emmanuel1976
JF-Expert Member
- Jun 17, 2011
- 301
- 80
Tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini CCM imekuwa ikikabiliana na changamoto kali kutoka vyama pinzania wakati wa chaguzi isipokuwa uchaguzi wa uliomweka madarakani Mh. Dr. Jakaya Kikwete mwaka 2005 ambao angalau ulikuwa na unafuu. Watanzania wamekuwa wakilalamikia baadhi ya mambo ambayo wanadhani yalihitaji marekebisho kutoka chama tawala. Wamekipa muda wa kutosha chama tawala ingawa ni kama vile sikio la kufa huwa halisikii dawa. Mambo yale yale yaliyolalamikiwa na kupigiwa kelele yameendelea kufanyika ndani ya serikali ya chama tawala.
BAADHI YA MAMBO YATAKAYOING'OA CCM MADARAKANI 2015
BAADHI YA MAMBO YATAKAYOING'OA CCM MADARAKANI 2015
- Makundi yaliyojenga uadui na uhasama ndani ya chama.
- Ufisadi uliokithiri. Hii haihitaji tafsiri.
- Rushwa iliyopindukia.
- Kukosekana kwa huduma za jamii za lazima kwa wananchi. Mfano; Elimu duni, huduma za afya, nishati ya umeme na maji, nk.
- Ukosefu wa ajira kwa vijana wengi.
- Mahakama ya kadhi. Hiki ni kisu chenye makali kuwili. Upande mmoja kuna wakristu na upande wa pili waislamu. Walioingiza jambo hili kwenye ilani ya ccm hawakuwa wanaona mbali.
- Migogoro ya wakulima na wafugaji.
- Kutupwa kwa rasimu ya katiba ya jaji Joseph Sinde Waryoba ambayo ndiyo maoni ya wananchi.
- Dai la jeshi la polisi kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia. Dai hili linaambatana na wananchi kubamkikiziwa kesi za uongo.
- Dai la udhaifu wa wengi wa wabunge wa ccm kutokusimamia mambo muhumu yenye maslahi ya taifa bungeni badala yake wengi wao wamekuwa watu wa ndiyoooooooooooooo!
- Kupuuzwa kwa madai ya maslahi ya wafanyakazi wa umma.
- Muungano wa ukawa ambao ni zao la kupuuzwa kwa rasimu ya katiba ya jaji J.S.Waryoba
- Kupitishwa kwa sheria ya makosa ya mtandao???????
- ​Migogoro ya ardhi
- Mengine ongezea