Mamia Pangani wahamia CHADEMA.

Mamia Pangani wahamia CHADEMA.

Asante sana kamanda mtoi siku tanga wakiamua kwa nguvu zaozote kuikataa ccm basi ukombozi umefika, yaani kamanda golugwa namkubali sana kwa siasa zake za kistaraabu na akili nyingi, ccm hakika mmeishiwa
 
kamanda MTOI tunakushukuru sana kwa taarifa , MUNGU akulinde sana .
 
Kakae na mwalimu wako wa hesabu za darasa la kwanza umuulize watu 85 wa Pangani + watu 70 wa kiomoni wilayani Tanga jumla yake ni ngapi?!

Ukipata jibu kameze panadol upumzike.
teh teh, nimeipenda hiyo, inaonekana ni division 5 huyo!
 
Wanachama 85 waliokuwa CUF, ADC na CCM wilayani Pangani wamehamia CHADEMA leo mara baada ya kukutana na katibu wa kanda ya kaskazini Bw Amani Golugwa alipo kuwa anafanya ziara ya kukagua zoezi la Chadema ni msingi wilayani humo.

Miongoni mwa wamachama hao alielezea namna walivyo wahi kupelekwa kisiwani Pemba wakiwa wamevalishwa mavazi ya kijeshi ili wakapigie kura chama tawala wakati wa uchaguzi wa mwaka 2010.

Zoezi la chadema ni msingi linaendelea kwa kasi mkoani Tanga huku mamia ya wananchi wakizidi kujiunga na chadema, miongoni mwa wananchi hao amekemea propaganda mbaya za udini zilizokuwa zinatumiwa na ccm dhidi ya vyama vya upinzani kwa kusema kuwa zimechangia kwa kiasi kikubwa sana kuleta mgawanyiko na malumbano ya udini yasiyo kuwa na tija kwa taifa.

Alisema mara zote ccm wamewaaminisha watu wa Pangani kuwa CUF ni chama cha waislamu na chadema ni chama cha wakristo lakini hakuna hata siku moja ambayo ccm wamesha wahi kusema kuwa wao ni chama cha watu gani. "...Baada ya sisi kutumiwa sasa tumeamua kufuata chama chenye dhamira na nia ya dhati kutukomboa"

Jana wanachama zaidi ya 70 wa kata ya kiomoni wilayani Tanga ambayo hivi karibuni kwenye uchaguzi wa kitongoji chadema iliibuka mshindi wamejiunga na chadema na wako kwenye maandalizi ya kushinda kiti cha udiwani kilicho wazi kwenye uchaguzi mdogo unao tarajiwa kufanyika mapema mwezi Februari.

Boss, mamia yana tarakimu tatu. Ulale salama (kama unalala)
 
Mkuu mbona picha zako hazisadifu unachokizungumzia?
hao mamia na huo mkutano mbona hakuna picha?
 
Ccm inakufa kifo cha kimya wamekazana kuizungumzia chadema bila kujua wanakitangaza zaidi chama kingine kuliko chao na sasa watu wanasepa chama cha mateso na mauaji CCM na kujiunga na watetezi wa haki chini ya chama cha Chadema
 
Kuna watu wajinga mnajifanya mna akili lakini kumbe kichwani ni mbulumundu plus plus. Umeambiwa mamia ya watu waamia chadema. Hao 85 ni wale waliotokea ADC, CUF na CCM tu. Angeanza kutaja wa NCCR,TLP Pona, SAU, Chaumma wangefika idadi ya mamia. Hao 85 ni wa CUF, CCM na ADC.
Mgosi Mohamedi Mtoi asante kwa taarifa ya kutia moyo kwenye harakati hizi za kumtoa mkoloni mweusi

Heading "mamia" halafu kwenye habari yenyewe "mamia" wamesahaulika!!
Hiyo inawezekana kwenye chama cha kilaghai tu...
 
Last edited by a moderator:
Chadema Bravo hakuna kulala lazima uvute na kunywa maji ya uzima
 
Kamanda Mtoi endeleza swaga mafanikio yanaonekana, siku ukirudi jukwaani ushindi kabla ya kupiga kura
 
Mtoi,
acha uongo, gharama ya uongo ni kubwa mana inaweza kukushushia heshima na thamani a utu wako

ktk taarifa yako umetoa takwimu za watu 85 na hapo hapo 70. Unapodanganya jitahidi kuwa na kumbukumbu

Acheni umbea,kama hamuamini nendeni mkajionee kwa macho yenu,una panda bus la raha leo kutoka dar-pangani,mimi nimepigiwa simu kutoka sakura,kilimangwido,Boza,mauya,Bweni na mkwaja kuwa Chadema inakuja kwa kasi Pangani.Kwa taarifa ya mohamed Mtoi naunganisha dots.HUTAKI UNA ACHA.
 
Mohamedi Mtoi mbona hakuna picha hapo inayozidi watu watano, wacha hao mamia uliosema?

Hivi uongo unawasaidia nini? hata haya huoni? wala vibaya hujui?

Ukitaka kula nguruwe usiseme unaonja, mle ushibe. Si ungesema mamilioni au malaki.
 
Picha huwa ni kioo cha kile unachokisema.

Sasa hii ya kusema watu mia halafu picha inaonyesha huyu binadamu alikuwa na mkutano wa kaya ni mwendelezo wa ulaghai ndani ya CHADEMA.

CHADEMA kimejaa watu ambao ni mafundi wa kutengeneza uongo na kutaka kuaminisha kwa nguvu zote kuwa kweli.

Siyo ajabu hata migogoro yao inawashinda kuitatua. Huwezi ukasimamia matendo ya kilaghai ukategemea kutoa haki. Never!

Ulaghai unaitafuna CHADEMA.

Kwa sasa wanawalaghai watu kuwa CCM ndiyo kichocheo wakati ulaghai wao ndiyo chanzo cha migogoro.
 
Back
Top Bottom