Mambo yawa magumu kwa Rais Joyce Banda wa Malawi

pmwasyoke

JF-Expert Member
May 27, 2010
4,594
2,981
Hivi sasa kuna mgomo wa wafanyakazi karibu wote wa serikali wa ngazi za kati na chini nchini Malawi.

Wanaoendelea na kazi, ni madaktari na manesi tu ambao pia wanasema watajiunga na mgomo huo baada ya siku kadhaa iwapo madai ya wafanyakazi hayatekelezwi.

Viwanja vya ndege vimefungwa, mipaka haipitiki, shule zote za serikali zimefungwa, maofisi ya serikali yamefungwa nk.

Wafanyakazi wanataka nyongeza ya mshahara ya asilimia 67 na mambo mengine kadha wa kadha yahusianayo na kuboreshwa vipato na mazingira ya kazi.

Rais Banda, mara alipochukua madaraka mwaka jana baada ya kifo cha Bingu wa Mutharika, alidevalue kwacha na kuachia thamani yake ifloat. Hii ilikuwa kukubaliana na masharti ya IMF. jambo hili limesababisha hali ngumu sana kwa watu wa kawaida kwa sasa - japo wanaambiwa huko mbele hatua hizi zitasababisha recovery nzuri ya uchumi.
 
Hakuna mahali popote pale duniani ambapo masharti ya IMF na WB yalileta mafanikio yoyote yale ya kiuchumi. Mwalimu RIP alikuwa na upeo mkubwa sana katika kuchanganua mambo na kukataa masharti mbali mbali ya IMF na WB likiwemo la devaluation of Tanzania's currency. Waliofuata baada ya Mwalimu waliyakumbatia masharti ya IMF na WB lakini hadi leo hii ukiwauliza mafanikio yake wanang'aa macho.
 
Na kwa kweli hali ilivyo hivi sasa hapa Malawi masharti ya IMF yanawatesa ile mbaya. Lakini kabla ya huyu mama kuingia madarakani na kuikumbatia IMF, nchi ilikuwa haina cha mafuta, forex, nk., vitu ambavyo kwa sasa kuna unafuu mkubwa. Issue ni uwepo wa mafuta na forex kiasi hakuwasaidii walio wengi wanaoathirika mno na thamani ya kwacha inayodondoka kasi mno kila kukicha!
 
Hata tukiingia vitani wanajeshi wake wote watagoma

Nadhani hapo watashikamana na kusahau tofauti na serikali yao!

Ajabu watoto wa shule za Msingi na sekondari wanaandamana kudai haki yao ya kufundishwa - kwani walimu wako kwenye mgomo. Inaelezwa kuwa madaktari na wahudumu wengine wa afya nao wameanza mgomo!
 
Sasa imekuwa vipi tena. Kila siku kulikuwa na media spinning hata hapa JF watu walizinunua hizi spinning na kumuona Mama ni gwiji wa mabadiliko ya kiuchumi nchini.

Kuuza presidential jet na presidential car limousine nilifikiri 'kutasaidia kuondoa umaskini' au nayo ilikuwa ni changa macho.

Ukiona Kiongozi wa nchi ya Africa anaanza kupongezwa na watu wa WEST na media zao ni dalili ya kutosha kujua kama huyo ameisha ula mkenge na wameisha pata walichokuwa wanakitafuta (samaki amemeza ndoana).

Mama wa watu kila akihojiwa na media za west, yeye majibu yake mengi yako kwenye fikra za misaada badala ya fikra za nchi yake kujitegemea.

Hizo pesa wanazompatia wanajua watazikamua kwenye natural resources ambayo iko mbioni kuanza kuvunwa nchini.

Mama Banda, there ain't no such thing as a free lunch.
 
Sasa zile fujo za ziwa Nyasa alitaka kuwapotezea wananchi wasahau machungu ya maisha?akiingia kwenye vita itakuwaje?
 
Habari za kugombea ziwa nyasa zimefia wapi? Vita ipo....?

Walisema habari ile ingeshughulikiwa na kamati ya baadhi ya marais wastaafu wa nchi za Afrika. Malawi walitangaza kwamba wamekwishapeleka submission yao kwenye kamati hiyo. Sielewi kama na Tanzania imekwishapeleka au bado.
 
Vita ipo baada ya migomo kuisha tutamalizia machungu kwenu watanzania , hivi huko Malawi vyama vya upinzani havifanyi uchochezi kama huku tz ,

Hata hivi chama tawala (PP) kinaamini kwamba vyama vya upinzani, na hasa DPP, ndivyo vimechochea mgomo unaoendelea na kuhamasisha/kushabikia maandamano. Ukizingatia kwamba mwakani (2014) Malawi wana uchaguzi mkuu ni wazi kurushiana tuhuma miongoni mwa vyama kumeshika kasi.
 
Back
Top Bottom