Man Walter' abwaga manyanga

Man Walter' abwaga manyanga

Nyundo_tz

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2009
Posts
640
Reaction score
21
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"][/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD]
Prodyuza na mmiliki wa studio ya Combination Sound, John Shariza a.ka Man Walter amezitaja sababu zilizomfanya msanii 20% kutokwenda kwenye studio yake.

Msanii huyo ambae ameandaa albamu yenye nyimbo kadhaa ambazo amezifanya na waandaaji tofauti badala ya Man Water aliyemfanyia kazi kwenye albamu iliyopita ambayo ilimfanya ashinde tuzo tano kwenye shindano la Kili Music Award.

Man Water alisema 20% hawezi kwenda kwenye studio yake na nawezekana anaogopa kutokana na matendo aliyofanya kwenye shoo aliyoiandaa rasmi kwa ajili ya kuwashukuru wapenzi waliowasapoti mpaka 20% kushinda tuzo tano aliyoiita 'Shukrani' ambayo ilifanyika Morogoro.

Alisema aliwaalika baadhi ya wanamuziki kufanya shoo akiwemo 20% lakini hakuna walichokifanya stejini zaidi ya kupiga kelele na kuongea walichokitaka wao kiasi kwamba mashabiki walianza kutoka ukumbini.

"Nilikuwa na nia nzuri ya kuwashukuru mashabiki wetu kwa kutuunga mkono alkini kilichotokea sikukitegemea na sijawahi kuzungumza na vyombo vya Habari kuhusu hilo ,lakini 20% alinitukana an kusema ninamtumia kama sabuni kujinufaisha kama hiyo haitoshi atakuja kunifanyia kitu kibaya ambacho sitakuja kusahau na kwamba Combination kitu gani Studio zipo nyingi "alisema M an.

Kwa upande wake 20% alisema kuwa hana tatizo lolote na Man nakilichomfanya akafanye kazi zake kwenye studio nyingine ni kwamba kipindi anafanya hizo kazi Man alikuwa na kazi nyingi hivyo asingeweza kumudu kuandaa na za kwake.
"Sina tatizo na Man na hata kilichotokea Morogoro ilikuwa ni kuelekezana tu sasa mkielekezana si lazima muonyesheane vidole au muongee kwa nguvu kidogo ndio watu wanadhani tumegombana"alisema 20%.


[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Man walter abwaga manyanga
 
Mkuu ni kweli wasanii wa Bongo taabu kweli kweli dogo badala ya kutazama alikotoka na anapokwenda kashaanza kunyanyua mabega juu.

Wasanii wa bongo mafanikio kidogo tu wanaleta kujua, ndio maana wengi wao Albamu moja tu wanapotea.
 
Wasaniii wetu wakizazi cha awali na kipya (hawana tofauti sana ikija katka sula hilii la jinsi ya ku handle umaarufu) wana taabu sana ya ku-handle umaarufu!!! Akisikika katika radio zetu akashinda nafasi katika chati za FM radio zetu baada ya muda mfupi anajiona sawa na mastaa wa majuu!!!

Kama ni kundi, utasikia anayedhani ni muhimili anatoka na kuanza kutumbuiza kivyake!! Producer na/au meneja anabadilisha kisa; wanamwibia na kumtumia......Kwani hawana mikataba????

Kuendelea kwa wasanii wetu kutatokana na kuheshimu fani zao na kukubali kuwa kukua katika fani yoyote ni process; haikosi mikwaruzano na kukubali kujifunza kila siku!!! HAwa wasanii wetu wanadhani wanajua kila kitu!!!!
 
ni kweli jamaa alikuwa anmtumia...he was never a good manager..huwezi ukaandaa show then utegenee msanii afanye reharsals mwenyewe
 
Watz wengi wanashindwa kujua kwamba vitu vyote vizuri vinahitaji garama! Na kuna watu wanagaramia, hawa wasanii wanapoenda stejini na kuona mass imehudhuria na stage inapendeza hawafikirii kwamba haikuwa rahisi kufanikisha hayo, na kudhani pesa yote inayopatikana kwenye shoo iwe ya kwao! Never, it's not like that. Huyo 20 hapo ndio mwisho wake, amini msiamini!
 
leo ndo nimejua kuwa shariza ni man wota, nilidhani wako mapacha
 
Dah, rest in peas 20% umeamua kujizika mwenyewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom