mgombea Udiwani kata ya Kariakoo Haji Manara akiomba kura ndani ya Daladala
Manara alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha ndani cha Kamati ya Siasa ya CCM Kata ya Kariakoo, kilichoitishwa kwa lengo la kujadili na kupanga mikakati ya kampeni kwa ajili ya kuwaombea kura wagombea wa chama hicho. Kikao hicho kilijadili mikakati ya kumsaidia mgombea urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na mgombea ubunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Azzan Zungu.