Mambo yatakayoing'oa CCM madarakani October 2015

Mambo yatakayoing'oa CCM madarakani October 2015

kujiaminisha na kujisahau kwamba wao ndo watawala wa maisha wa taifa hili
 
Imefanya nini hiyo miiko ya viongozi?

haitumiki vizuri na hata ikitumika inapika chakula kibichi hakiivi ndo mana tunaaamua sasa kufanya maamuzi magumu OCT 15
 
Kwa dalili hizi zilizotajwa hapa ukweli ni kwamba kazi ipo!
 
21. Safari nyingi za nje zisizo tija, au tija yake haikufafanuliwa
22. Ridhwani Kikwete
 
(21)Kung'oa watu kucha na meno bila ganz,
(22) kuwaambia watanzania wasiotaka kulipa bili ya umeme mpya watumie vibatar,
(23) Asiyetaka kulipa nauli mpya ya kivuko apige mbizi,
(24) watanzania wapigwe tu hatuna jins maana tumechoka,
(25) nimetochoka na nchi hii nataman mda wangu wa Urais uishe nikachunge mbuz chalinze n.k
 
emmanuel haya ni mawazo yako ila kwa taarifa yako na kwa kuwa husomi magazeti ningekushauri uanze kusoma uangalie jinsi wabunge wa ccm wanavyopokelewa majimboni na kuchangiwa fedha za kugombea tena. ninyi mnazunguka na chopa mnakusanya watu wanaoshangaa chopa mnajiaminisha kuwa mtaing'oa ccm madarakani. inawabidi mjipange haswa kwani ajenda hizo ulizotaja wananchi wameelewa ukweli kwamba serikali sio fisadi bali mtu mmojammoja ndio fisadi, rasimu wameisoma na kuielewa na wataipigia kura ya ndiyo, mahakama ya kadhi waislamu wameeleweshwa namna mchakato ulivyo na wameelewa. mimi nadhani tusiandikie mate wakati wino ni oktoba 2015. tusubiri tutajua mbivu na mbichi

Mnakusanya watu kwa fisi ndo mnapokelewa? Kuwanunua watu kusomba na malor ndo mnakubalika?
Wabunge wa ccm kuwaandaa wakinamama wa ccm kuwapa pesa kisha wajifanye wanawaunga Mbunge mkono ili agombee ubunge? Kumbe ni futuh tupu, Kawadanganye Mambulula wenzako wa ukoo wako si Watanzania wanajua machungu kwa nchi hii, mnalala Bungen tu kila kitu Ndioooooooo kibaya Ndiyooooo, pesa zikiombwa huku kwa mjomba mnajisifia na kupigiana makofi hamjui mtazirejeshaje,
Kama unatakwimu vzr angalia Deni la Taifa limefika kias gan? Kila Mtanzania anadaiwa zaid ya 700000 halafu achague ccm tena deni liongezeke atakuwa kalongwa..
 
Mkuu hizi zote ni kazi za chadema usihamishe ukweli kabisa.

Watu wanaojitoa ufaham kama wewe ni wa kupuuza tu! Kwanza kaa huko huko Somalia, mambo ya TZ hayakuhusu kabisa!!
 
Imefanya nini hiyo miiko ya viongozi?

Sio lazima uchangie kila mada! Usipende kujiweka wa mwisho sana, jaribu kuwa mbele kwa kukaa kimya maana sometimes ukimya nao ni jibu!!!!

Unaandika shudu sana dogo!
 
Jambo jingine litakalo iangusha ccm ni kumuengua
(1)Lowasa kwenye urais
(2)Kumdhalilisha Warioba
 
emmanuel haya ni mawazo yako ila kwa taarifa yako na kwa kuwa husomi magazeti ningekushauri uanze kusoma uangalie jinsi wabunge wa ccm wanavyopokelewa majimboni na kuchangiwa fedha za kugombea tena. ninyi mnazunguka na chopa mnakusanya watu wanaoshangaa chopa mnajiaminisha kuwa mtaing'oa ccm madarakani. inawabidi mjipange haswa kwani ajenda hizo ulizotaja wananchi wameelewa ukweli kwamba serikali sio fisadi bali mtu mmojammoja ndio fisadi, rasimu wameisoma na kuielewa na wataipigia kura ya ndiyo, mahakama ya kadhi waislamu wameeleweshwa namna mchakato ulivyo na wameelewa. mimi nadhani tusiandikie mate wakati wino ni oktoba 2015. tusubiri tutajua mbivu na mbichi

Wewe unasoma magazeti gani mkuu? kweli tz kuna vilaza aisee!
 
wapigaji kura wengi wapo vijijini na bado wanaipenda CCM
Mkuu Malipula, kwa taarifa yako, ccm inawapiga kura mijini na si vojijini. Vijijini watu wanaumia zaidi na wamechoka sana lakini pia ulimwengu wa sasa ni wa sayansi hivyo taarifa zote ziko kiganjani mwa mwana kijiji.
 
(21)Kung'oa watu kucha na meno bila ganz,
(22) kuwaambia watanzania wasiotaka kulipa bili ya umeme mpya watumie vibatar,
(23) Asiyetaka kulipa nauli mpya ya kivuko apige mbizi,
(24) watanzania wapigwe tu hatuna jins maana tumechoka,
(25) nimetochoka na nchi hii nataman mda wangu wa Urais uishe nikachunge mbuz chalinze n.k

Mkuu hiyo ya kwanza (21) kuna hospital wanag'oa watu meno na kucha bila ganzi?
 
mambo hayo bwana emmanuel 1976 ndiyo yatakayo wanyima kura chadema na ukawa yao kwani sisi wananchi wapiga kura tumeshabaini ninyi ni watungaji wa uongo tu mkisaka tonge..hamna cha huruma wala kitu chochoite kwetu
Tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini CCM imekuwa ikikabiliana na changamoto kali kutoka vyama pinzania wakati wa chaguzi isipokuwa uchaguzi wa uliomweka madarakani Mh. Dr. Jakaya Kikwete mwaka 2005 ambao angalau ulikuwa na unafuu. Watanzania wamekuwa wakilalamikia baadhi ya mambo ambayo wanadhani yalihitaji marekebisho kutoka chama tawala. Wamekipa muda wa kutosha chama tawala ingawa ni kama vile sikio la kufa huwa halisikii dawa. Mambo yale yale yaliyolalamikiwa na kupigiwa kelele yameendelea kufanyika ndani ya serikali ya chama tawala.

BAADHI YA MAMBO YATAKAYOING'OA CCM MADARAKANI 2015



  1. Makundi yaliyojenga uadui na uhasama ndani ya chama.
  2. Ufisadi uliokithiri. Hii haihitaji tafsiri.
  3. Rushwa iliyopindukia.
  4. Kukosekana kwa huduma za jamii za lazima kwa wananchi. Mfano; Elimu duni, huduma za afya, nishati ya umeme na maji, nk.
  5. Ukosefu wa ajira kwa vijana wengi.
  6. Mahakama ya kadhi. Hiki ni kisu chenye makali kuwili. Upande mmoja kuna wakristu na upande wa pili waislamu. Walioingiza jambo hili kwenye ilani ya ccm hawakuwa wanaona mbali.
  7. Migogoro ya wakulima na wafugaji.
  8. Kutupwa kwa rasimu ya katiba ya jaji Joseph Sinde Waryoba ambayo ndiyo maoni ya wananchi.
  9. Dai la jeshi la polisi kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia. Dai hili linaambatana na wananchi kubamkikiziwa kesi za uongo.
  10. Dai la udhaifu wa wengi wa wabunge wa ccm kutokusimamia mambo muhumu yenye maslahi ya taifa bungeni badala yake wengi wao wamekuwa watu wa ndiyoooooooooooooo!
  11. Kupuuzwa kwa madai ya maslahi ya wafanyakazi wa umma.
  12. Muungano wa ukawa ambao ni zao la kupuuzwa kwa rasimu ya katiba ya jaji J.S.Waryoba
  13. Kupitishwa kwa sheria ya makosa ya mtandao???????
  14. ​Migogoro ya ardhi
  15. Mengine ongezea

 
Back
Top Bottom