Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Mkuu wa mamlaka hiyo akiwa na timu ya askari amaedai wamehamishia shughuli zao katika eneo lililoaribiwa na mvua zinazoendelea kunyesha na kwamba hawatatoka hadi miundombinu itengamae.
Wakati hayo yakijiri RPC wa Arusha ameeleza kwamba wapo katika hatua za kuwasaka wahujumu uchumI waliopiga picha barabara hiyo na kusambaza mitandaoni huku akimwelekeza Mbunge wa Arusha Mjini kukaa mbali na jambo hilo na asitafute mtaji wa kisiasa.
Haya yanajiri baada ya video kusambaa zikionesha ubovu wa barabara katika hifadhi hiyo jambo lililopelekea Mkuu wa Mkoa wa Arusha kukemea tabia ya watu kusambaza taarifa zinazochafua taswira ya nchi kwenye mitandao badala ya kuripoti matatizo yao katika mamlaka husika yaweze kupatiwa ufumbuzi. RC Gambo alikwenda mbali zaidi na kufananisha kitendo cha kusambaza taarifa hizo kama kosa la uhujumu uchumi.
Baada ya mamlaka kujitokeza na kueleza madhara yaliyoletwa na mvua zinazodaiwa kuanza kunyesha septemba hadi sasa, wadau mbalimbali wameibua majadiliano wakihoji ni nani yupo sahihi kati ya mchukua video aliyeisambaza mitandaoni na kuzifikia mamlaka za serikali, RC aliyepiga vita tabia ya kusambaza picha na Muhifadhi Mkuu aliyekiri uwepo wa tatizo na kulitaftia ufumbuzi.
Baadhi ya wadau wameendelea kuhoji, je kitendo cha Mamlaka kukiri na kupeleka timu huku wakitumia vyombo vya habari kuwahabarisha wananchi juu ya kile serikali inafanya haiwezi kuibua msuguano wa kiutendaji na kuwafanya waonekane wamekwenda kinyume na maelekezo au mtizamo wa RC?
Wengine wanahoji, kwanini RC hakujikita katika kutafuta suluhisho la tatizo kwani ni ukweli ulio wazi kwamba eneo la hifadhi halijengwi barabara za lami na ni jambo la kawaida barabara za vumbi kuaribiwa na mvua au hata magari na kila wakati hufanyiwa ukarabati, kwanini aliona kama njia iliyotumika ililenga kuhujumu uchumi na si kuujenga uchumi?
Wadau wengine wanahoji wizara yenye dhamana ilikuwa wapi hadi uharibifu kama huo unatokea na hawakuchukua hatua? Mamlaka ilikuwa wapi hadi kero inakuwa kubwa kwa kiasi hiki?
Je, njia sahihi za kufikisha ujumbe kwa serikali ni ipi na imeandikwa wapi? Tumezoea wananchi wakiibua hoja dhidi ya changamoto wanazokabiliana nazo, hoja hizi uibuliwa katika mikutano ya adhara mbele ya vyombo vya habari, je huu ni uhujumu uchumi?
Wakati hayo yakijiri RPC wa Arusha ameeleza kwamba wapo katika hatua za kuwasaka wahujumu uchumI waliopiga picha barabara hiyo na kusambaza mitandaoni huku akimwelekeza Mbunge wa Arusha Mjini kukaa mbali na jambo hilo na asitafute mtaji wa kisiasa.
Haya yanajiri baada ya video kusambaa zikionesha ubovu wa barabara katika hifadhi hiyo jambo lililopelekea Mkuu wa Mkoa wa Arusha kukemea tabia ya watu kusambaza taarifa zinazochafua taswira ya nchi kwenye mitandao badala ya kuripoti matatizo yao katika mamlaka husika yaweze kupatiwa ufumbuzi. RC Gambo alikwenda mbali zaidi na kufananisha kitendo cha kusambaza taarifa hizo kama kosa la uhujumu uchumi.
Baada ya mamlaka kujitokeza na kueleza madhara yaliyoletwa na mvua zinazodaiwa kuanza kunyesha septemba hadi sasa, wadau mbalimbali wameibua majadiliano wakihoji ni nani yupo sahihi kati ya mchukua video aliyeisambaza mitandaoni na kuzifikia mamlaka za serikali, RC aliyepiga vita tabia ya kusambaza picha na Muhifadhi Mkuu aliyekiri uwepo wa tatizo na kulitaftia ufumbuzi.
Baadhi ya wadau wameendelea kuhoji, je kitendo cha Mamlaka kukiri na kupeleka timu huku wakitumia vyombo vya habari kuwahabarisha wananchi juu ya kile serikali inafanya haiwezi kuibua msuguano wa kiutendaji na kuwafanya waonekane wamekwenda kinyume na maelekezo au mtizamo wa RC?
Wengine wanahoji, kwanini RC hakujikita katika kutafuta suluhisho la tatizo kwani ni ukweli ulio wazi kwamba eneo la hifadhi halijengwi barabara za lami na ni jambo la kawaida barabara za vumbi kuaribiwa na mvua au hata magari na kila wakati hufanyiwa ukarabati, kwanini aliona kama njia iliyotumika ililenga kuhujumu uchumi na si kuujenga uchumi?
Wadau wengine wanahoji wizara yenye dhamana ilikuwa wapi hadi uharibifu kama huo unatokea na hawakuchukua hatua? Mamlaka ilikuwa wapi hadi kero inakuwa kubwa kwa kiasi hiki?
Je, njia sahihi za kufikisha ujumbe kwa serikali ni ipi na imeandikwa wapi? Tumezoea wananchi wakiibua hoja dhidi ya changamoto wanazokabiliana nazo, hoja hizi uibuliwa katika mikutano ya adhara mbele ya vyombo vya habari, je huu ni uhujumu uchumi?