KERO Mamlaka za TANROAD Kigamboni zipo?

KERO Mamlaka za TANROAD Kigamboni zipo?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Barabara za Kigamboni hazina usimamizi wakati wa kufanya marekebisho. Ni kama vile hakuna usimamizi au mamlaka za TANROAD hazipo Kabisa Kigamboni.

Kipande cha kurekebisha wiki moja kinachukua miezi 6 hadi nane.

Mathalani ukipita Kigamboni maeneo ya Machava hadi Tanzanite kuna vipande vya barabara vimeanza kufanyiwa ukarabati kwa sasa inakwenda mwezi wa 6 havijakamilika. Ni vipande ambayo vingepaswa kukamilika ndani ya wiki mbili tu.

Serikali na mamlaka zipo wapi?
 
Kuna kipande pale Geza juu, hakizidi mita 50 tangu mwaka huu uanze hakiishi. Sio Tanroads tu idara nyingi za serikali sasa hivi haku a uwajibikaji.
 
Back
Top Bottom