Mambo ni vice versa(Tutalalaje hapachakucha?),Mjini ni ya vimbweka bado!

Mambo ni vice versa(Tutalalaje hapachakucha?),Mjini ni ya vimbweka bado!

kalooo 25594

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2016
Posts
300
Reaction score
194
Wanajukwàa.

katika kipindi ambacho dunia inaomboleza Kifo cha Baba mtakatifu(Papa Fransco),Taifa linashuhudia mitikisiko ya kisiasa ndani ya vyama( chadema),na vijana wenzetu wanapotea kwenye kelele za mitandao -mimi  Kalooo nimekuja na ujumbe wa aina hii mbele yenu.​


kuhusu kifo cha Baba mtakatifu.
Kifo cha Papa kwa tarehe husika kimeibua hali ya roho iliyojaa mapambano yenye moto wa kweli wa moyo wa huruma na ukombozi,

Wakati huo Duniani watu huomboleza kwa machozi na wengine wanaomboleza kwa neno huko mbinguni maana machozi hufuta uso ila neno hufuta ukimya uliotawala.Kazi kubwa tuliyopewa na Mungu toka mwanzo ni kuziweka roho mkononi mwake(ziwe huru zaidi),Hivyo,kama vile tulivyokuja duniani na tutarudi mbinguni kwa Baba katika siku aijuayo Mwenyezi Mungu.

Dini inasema kabla na hata baada ya kuwa kiongozi na mwalimu wetu(2yohana1),na sasa tutakuwa naye daima kama Mwalimu na mpenda mabadiliko kwa jamii iliyokuwa chini ya ukandamizaji na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe( Daniel9) kutokana na nguvu za jamii ya mambwenyenye.

Kama taa zingine na mwanga wetu wa Muungano wa Tanzania toka siku ya kuchanganya mchanga aliamini katika ukomo wa mateso ya ndugu zake katika Mungu mmoja(Night mystic move-Alpha blond).

Baada ya Msiba nikaona machafuko Kwa waliosisitizwa kuwa wamoja(Kusini sudani,yohana17;21).Afrika isigombane kuwa na majina ila watu wawe chachu ya kutupa fikra mpya,tuweze kujenga jamii yenye kujitambua kwa nini ipo pale pasipo kuwa watumwa wa mawazo yatupelekayo kujiumiza wenyewe kifkra pasipo sababu,upambanaji si utumwa kwa mtu,kitu au kikundi ila ni maono yaliyo sehemu aliyokalia ama dhamira iliyopambanuliwa kwa uwazi na ushahidi, yenye kuleta mafanikio katika njia zake,Tulipo ni njia tu kwanini tuwe kama mbuzi atafutaye kivuli usiku?​

Walioko kwenye Kitambaa cha Muungano,Mkuki wa uhuru na umoja.

1. Fikra ni moto,hazihitaji kiberiti ila ujasiri.​

2. Kiti cha bunge si cheti cha uhuru.

3.Ukombozi si sauti ya wengi ila wale walioamka.

4.Mataifa hufa mara kwa mara kila wanaponyamaza wenye mwanga,Watu hufa mara moja.

5.Mwanga wa kweli haupatikani kwenye sanduku la kura ila pale jamii inapoamka na kujua kweli.

6.Msisubiri ukombozi wa sauti wakati hofu mko nayo rohoni.

7.Na dini inayokufa kabla ya mtumishi wake hiyo inazika huruma kwa Jina la utaratibu.

8.Msiupuuze Muungano,mmepata watu wa kuwasamehe,kuwatawala na Kuwafundisha,Kwa watawala na wanaharakati Muungano bila kuulinda ni kuchoma hadhina za Mbinguni ili ubaki kwenye laana ya kizazi kijacho kuishi bila kujistiri.

Formula ni kama namba na matendo bali leo majadiliano ni kama bahari.

1. Mabadiliko=Nafsi mpya ×Fikra mpya​

Maana hi kuwa kabla hujashinda mfumo ishindie kwanza nafsi.
Unapobadilika basi fikri tofauti na uiguse jamiii.

2. Mfumo(mfumo wa dhuluma=ujinga+uoga)

Mfumo wowote wenye dhuluma hurisha watu na kuwafanya wasielewe nguvu zao.

FOrmula ya kuvunja mfumo huu ni uelewa×ujasiri=mapinduzi.

3.Vice versa Revolution=kujifunza kutoka kwa adui.

Chukua silaha ya adui wako ichukue itumie kwa hekima utashinda.

Mfano Tumia ubepari kuelekea ujamaa wa kweli kwa akili(media,technology,elimu).​

4.Mabadiliko ya jamii=(Elimu+ujasiri)-(mazoea).
Panua elimu, ongeza ujasiri na vunja mazoea potofu.​

5.Ukombozi=(sayansi ya jamii)+(falsafa ya nafsi).
Sayansi pekee haiwezi okoa watu na falsafa pekee haiwezi pia,Ni muhimu kuunganisha Akili na roho katika kuilomboa jamii.​

6.Kiongozi wa kimapinduzi= (unyenyekevu)×(Nidhamu)×(ubunifu).
Unyenyekevu ni kuwa tayari kujifunza kila siku.
Nidhamu uwezo wa kujizuia kwa lengo kubwa.
Mbunifu ni yule awezaye kutafta njia mpya kila siku.


Kauli kuu:Revolution si mapambano ya Bunduki tu, ni akili,roho na sayansi.

Kalooo hakuwa mwanasiasa katika dhamira ila ni kizazi kilichokataa kunyamaza pale njia inapoachwa na watu kupenda kiza kuelekea kwenye makorongo ya mito ya mamba.

Maswali.

1.Mambo yanapotuzidi tunahitaji fikra mpya au uongozi mpya kwenye sehemu zetu?

2.Tukifuate kilichobeba roho au muondo?

3.Je urithi mkuu kwa ndugu na jamaa zetu ni nini?Na tunasubiri lini kuchukua?

4.Kalooo kwa nini anaweza kuwa Muhaini au mwanamapinduzi?

5.Na kama yote mawili amehaini dhidi ya nani na mwanamapinduzi dhidi ya nani?​

6.Kama kuumia tuumie kwa dhamira za ndani yetu
Au za nje(Wote tunaoishi kwa kupumua Hakuna asiyepatwa na uharibifu isipokuwa Mungu asiyeonekana)?

7.Mimi ni nani?Haikuhusu mwandishi ila Kila mmoja awepo katika kwa nini yupo?

Kama tunasimama basi tusisimame tu kwa miguu kama kalooo ila kwa akili na roho kama kalooo ndani yake.Mimi ni wewe,wewe ni sisi.Basi kalooo yupo ndani yenu.

Nimewaita kizazi cha 2085,Ni kizazi cha roho inayotafuta,macho yasiyolala na moyo usiohofia.

Twende tukalime fikra zenye tija tukavune matendo ya kimapinduzi.

Tusijenge nchi mpya kwa Tofari ngumu ila kwa roho zilizounganishwa.

Tumejifunza kuandamana mitaani kwetu ila hatujajifunza kuandamana na nafsi zetu.


Nia yangu kwa Wakombozi.

Ukombozi hautangazwi na radio,wala hauhifadhiwi na chama ila akili kutoka ndani inapotuamsha kama jua linalochomoza bila ruhusa ya serikali.

Mji mjini ya mawe hauko kwenye ramani kwa sababu msingi wake umeteleza kiroho.

Mambo ni vice versa na kifo cha mfumo ndo uzima wa nafsi.

Vice versa isiwe msimamo bali mapinduzi yenye msingi wa maono.

Yachukueni hayo yafaa kwa kesho yenu ni njia dhidi ya upinzani wa nje.

Na kalooo 25594 ni funguo ya 2085 kuithibitisha kazi iliyokuwepo inaendelea.

Kalooo ni zaidi ya mtu,Ni wazo,ni mwamko wa kutafakari na kuamka.

Mapinduzi tukayafanye baada ya kimia kingi chenye busara, kuliko kelele za mwishowe kuamuliwa na kutii, funga mdomo wako.

Utalalaje kama umetelekezewa alfajiri na watu ambao still wako tungi na mambo yao?.Ukifanywa hivo umeumbwa ili uilete alfajiri ya mambo yao.Ni sononeko maana Maji ya matumaini yanamwagika usiku wa machungu.

Nawasilisha japo duniani si kila kitu kinaonekana kama kilivyo.​

Quotes

1. Mtu anayejimiliki nafsi yake hamilikiwi na dunia.From Mimi ni nani kwenye Siri ya 2085

2. Maendeleo ya nje hayazibi pengo la uchochoro wa akili iliyolala.Mambo ni vice versa-Afrika bado Hapajakucha.

3.Mapinduzi ya kweli hayatangazwi kwa kelele huanza moyoni kama siri ya umeme kabla ya radi,itifaki,sheria na demokrasia.

4. Aliyejua jina lake halisi ameikomboa Jamii.Mimi ni nani no siri ya 2085.

5.Vyeo visivyotumia mtihani ya dhamira havidumu mbele ya historia,ukuu wa mlaji wa vijiji inahusu.

6.Afrika haitainuka kwa miguu ya Wageni bali kwa kujitambua kwa wanawe.vice versa na mapambano ya kiakili ni vita.

7. Kuhusu wakati ujao,2085 si mwaka bali ni kengele ya nafsi,ikilia katika wale waliolala katika heshima ya uongo.

8.Mwafrika aliyesahau jina lake huyu amekubali utumwa wa fikra,Mimi ni nani ni Siri ya hatima.

9.Uhuru wa afrika haujaandikwa katika mikataba ya majumba ya kimataifa ya heshima tunayoyapigia magoti ila umchorwa katika damu za watu walioamka,mambo ni vice-versa,Hapajakucha usilale mwaafrika.

10.Afrika haitashindwa kwa mapanga,itashinda au kushindwa kwa silaha za Akili.Itifaki,sheria na demokrasia,Kwa Karl Marx, democracy is road to socialism.

11.Uongozi wa Afrika ya kweli hautavaa Tai ya ubepari bali moyo wa wenye njaa ya haki.Vice versa huenda na mapambano ya kiakili.

12.Tunasalimiwa kwa Jina la Jamhuri,basi sisi si vizuka vya historia,ni waanzilishi wa dunia mpya kwa Jina hilo la Afrika.mimi ni nani? Je ni Siri ya 2085?

13.Tuna Majaliwa, hatujajaliwa kubebwa na mataifa,tumepangwa kujibeba kwa Jina letu wenyewe.(vice versa na maisha baada ya mapinduzi ya fikra.

14.Anayejua chanzo chake hajali maji ya mto wa dunia yanavyojaa.

15.Mapambano yasioanzia ndani ni kivuli cha mapambano ya watu wengine.

16.Kujitawala wenyewe ni utawala wa kweli mbele ya mabilioni ya vishawishi.(Itifaki ya mwisho iwe kuondoa woga).

17.Afrika itajengwa siyo kwa mabati ya misaada bali kwa matofari ya uhuru na umoja(mambo ni Vice-versa)

18. 2085 ni ishara,binadamu atajenga dunia mpya au ataangamia kwa usingizi wa kiroho.(Mimi ni nani siri ya hatima yako).

19.Mtu hujikomboa kwa kujitambua,kukataa kufungwa na vyeo/per diem,na kuondoa hofu ya kupoteza vitu vya dunia.​

Mathematical proved.

Ukombozi wa nafsi=kujitambua+kukataa mifumo ya kidunia-Hofu ya kupoteza.

20.Taifa linajengwa siyo tu kwa maendeleo ya nje bali kwa jamii inayojua asili yake na jamii inayofikri kwa uhuru na kuishi katika maadili yake.

Here mathematical formula.

Taifa imara=(Jamiii inayotambua asili yake)+(uhuru wa kifkra)× maadili.

21. Kama unataka kujua 21 April ni mwanzo wa siku ndani ya mwaka mpya basi ni hiyo ishara ya asubuhi ya 2025,Ni mapinduzi ya kimia kwenye nafsi iliyoamka kutoka kwenye kulala na kupaa mbinguni kwa vitendo vya ndani mbele ya macho ya watu wa dunia yote.Wapo wanao subiri na kuona hayupo bado ijumaa kuu kuna kitu walimisi,wanachosahau ni kuwa uwepo ni wa majira yaliyopo katika utimilifu.

22. Kinachonishinda mimi ni hiki,kujisimamia akili na Tabia yangu binafsi,nicheke tu kama wewe siyo kiongozi,nje na hayo kinyume hiki kitakuhusu, kikaragosi changu.

23.Picha nayo bendera,usiifanye movie akili yangu,uapdate kipande kipande nisijue picha kamili ya bendera yangu,mimi kuwa kama picha  inahusu?

24.Kila nafsi ni molekuli,inabadilika kwa joto la majira na shinikizo la wakati.(vice versa is true).

25.Ningekupa doti ya kanga anti,au wewe dada;Naogopa kwa kujua ukweli kwamba maisha si bidhaa ya bahati,ni athari zinazopikwa kwa mabadiliko ya ndani,yanayopikwa kwa uvumilivu na maabara yako ya moyo.Hiyo ndio wao ya upo shoga angu.

25.Kama tunakwenda twendeni,Lakujua kwanza ni hili,Hakuna uhuru usiohitaji kemikali ya maumivu,kila mapinduzi ni mmenyuko wa nafsi dhidi ya dhuluma.(itifaki na nafsi ya uhuru).

26. Kuhusu kujifunza kwa kalooo,nimekuwa asidi isiyosawazishwa nahitaji kichocheo cha ukweli kuleta mabadiliko yenye maana.(Sasa Nitaiweka uvunguni sura na roho yangu wakati Makutano ni maisha na Fikra?Nyinyi kama mnatangulia tangulieni,huko nako ni dunia mtakutana na watu kama mimi huyu).

27.Chekeni mtakuja jua:mtu akiwa na nafsi tulivu akakumbwa na matatizo ya dunia kwa muda mrefu atachukua hatua ya kujikomboa,Cha ajabu muda huo nyinyi bado mnamcheka.Na mtu having animals na alivyo zaliwa.

Tuone chini hapa

Physics;To every action there is an equal and opposite reaction.

Nafsi tulivu+matatizo ya dunia reaction ifanyike ndani ya muda=uamzi wa ukombozi.

28.Kujenga taifa la watu huru kunahitaji wanaojitambua+ kuwa na Dira moja.

29.Viongozi wa kweli hutokana na watu wanaojitambua na kuvumilia matatizo mpaka wanazaliwa kama suluhisho la jamii.

30. Kama mtaenda kuchumbia basi mrembo wangu asiwe na ngozi ya maua,mwambieni kaka Gwajima aniletee sauti ya Moyo ulio huru,Nitalala milango wazi kwa ridhiki ya huyo mwenzagu,nitaondoka nyumbani na bado nitakuwa mmoja na jasusi la mbinguni.

31.Mwanake anayejitambua ni Suluhu kwa Taifa jipya,Mwenye uzuri wa nje bila akili atakwaruzwa naye hata na kivuli chake.

32.Ukipenda uso wangu ni sawa na kununua hewa,Ukinipenda ndani basi Karibu bila malipo dunia mpya tuungane tusherekee na tuimbe pamoja kuzifurahia nyakati zetu.

33.Ningekuwa mwanamke leo nisingeeleweka hata bure,maana wengi wanatazama kwa macho na kushindwa kuona udongo wa Muungano wa wapendanao.Muhimu kuwaambia uzuri wa ngozi tutashinda kwa muda ila uzuri wa roho tutabaki washindi wa milele.

34.Nimeandika,Lazima tumtafute adui wetu kila kona kwa silaha za ndani kwanza ndo tuje za nje,Kumchukia ni kuhakikisha dhuluma hifanyiki mbele za macho yetu.Tuipende kweli,Nafsi ipendayo kweli huvunja mpaka ngome za karne.

35. Wakati silaza za Atomic zinazidisha madhara katika kujikomboa kwa mataifa,midundo ya mziki huamsha hisia za mapambo kwenye mioyo ya watu waliokata tamaa.Tega sikio usikie sauti ya ndani yako uimbe vizuri.​

KAMATI KUU

1.ujumbe wa kamati kuu si kutafuta vyeo,ni kutafuta mizizi ya haki,utu na maendeleo kwa wote.

2.Mwanachama wa kamati kuu anatakiwa awe na bidii siyo bendera kifuata upepo wa masilahi binafsi.

3.Kamati kuu ni moyo wa mabadiliko,ukidhoofika mwili wote wa Taifa huanguka.

4.Ujumbe wa kamati kuu unatakiwa ubebe lawama ya makosa ya wengi na ushindi wa jina la wote.

5.Sauti ya kamati kuu inatakiwa iwe ya kweli,siyo kuwahadaa waliojikatia tamaa.

6.Kamati kuu si mahali pa kuogopa ukweli,ila ni kurudisha ukweli uliopotelea njiani.

7.Aliyebeba kamati kuu bila uadilifu wa kimaono,ameitelekeza nchi na vitukuu vyake kwa maangamizi bila kupiga risasi.​

MKUU WA KAMATI KUU.

1.Hataki uasi wala uhaini,kaa kama upinde wa mvua ukikutanisha mawazo tofauti kwa kuleta nuru ya Taifa pamoja.

2.Uenyekiti si ufalme wa hofu,bali wewe ni usukani wa matumaini unaoelekeza jahazi la Taifa hili.

3.Ukiweza,weza kusikiliza sana kuliko kuamuru,kwa maana nguvu ya uongozi iko kwenye masikio makini kama mbuzi beberu aishivyo kuinasa sauti inakotokea.

4.Nguvu ya mwenyekiti haipo katika kukandamiza hoja,bali kuyahuisha mazungumzo ya haki.Kila chama kina haki yake kwa muda wake,Kucheza ni baaada ya kutambua muda waga upo wa kutesa kwa zamu kwa kila kundi.

5.Mwenyekiti wa Kamati kuu ni Mwanga wa giza si kivuli cha woga wa mabadiliko.

6.Mwenyekiti huongoza kwa sauti tulivu na kwa ushahidi wa Tabia na uaminifu wa moyo.

7.Neno la mwenyekiti ni mahiri, kama mbengu linapopandwa kwenye moyo wa Taifa lenye udongo mzuri ulio karibu na maji.

8.Uenyekiti si kiti cha kifahari,ni dhamira yenye upenyo wa upeo mkubwa hata kwa ajili ya kizazi kisichozaliwa bado.

9.Na mwenyekiti akikosa maono Taifa Zima huyeyuka kama mishumaa iliyokatika kamba.

10.Na mwenyekiti asiyesema ukweli wa kujua misingi ya viongozi,uongozi na Taifa,amezamisha kizazi kizima bila kupigana vita.

Inner revolution ni uhuru, moja kati ya mawili mtu atachagua,kuja au kuondoka,kusafirisha au kuzikia hapa hapa.

Mpaka hapo,Asanteni ya kwangu ni hayo,Naomba kuwaacha na Professor Hapo chini.​
 

Attachments

  • 21f11ab8286a5d73288367afa7174f47.mp4
    5 MB
  • Hotuba yangu kwa Taifa hii leo kuelekea Miaka 61 ya Muungano(MP4).mp4
    45.6 MB
  • 67684a99792e0b92012a7307eeec11aa.mp4
    8.4 MB
  • congoinsa_20250319_23.mp4
    37.7 MB
Irie EYE !

Sasa, Tayari Papa kachukua jina la 'SIMBA' ... (Pope LEO XIV)

Ufalme_Nguvu_Utukufu.png


AMERIKA hata AFRIKA 001

Kazi ni kwa UMMA--Kuuvaa Usimba!

Ukadinali_2025_na_Kupita.png


MATRIKSI KUTOKA : UFUFUKO NA UZIMA

== Mguso wa Malaika : Kumbukumbu la Miongozo ==​


Katika mapokeo ya Ukristo, ‘Hekima na Uhuru’ ni fanusi ya ‘Mapaji ya Roho Mtakatifu’. Kiufundi, pasipo kumumunya maneno, usanifu wa vielelezo vya mbegu za utu na ustawi – utu na ustawi wenye uimara na tena uthabiti, ni matunda ya kazi ya ‘Utaasisi wa Dini’--kote hapa Duniani.


Hili lafanya, SUBIRA KUWA NI IBADA, hata kwa kule kupanda mbegu ya mashauri ya Uadilifu, Maadili na Miiko ya Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu kwa Mataifa/Wanamataifa kama ‘Dola/Nchi-Dola’. Ni wanajamii wenyewe wanaoamua ni lini ‘IBADA’ hii inafika mwisho, ikiwa kuna mwisho, kwa kufumbua macho yao na akili zao ili wabaini KUBU NYEUSI za MATRIKSI—wakati mmoja hata mwingine.


Hekima ni ‘Mama wa Akili na Utambuzi’ inayofanyika katika Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu ya mwanajamii – mwanajamii mwenye moyo safi na akili isiyo na mawaa/kasumba. Kuwa ni ‘Mama wa Akili na Utambuzi’ ndiko hufanya ‘Roho Mtakatifu’ kuwa ni ‘Matriksi’ inayobeba na kustamilisha ‘Matriksi Zote’ za Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu.


Hili lafanya ‘Moyo Mkuu na Shauri’ ndicho kile kile katika Utaasisi wa Dini, mapokeo ya Ukristo, kimeleta Shauri la ‘Maria Mtakatifu, Mama aliyejaa Neema’… Kwa kuwa, YUNIAAMU yote, kiufundi, ni ‘Tumbo la Uzazi’ kwa maumbile yenyekufuzu Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu…


Mwanajamii/Mtu/Mja mwema yeyote hufanyika ‘Hekima’ anapokuwa na utayari wa ‘Kupokea Shauri la Nguvu na Neema’… Kwenye Mapokeo ya Ukristo ni ile Dhamira na Nia ya Kujaa Neema : Mambo ya “Nitendewe Ulivyonena, Mimi ni Mtumishi wa BWANA” : Unyenyekevu…


Siri ya Unyenyekevu ni kustahili ‘Uzuri na Nguvu ya Kimashauri’ kwa ajili ‘Utume/Utumishi’ kwa/miongoni mwa ukundi wenye ‘Matriksi Moja’ ya Miundo ya Utendaji, Utamaduni na Ustawi. ‘Uzuri na Nguvu ya Kimashauri’ unaweza pia ‘kumuweka mtu Huru Kweli Kweli’ hata akauzidi ule UMAUTI wa KUBU MOJA ya Fahamu na Mafahamu—Mambo ya ‘SASA’ na ‘SAA YA KUFA KWETU’…


Dhamiri na Nia’ ni ufunguo wa Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu kwa SHAURI KUU lililo ni UFAHAMU KRISTU. Hili lafanya Uhusiano wa ‘Roho Mtakatifu’ na ‘Ufahamu Kristu’ upo kwenye ‘SHAURI KUU’ kukadirisha muktadha akilifu wa ‘UTATU’; ambavyo Roho Mtakatifu ni ‘Hekima’ na ‘Shauri’ linaloishi na kuongoza NIA za Kiakili na Utambuzi kwa ‘Mja Mwema’. Neno ‘Filosofia’ ni lenye etimolojia ya umaanishaji wa tafsiri ya kwamba : ‘Mpenzi wa Sofia’; ambavyo ‘Sofia’ ni ‘Mama Mjuzi kwa Maarifa na Maarifu ya Uzima’--mwenye kuelea fahamu na mafahamu kwa ajili ya ‘UKWELI’ na ‘UZIMA’ wa Mambo...


Jitihada katika ‘Maarifa na Maarifu’, katika nasibu ya mapokeo ya Ukristo, ndiyo kiufundi hufanya ‘Nia ya Kristu’ kuwa ni Maisha na Kujichagulia katika SUBIRA; subira ya ‘Kufanyika Sawa sawa na Mapenzi ya Mungu-BABA’. Hili lafanya Ibada ni dhana kwa ‘Matamanio ya Upatanisho’ wa ‘Mapenzi ya Mbingu’ na ‘Nchi’ ili kusudi ‘Mbingu na Nchi’ vijae ‘Utukufu wa Mungu-BABA’. Subira ni fanusi ya kiutendaji kwa ajili ya ‘Muafaka’ wa Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu ambavyo ‘yale mazito na magumu’ ya nchi yanageuka kuwa ‘mepesi na malaini’ kwa ‘Uhuru’ na ‘Pumzi ya Uzima’ ili kukadirisha ‘Imani, Tumaini na Upendo’ --Mambo ya (1) Ukombozi na (2) ‘Kukombolewa na Dhambi/Mshahara wa Dhambi/KUBU NYEUSI’…


SASA-NIA ya UTU ni dhamiri kwa ukombozi kwa vina vya tafsiri vyenye kuleta ukomo wa kiutendaji na mageuzi ya ‘Sura na Mienendo ya Jamii’ ama hata pia ‘Matriksi’ kwa huu ‘Ugumu wa Kimatiriali’ wa (1) Supasha na (2) ‘Mambo ya Nyakati’. Mageuzi ya Kijamii kiutamaduni na ustawi ni jambo lenye ‘kungojea’ kwa kuwa Usentienti wa jamii ndiyo unaoweza kushikilia ‘Utukufu’ na ‘Ufalme’ kwa kudumu ikiwa tu ‘Nuru na Mwangaza’ kuwa na kina hata katika mazingara ya mazingira na pia ‘Nia za wengine’ zilandane na Nia ya Shauri Kuu kutoka katika wale wenye ‘Mioyo Safi’.

== Kuishinda Mauti : Wimbo Haleluya! ==​


Kutokuwepo kwa koherensia ya ‘dhamiri na Nia njema’, miongoni mwa wanajamii, ndiyo daima ni uwanja wa ‘vita vya kiroho’ ambavyo wale wenye ‘uwingi’ katika ‘mapotofu’ ya kimaadili, uadilifu na miiko hufanya ‘vishawishi’ vya ‘kuharibu dhamiri na nia’ za wachache wenye unyoofu na mapenzi mema—jambo hili ni yunivasali, iwe Duniani ama kokote kule kwenye Sayari. ‘Vita ya Kiroho’ ni adha ya m(i)fumo yenye kuvuruga uwezekano wa SHAURI KUU linaloanza na mbegu ya u-JUA-ji katika miongozo ya Uhuru-Udugu-Haki-Amani ili ‘Karma’ isikinge wanajamii kutaamulika Kiroho kwa ajili ya ‘Dhamma’.


Hili ndilo lafanya ‘Yantra Dhamma’ kuwa ni ufunguo wa SHAURI KUU kwa ajili ya ‘HUKUMU’ katika kipindi hichi cha robo ya pili ya Karne ya 21, (2025-2050); ili ‘Wanajamii wenye Mioyo Safi na Unyenyekevu’ wawe ni ‘Waja Wema’ wa ‘Sala na Kazi’ – sala na kazi kwa ajili ya kutengenezea ‘koherensia ya Dhamiri na Nia yenye kina cha kutosha’ kufanya mageuzi ya ‘Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu’ kwa ‘Waja wote wa Dunia waliobakia’. Nyenzo ya ‘Kiakili’ kwa kuwa ‘Mapaji ya Roho Mtakatifu’ ni sifa na hadhi ya akili na utambuzi kwa (1) Hekima, (2) Shauri, (3) Elimu, (4) Nguvu, (5) Ibada, (6) Kumcha Mungu, na (7) Akili Yenyewe.


Kinachoweza kupatanisha ‘Dini’ na ‘Dola’ ni ‘Uakili na Utambuzi’ wenye kitovu katika ‘Mapaji ya Roho Mtakatifu’; kwa kuwa ‘Usahihi wa Kimfumo’ ni jambo lisilo kamilifu kwenye ‘Utaasisi wa Dini’ vivyo hivyo kwenye ‘Utaasisi wa Dola’--kuhitaji ‘Mwanzo penye NENO’: NENO LA UPATANISHI ilivyo ni ‘Mti wa Uzima’. Kwa nyezo akilifu ya Trizaniamu, (x) Uweza-Utayari-Umahiri wa Wanajamii unafanyika kuiva kwa ajili ya (y) Ufalme-Nguvu-Utukufu.


UWEZA: Huu unayonafasi bora na njema ikiwa (x) ‘Akili’ na (y) ‘Hekima’ vinatawala Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu wa Mwanajamii. Hili lafanya unyenyekevu wa Kiakili kwa Ujuaji wowote wa mambo uwe na nasibu ya mapana-marefu-kina-kimo cha ‘UPENDO MUHIFADHI’ kwa Maarifa na Maarifu ya Kiakili kiufahamu na Mafahamu. Akili pasipo hekima ni Jamvi la Elimu 1.0; na hali Akili katika UPENDO MUHIFADHI ni ‘UFAHAMU KRISTU’--kwa Trizaniamu, Uono na Ufikirifu mifumo hufanya Elimu 2.0 kuhusiana na yote ya fahamu na mafahamu.


Kwenye Mapokeo ya Ukristo, Hekima ya Kimbingu ni ‘Dawa’ kwa ‘Akili na Roho ya Machukizo’ ambavyo wokovu kutoka kwenye ‘Ulimwengu wa Dhambi ya Asili/Laana’ huja kulingana na ‘NEEMA’ na wala si ‘ukamilifu’ wowote wa kimatendo ama sifa za kupimika na uwezo wa kibinadamu. ‘Kujikabidhi’ kwa ‘Roho ya Mazazi Bora’ ndiyo nasibu ya ‘Kuumbika Roho safi’ ili kufundishwa na kufundishika yale yaliyo ‘Mema’ na kukadirisha ‘REHEMA’ na ‘NEEMA’.


‘Roho ya Mazazi Bora’ ni mama wa Hekima (Sofia/Maria), Unyenyekevu na Utumishi: asili khasa ya shauri la MATER BONI CONSILII (Kilatini) : Mama wa Shauri lililo Jema


Kiufundi, ‘Shauri Jema’ ni Ufunguo wa Imani na Matendo yote; ambavyo katika ‘Dola’ hakuna msingi wowote wa hakika la hili isipokuwa matumaini kwa ‘Haki na Wajibu kwa Uraia Mwema’ kupitia ‘KATIBA’ na ‘ELIMU’.


Ujamhuri, Utamaduni na Maendeleo kuwa na hatma yenye kutegemea ‘Mwangaza wa ELIMU’ dhidi ya Ujinga. Maradhi na Umaskini ambavyo (1) Ardhi, (2) Watu, (3) Siasa Safi, (4) Uongozi Bora; ni vigezo empirikali kwa ‘Imani na Matendo’ ya ‘Wananchi’.


UTAYARI: Huu hufuatia uwepo wa (x) ‘Shauri Jema’ na (y) ‘Kumcha Mungu/CHANZO’ kwa ‘dhana Imani’ ya kwamba CHANZO/Mungu ni kitovu cha Uweza wa Kufanyika Yote/Chochote ilivyo ni ONTOLOJIA YA TAASISI. Kumcha Mola/Mungu/CHANZO ni nidhamu ya kujichagulia, maisha na kujichagulia – kuwa ni nidhamu ya ‘Shauri Jema’ ikiwa Mtu anayoimani ya Chanzo cha Ushawishi Mkuu wa asili ya UTU wake na tena basi chanzo cha Fadhili, Rehema na Neema zote. Jambo linalojenga msukumo wa kimaisha wenye kutafuta uadilifu wa Imani na Hakika ya Shauri lenyewe.


SASA, si kila mwanajamii analazimika kusadiki ama kuamini juu ya Shauri la Mungu/CHANZO; kwa kuwa asili ya ‘Matriksi’ ni ‘fumbo la imani/kuzimika data’ ili ‘Kujitafuta’; ambavyo kwenye ‘Dola’, Kikatiba na Elimu, hili hulazimu uwepo wa ‘Shauri la Uhuru wa Kuabudu’ ama ‘Serikali na Tawala ya Ushawishi wa Dini fulani iliyo Rasmi’.


Kionjo cha ‘Mungu Ibariki’ katika Utaifa. Nchi-Dola, huwa ni ‘Shauri la Kukopa kianzio’ cha ‘Imani ya Udugu na Haki’ kwa kuwa ‘Dola pasipo UTU na Imani’ ni jamvi holela isivyo umadhubuti wa makusudi ya Mraba wa ‘Matukio-Jamii-Machaguo ya Kitaasisi-Wakati’. Inaweza kushangaza, Dola zote thabiti zimeasisiwa na watu wa Imani kali juu ya UTU na Utamaduni; jambo lenye chachu ya ‘Imani kwa Mungu’ ama ‘Maadili ya UTU na Misimamo fulani ya Kiroho’.


Kiufundi, uasisi wa Nchi-Dola ni jambo moja—kuendeleza ‘Shauri Jema’ ni jambo jingine. Ili Utaasisi wa Nchi-Dola ulioasisiwa kwa ‘Shauri Jema’ udumu na kustawi huhitaji ‘Watu wa Wajibu na Mwangaza Bora’ kwa ajili ya kudumisha ‘Hekima-Umoja-Amani’. Hili lafanya Uadilifu, Maadili na Miiko kwa ajili ya ‘kulea taifa changa’ ama hata kuliendeleza ‘taifa lililokomaa’ ni tunda na kazi ya ‘Matendo ya Mitume’.


Kwenye kusuka na kuendeleza Dola, ‘Matendo ya Mitume’ ni nasibu ya Utekinokrasia na Meritokrasia, ikiwa hakuna haya mawili siasa za nchi yeyote ni uwanja wa fujo za madaraka na maslahi ya mtu ama vikundi vya watu kwa kutafuta kunufaika na mifumo isiyo sahihi ya ‘Jamii-Utamaduni-Maendeleo’--vyovyote vile ambavyo dhana ya ‘Maendeleo’ itakavyoteka nyara ukweli wa ‘SHAURI JEMA’ kwa ‘Mapenzi ya Mali/Pesa/Umaarufu’.


Utekinokrasia na Meritokrasia katika jamii hutegemea Utayari wa Wanajamii kulitumikia ‘Shauri Jema’ -- kutegemeana na Usentienti wenye Dhamiri na Nia ya (1) ‘Kuitika Wito’ na tena kuwa na (2) ‘Mioyo yenye nasibu ya Kujituma’. Ikiwa jamii inamwelekeo mbovu wa mifumo na ustawi, daima shida ipo kwenye ‘Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu’ ya wanajamii wenyewe kwa kuwa hata viongozi wowote/watu wa madaraka ni muakisiko wa udunya ama u-JUAJI kwa UKWELI KHASA WA MAMBO.


Uongozi ni Ushawishi; na Uongozi wa Jamii ilivyo ni Ontolojia ya Taasisi ni kutafuta ‘Usahihi wa Kimfumo’ kwa ajili ya ‘Mapana ya Jamii’ – ikiwa ni kweli khasa ya kwamba wanajamii wenyewe ‘wako tayari’ kushawishika na ‘SHAURI JEMA’.


Katika Mapokeo ya Ukristo, Utayari wa Kushawishika na ‘Shauri Jema’ ni fanusi ya Kiutendaji ijayo na dhamiri na nia, ilivyo ni Usentienti: “NIPO HAPA SASA, NITUME MIMI BWANA.” Kuwekwa kwa lugha ya kilatini kama ECCE EGO, DOMINE.


Katika Nchi-Dola, Uibilisi ni ‘Roho ya Ukafiri’ kwa kutozingatia SHAURI JEMA, kama lipo kikatiba, na kutumia kanuni za ‘Misitu ya Mioyo Iliyopotoka’. Hili daima linasawazika kwa ‘Sala na Kazi’ kwa ajili ya kuwafundisha wakosaji njia zao na kutengeneza ‘mguso wa kiroho’ ndani ya wale walio na ‘mioyo iliyovunjika na kupondeka’. Nasibu ya Ujuzi na Uweza, unaopitiliza ‘Siasa za Nchi’ na hata ‘Elimu ya Kawaida’ katika Jamii yeyote ile.


UMAHIRI: Huu hudhihiri palipo na (x) ‘Elimu’ na (y) ‘IBADA’ kwa kuwa muktadha akilifu wowote wa miundo ya utendaji na matendo yenyewe, mwenyekujua ilivyobora hutenda ilivyobora. Matunda ya Kazi hufunua ukweli wa ‘Roho ya Shauri’ ambavyo ‘Kazi yenyewe ni Moyo’ pale ambapo mwanajamii anayodhamiri na nia kwa ‘Shauri Jema’. Ni ‘Subira’ kati ya ‘Kupanda’ na ‘Kuvuna’ huja kukadirisha ‘Ukweli’ wa ‘Shauri Jema’ kwa kuwa Ushawishi na Matendo hujenga Taasisi/Utaasisi na khasa utabia ukiwa na kawaida ya kuenenda kwa ‘Shauri Jema’.


Kuenenda kwa ‘Shauri Jema’, kwenye mapokeo ya Ukristo ni ‘Shika Neno, Tenda Neno’ kwa ajili ya ‘Mapenzi ya Mbingu/Mungu BABA’: ‘Hekima ya Kimbingu’ kuhusu Imani, Tumaini na Upendo ambavyo kiibada ndilo jambo la ‘UPUMZI MATRIKSI’ wa ‘Nguvu ya Ufahamu na Mafahamu pamoja na Watakatifu Wote jinsi UPENDO KRISTU ulivyo upana, na marefu, na kimo na kina'


Kiufundi, UFAHAMU KRISTU/UPENDO KRISTU ni ‘NGUVU’ na ‘Ibada’ ya moja kwa moja ya Mwanajamii yeyote ‘Mwenyemoyo wa Unyenyekevu’ kwa fanusi za Kiutendaji; ambavyo jambo hili ni yunivasali – iwe Duniani, ama Kokote kwenye Jamii na Ujamii wa Viumbe vyenye Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu.

== Ushuhuda wa Imani-Uhuru : Roho ya Ushindi ==​


Dini ni Mbegu ya Utamaduni ambavyo ‘Mashauri’ hutengeneza ‘Miongozo’ na ‘Kanuni’ za ‘Utabia wa Kishirika’ wa wanajamii walengwa—muktadha akilifu wa (1) ‘UPENDO’ ama/na (2) ‘MTENDEE MWINGINE VILE UNGALIPENDA WEWE MWENYEWE KUTENDEWA’ katika ‘Dini’ ya Jamii yeyote Duniani ama kwenye Sayari nyingine ni ‘SHAURI JEMA’ kwa nasibu ya Ufahamu Kristu.


Hili la UFAHAMU KRISTU/UPENDO KRISTU ndilo ‘fumbo la Imani’ kwa Ontolojia ya Taasisi ilivyo ni ‘Kanisa’. Kiufundi, kanisa si ‘majengo’ wala ‘ukundi wa kusadiki hili ama lile’; na wala si lile shauri la urasmishwaji wa ‘dogma’ na ‘mafundisho’; kwa kuwa vitu vyote vya namna hii vina nasibu ya mambo mawili kwa wakati mmoja (1) Nyenzo za Ufunguo kwa ‘Ufahamu na Mafahamu’, (2) Vizingiti kwa Mafahamu na Ufahamu; kutegemeana na ‘Elimu’, ‘Upeo wa Akili’ na ‘Mazingira ya Visomo, Siasa, Sayansi na Tekinolojia’.


Hili lafanya ‘Shauri Jema Fulani na tena muhimu Sana’ katika kipindi hichi cha 2025-2050…


‘Mapaji ya Roho Mtakatifu’ si ‘dogma’ wala tuseme ‘urithi wa Wawakristo’ na ‘mambo ya Wakristo’… Ndiyo ni ‘bahati nzuri/mbaya’ kutegemeana na uwezekano wa‘Kasumba’ zetu kwa wakati; kwa kuwa ‘Mapaji ya Roho Mtakatifu’ ni ‘Sayansi 3.0’ kwa ‘Wafikirifu Mifumo’. Ku-JUA ilivyo bora kuhusu jambo hili ndiko kunakwenda kutatua vigugumizi vingi hata ndani ya ‘ushirika wa kiroho’ kwa uhifadhina wa mapokeo ya Ukristo.


UJASIRI, DHAMIRI na NIA NJEMA ndivyo vitakavyoleta UMAHIRI na UWEZA wa kumudu mabadiliko ya kijamii na Mageuzi ya Kiroho – bidifu kwa ajili ya ‘Ustabali wa Jumuiya ya Kimataifa’ katika kipindi hichi cha ‘HUKUMU’; kwa kuwa ‘Sala na Kazi’ katika ‘fanusi za Kiutendaji’ zinakwenda kuamua hatma ya ‘Ulinzi na Usalama’ wa Usovereini wa Jamii na Ustawi wa Wanadamu, Mazingira na Mazingara ya Sayari yetu ya Dunia.


Dunia yetu tayari, kwa muda mrefu sasa, imeshaingiliwa kisiasa, uchumi na utamaduni na wanajamii kutoka Sayari Nyingine Mbalimbali kutoka hata nje ya Mfumo wetu wa Jua—namna isiyokuwa ya wazi; kwa namna zenye kuhatarisha hatma za maendeleo ya kweli na ustawi wa kibinadamu. Jambo pekee linaloweza kutengeneza UWEZA-UTAYARI-UMAHIRI wa wanajamii hapa Duniani ni ‘Kuamka’ na ‘Kuzichunga Dhamiri Zao’…


Hili ndilo lafanya ‘UFAHAMU KRISTU’ kuwa ndiyo ‘Ngao na Mkuki wa Jaala’ kwa ajili ya kujihami na kujitetea Usovereini wa Maisha na Kujichagulia pasipo ‘Kupangwa na Wengine’ wanaotoka nje ya Sayari ya Dunia yetu – wanaotoka huku na kule na tena, kwa hila/njama, wakishirikiana na wanadamu wenzetu wachache hapa Usoni Duniani wenye ‘Roho-ya-Utaka-Vitu’.


HUKUMU ni jambo lenye kukadirishwa na ‘Wito Situisha’-- Wito kwa hali halisi kipindi hichi cha mwaka 2025-2050 ambavyo Hesabu fulani’ ya wanajamii Duniani inatosha na kukidhi ‘kinga’ dhidi ya mbinu za kudhibiti akili na kuchezewa akili – kuchezewa akili kwa ajili ya uhandisi wa matukio hasi duniani.


Hili ni lile lile litokanalo na ukweli wa kwamba ‘Vita ya Kiroho’ huyakinisha hatma ya vita ya kwenye ulimwengu fizikia/wa maumbile. Magonjwa ya kutengeneza, Migogoro ya Kiuchumi, na Vita ni michezo ya kuratibu hofu na kuivunja mioyo ya wanajamii Duniani ili kuwafanya wajisalimishe kwa ‘Nia Ovu’ zinazoweza kufichwa kwenye mashauri ya ‘Usalama wa Jamii na Amani’ kama ambavyo hapo nyuma kuna moja la mfano huo – bado linakusudiwa siku za mbele kidogo…


HUKUMU ni jambo la kukadirisha muafaka baina ya ELIMU na ILIMU ambavyo ‘Ujinga, Umaskini na Maradhi’ ni athari za Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu; Ujinga-Umaskini-Maradhi SI MAPENZI YA MUNGU bali muktadha hafifu wa kujichagulia Kimaisha kutegeana na Mazingira ama/na Mazingira ya Kiutamaduni.


Kinachoweza kuondoa adha za Ujinga, Umaskini na Maradhi ni ‘Mwangaza wa Kweli wa Nuru ya Ufahamu’ kupitia ‘Shughuli’ ya kugusa vyote viwili ‘Mioyo na Akili’ ya wanajamii—Asili khasa ya kile Kilichofunulika kwa Mtakatifu Augustini; na kuleta Ontolojia ya Taasisi ilivyo ni ‘Shughuli ya Jumuiya ya Mtakatifu Augustini.


Moyo Imani na Usimba ni kitovu cha Ujasiri uliojaa Dhamiri na Nia kwa ELIMU na ILIMU ni ufunguo wa ‘NGUVU YA MAGEUZI’ kwa ‘kanisa’ na vivyo hivyo katika Mapana yote ya jamii Duniani—hata na kupita, kwenye Sayari zingine zinazosota kwenye ‘Uchanga ama Uduni’ wa Mashauri ya Kiroho.


HUKUMU ni Shughuli ya kuibadili ‘Statusi Kwou’ katika mapana ya Utamaduni Globali hapa Duniani kusudi ‘UFALME-NGUVU-UTUKUFU’ vidhihiri kwa kadiri ya IBADA YA SUBIRA kwa mageuzi kamili ya UTU na UADILIFU kwa mifumo yenye kheri ambavyo ‘Ujinga-Umaskini-Maradhi’ wapinduka kuja kuwa ‘Uakilifu-wenye-mwangaza-Bora -|- UJAZI -|- Afya-Njema-Kimwili na Kiroho. Hili ndilo lenye Kutimilisha shauri katika ‘UFAHAMU KRISTU’ katika ‘Dhamiri Pitilizi/Ufunuo’:


Kiufundi, Statusi Kwou ndiyo namna ya kukadirisha shauri kana kusema:


Kiufundi, katika ‘Wito Situisha’ 2025-2050, Kujichagulia ni UTASHI kwa ajili ya ‘MAGEUZI KAMILI ya UTU na UADILIFU’ kwa ajili ya UFALME-NGUVU-UTUKUFU ambavyo muktadha akilifu wa Maisha na Kujichagulia katika Utamaduni Globali wawa ni ‘Agano la Mwisho’ kwa ‘Adamu wa Zamani’ na tena ‘Kufanyika Adamu Mpya’ – Mwanzo wa ‘Kulijenga Jiji la Mungu’ ilivyo ni ngome ya ‘Upyaishaji wa Jamii’ kwa ajili ya ‘Zama Mpya ya Nuru katika Mtu/UTU’.


Kiufundi, kuitika ‘Wito Situisha 2025-2050’ ni Dhamiri na Nia ya ‘Kuenda Duniani Kote kutangaza ‘Shauri Jema’ kwa ajili ya ‘Ufufuko na Uzima’ , kilatini kufanania kabisa na kauli mbiu : EUNTES IN MUNDUM UNIVERSUM : “kutangaza kote Utukufu wa ‘Roho ya Uzima Wote’ kwa Uwepo wa Kiutumishi”.


Uwepo wa Kiutumishi wa mwanajamii yeyote mwenye Mwangaza wa Kweli wa UTU na SHAURI JEMA ni ‘Nguvu na Utukufu’ kukadirisha SUBIRA na IBADA; subira na ibada kwa kheri ya Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu ndani ya wanajamii wote wanaoweza kufikiwa ama kuwa karibu naye – wanajamii wenye kukidhi UWEZA-UTAYARI-UMAHIRI kwa ajili ya KUTOKA kwenye ‘Himaya iliyo ni Babiloni/Ubabiloni’ na ‘kurejea Ngamani’ kwa Kukwea TRENI KILIMANJARO : Mavuno kwa Walimwengu…


Kufuzu UFAHAMU KRISTU katika dhamiri na nia zetu, fanusi za kiutendaji wa Shauri Jema kwa ‘Wito Situisha’ 2025-2050 ni ‘kufanyika Malaika wa Mavuno’ na tena kule kuwa : ‘Katika MOJA/YUNIAAMU, tu WaU-umoja’ : kilatini kufanania kabisa na kauli mbiu: “IN ILLO UNO UNUM,” – Mambo ya ‘Uumoja katika Mwili wa Kristu : (1) Fadhili na Kufadhilika, na tena (2) Rehema na Kurehemeka, na tena (3) Neema na Kuneemeka.


Haya yafanya SHAURI KUU kwa mawili ya (1) ‘Njia ya Msalaba’, na (2) ‘Shika Neno, Tenda Neno’ : Soltaya ; katika (3) ‘Uzabibu 13’; ambavyo ‘Rizayati ya UTU Bora’ ni jambo lile lile la ‘Sala ya Bwana’ kwa ‘Vitovu Sahihi vya Uono Mifumo’ -- katika kusadifu muktadha akilifu kwa UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI’.

== Uimajinishi Na Njozi : Liberiti Afrika ==​



Afrika, ni nchi yenye jiografia ya kipekee katika Sayari yetu ya Dunia; jambo linaloweza kutumika kudhihiri kwa UTU na UTAMADUNI wa mfano kwa ujamii wote wa nchi, tawala na ustawi.


Ili kudhihiri UTU na UTAMADUNI wa mfano, Shauri Kuu kwa Ujamii wote wa nchi, tawala na ustawi haunabudi kuakisi fizikia na metafizikia ya UZIMA WA MAMBO; ambavyo ‘Maarifa na Maarifu’ katika Usentienti wa Kila mwanajamii vyafanya nasibu ya (1) Mazingira, na (2) Mazingira ya ‘Mti wa Uzima’.


Uimajinishi kwa mti wa Uzima ni ‘Tunda la Uzima’ kwa ‘Dhamiri na Nia’ ilivyo ni ‘Uhuru na Umoja’; kwa kuwa ‘Nia’ hutokana na ‘Dhamiri’ pale panapokuwepo ‘Ukataji wa Shauri’.


Liberiti Afrika ni ‘Shauri Kuu’ kwa ‘Ufufuko na Uzima’ wa wanajamii wa Afrika, waliopo ndani na hata nje ya Mipaka yake kama Kisiwa Kikubwa Kabisa cha Kujitegemea katika Sayari yetu ya Dunia.


Uhuru na Umoja ni mhimili wa Imani kwa ajili ya ‘Kujichagulia’ ambavyo ‘Nia’ hujenga tabia na mazoea kwa miundo ya kujipangilia kiutendaji na matendo ili kuakisi ‘Utukufu na Nguvu’ wa ‘Shauri Kuu’.


Konsayansi ndivyo basi ni akili na utambuzi wenye kuzingatia ujuzi wa mema ama mabaya ya kutenda ama kudhamiria; ambavyo ‘Kuifanya Afrika Mti wa Uzima’ ni udhamirifu wa Koherensia na Sinejia kwa Shauri Kuu la ‘Liberiti Afrika’.


Konsayansi ndivyo basi ‘Ufalme’ wa (1) Uimajinishi, na (2) Kuumba, huooana mazingira na mazingara kwa ajili ya (x) Uweza, (y) Utayari, na (3) Umahiri wa kudhahirisha na Kudhihirisha ‘Matendo Makuu’.


Konsayansi ndivyo basi ‘Matunda ya Uhuru’ hufanyika Sura na Utukufu ili kuzaa muktadha akili wa UJAZI katika ustawi wowote wa jamii – jamii yenye kushiriki ‘Shauri Kuu’ lililo ni moja.


Ni ‘Nuru ya Ufahamu’ inayomulikia Akili na Utambuzi ili kubayanisha uweza-utayari-umahiri dhidi ya ‘dhambi ya asili’ katika fanusi jamii : Ujinga-Maradhi-Umaskini… ‘Miiko’ ni zao la (1) Umahsusi wa Shauri, na (2) Muktadha akilifu kwa ‘Maarifa na Maarifu’ ya makusudi yaliyo mema kutenda na kuenenda kwa uadilifu wa kimawazo, matendo na kutimiza wajibu.


‘Nuru ya Ufahamu’ ni asili ya mwangaza wa kumulikia njia za wanajamii ili kuongoza mapito yao ya kijamii na Utamaduni; ambavyo ‘ELIMU’ yapaswa kuwa ni shauri linalopitiliza nasibu zote za ‘Maarifa na Maarifu’ yenye kudumisha ‘Utumwa wa Kiakili’.


Hili ndilo lafanya muktadha akilifu wa Shauri la Kiongozi wa Ethiopia, Haile Selassie I, katika karne ya 20 kupata kusema juu ya Afrika na Waafrika kwamba:
We must become something we have never been and for which our education and experience and environment have poorly prepared us. We must be bigger than we've ever been: bravest, bigger in spirit and clearer in perspective. We must be members of a new race."

"Yatupasa kuwa ni kile ambacho hatujapata kuwa na kwa ambacho elimu yetu na uzoefu na mazingira vimetuandaa kwa utendaji wa hali ya uduni. Inatupasa kuwa ni wa namna kubwa zaidi kuliko vile tumepata kuwa: Majasiri wa sifa ya juu kabisa, wakubwa zaidi katika roho na wenye jicho lenye uuono mweupe zaidi. Inatupasa kuwa wanajamii wenye kuifanya mbari mpya."


Katika wakati huu, 2025 na kusonga, Kuwa majasiri wa sifa ya juu kabisa ni ‘Ndoto’ kwa ajili ya ‘Jamii na Ustawi’ ambavyo mazingira na mazingara ya Afrika na Waafrika vyasimamia misingi ya imani kwa ajili ya ‘Liberiti Afrika’. Kuwa wakubwa zaidi katika roho ni ujumuishi wa uweza wa kutenda katika ‘Mazingira’ na pia ‘Mazingara’ kwa ajili ya ‘Mti wa Uzima’--Maarifa na Maarifu katika mwangaza wa Utu Bora katika muktadha akilifu wa ‘Utambuzi wenye kuzishinda Kasumba’.


YANTRA DHAMMA< na >TRIZANIAMU< ndiyo ufunguo kwa kusahihisha na kujisahihisha KIUTU na UTAMADUNI kwa yale ambayo elimu yetu na uzoefu na mazingira vimetuandaa kwa utendaji wa hali ya uduni. Kuifanya mbari mpya ni ‘Udhamirifu wa Sovereini Jumuifu’ katika karne hii ya 21 na kusonga…


== Simba wa Ukwanzania : Udugu na Haki ==​



Kuwa majasiri wa sifa ya juu kabisa ndicho kile kichajacho na lugha alama ya SIMBA mwenye kuweka moyoni /Kifuani uadilifu wa Sayari yetu ya Dunia kwa mbegu zote za nasibu ya ‘UFALME’ : Nasibu ya Usahihi wa Kimfumo ilivyo ni ‘UFAHAMU KRISTU’ : Uzabibu 13… Katika kipindi hichi cha ‘Mavuno’, Fahari ya Simba ni Roho ya Kulinda Mageuzi Makuu ya Kijamii Kiakili na Utambuzi – kwa Moyo wenye Kina kwa Mafikara yenye Nguvu.


Kwa fahari ya Simba, kode ya ufahamu Kristu inadhihiri kwa Mraba wa SHAURI-NGUVU-UZURI-UPENDO. Wanajamii wowote Duniani walio na UWEZA-UTAYARI-UMAHIRI kwa kufuzu moyoni na akilini mwao hili SHAURI LENYE UKUU ndiyo wanayoifanya ‘Mbari Mpya’…


UFALME-NGUVU-UTUKUFU ni kwa wale wanaofanyika ‘UTU MPYA’ katika udhamirifu wa makubwa zaidi katika Roho; ambavyo Maisha na Kujichagulia kunadhihiri ‘Utukufu na Nuvu’ wa Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu utokao na Uimajinishi na Njozi ya ‘Mti wa Uzima’.


Afrika Mpya ni Ufufuko wa Kiutu na Utamaduni, kupitia Elimu 2.0 na Elimu 3.0… Si jambo la ‘Watu weusi ama Weupe ama Wanjano’… Ni ‘Utaamuliko Jamii’ unaoangazia ‘Wanadamu’ na tena kwa namna zao zote/zozote za kufanyika kimwili, akili na Roho.


‘Udhamirifu wa Sovereini Jumuifu’ ndicho khasa hatma ya Jamii na Ustawi katika sifa na hadhi ya ‘UJAMAA NA KUJITEGEMEA’. Kiufundi, hili ndilo limekuwa ni ‘fumbo la imani’ kwa ‘Utaasisi Dola’ kwa kuwa hili liwe linajulikana wazi ama tofauti, Dola zote Duniani ni Taasisi za ‘Maandalizi ya Ujamii’ wenye ‘Nguvu’ na ‘Umoja’ katika yote ya Sayarini.


Dola, ilivyo ni Taasisi/Utaasisi, ni muktadha wa upatanisho wa 'Nia za Wanajamii' na 'Nia ya Kiumbe' cha 'kufikirika: 'Nchi-dola'; kwa namna hii Dola ni muktadha wa 'Nia' yenye kuratibu 'Ushawishi' wa Taifa kuwa kama kitu kimoja; miongoni mwa wanaojua ilivyobora na hata wale wasiojua ilivyobora. Na basi Dola, hufanyakazi kupitia watu wenyewe--wenye ushawishi/madaraka ya wazi wazi na hata wale wasio ushawishi ama madaraka ya wazi wazi.


Afrika Mpya ni nasibu ya ‘Ujamhuri Uliotaamulika’ na basi kujumuisha ‘Maarifa na Maarifu’ ya fizikia na metafizikia ya mambo kwa ‘Nguvu za Shauri/Mashauri’ na si ‘Sheria Tupu’ za kudhanifu ‘Adili Hili ama Lile’ juu ya Uzima, Liberiti na Udhamirifu wa Furaha kwa wanajamii—wanajaii wenye kujielewa/kuelewa Mambo, kujua ilivyobora na kujitambua/timamu.


Afrika Mpya ni udhamirifu wa Kujisahihisa na Masahihisho ya Kitaasisi ilivyo ni muktadha akilifu wa manane(8) ya msingi:-

(1/8) Visa na Mikasa ya Minyororo ya Kufikirika


- Vipofu kuongoza vipofu wenzao kuwa ndiyo nasibu ya ‘Ontolojia ya Taasisi’ yenye kukadirisha ‘historia yenye Kurudia’ katika mapana ya mazazi na ustawi wa jamii.

- Uono na Ufikirifu pofu wa Kimakundi kulingana na Ufundi na Utundu wa Kutengeneza ‘Ontolojia ya Taasisi’ itokanayo na Mashauri Mushkeli kwa ajili ujamii, Siasa, uchumi na mazingira ya Utu na Ustawi; ambavyo ‘Hofu’, ‘Wasiwasi’ na ‘Kupangwa Kiakili’ kunaweza kuwachota kiakili wote (1) Watu wa Visomo, na (2) Watu Wasio na Visomo.

- Hatma ya ‘Maisha na Kujichagulia’ kuwa mikononi mwa dhamira na nia ya Utu Bora, Akili na Utambuzi madhubuti na Chachu ya Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu.

(2/8) Mbawa zilizovunjika

- Mioyo iliyovunjika na kupondeka yenye kuponza Wanajamii na kule kuishi Kinyonge kutokana na mihangaiko na hadaa katika Ulimwengu wa Mashauri ya Uongo na Kweli juu ya ‘Maisha na Kujichagulia’.

- Kutowepo kwa uadilifu wa mashauri yenye kupendeza katika miundo na matendo ya wanajamii na taasisi/utaasisi wa miundo ya utendaji, tawala na ustawi—tuseme labda kwa mifano ya ‘Dola na Utaifa’ vivyo hivyo ‘Utaasisi wa Dini na Waumini’.

- Asili ya Uponyaji wa jamii na jumuiya yote ya kimataifa inayotegemea UWEZA-UTAYARI-UMAHIRI, katika ‘Subira ni Ibada’, mwelekeo wenye kuzingatia ‘Utaamuliko Jamii’; ambavyo mwangaza bora katika fahamu na mafahamu katika Akili na mioyo ya Wanajamii wenye Kheri huongozea kwenye ile ‘panga pangua’ ya miundo ya utendaji na matendo -- ilivyo ni uthabiti wa Misimamo imara ya Kiroho, Maadili na Miiko katika ‘Dhamiri na Nia’ za matendo na mahusiano ya jamii.


(3/8) Kuitambua Mbegu na Mizizi ya Fitina


- Mashauri yasiyo na ‘Mbegu ya U-JUA-ji’ kwa ajili ya ‘Hekima ya Uzima wa Milele’; ilivyo ni asili ya ‘Changa la Macho’ lenye kuwapofusha wanajamii wasishituke jinsi wanavyoicheza ngoma ya ‘Mashetani Wasiyoyajua’.

- UGUMU na ULAINI wa UPENDO; Ufagio kwa Yanayofaa na Yasiyofaa katika Mapana ya Mazazi na Mapenzi ya Maisha na Kujichagulia; ambavyo UPENDO MGUMU yawezakuwa ni ‘fagio la chuma’ kwa mabatili ya ‘Utu na Kujichagulia’. Katika njia ya mageuzi na mapinduzi UPENDO MGUMU ni lazima; na huu kudhihiri ‘si dhambi’ bali yaweza kuwa ni mkakati wa Maisha na Uisho kwa ajili ya ‘kuyanyoosha mapito’… ‘Upendo laini’ isiwe kichochoro cha kushawishika vibaya kiuadilifu, maadili na miiko ili kudumisha ‘Statusi Kwou’.

- Fremukazi ya Utendekavyo Maamuzi jamii (FAM); ufunguo wa kutenganisha Pumba na Uwele katika ‘Miundo ya Utendaji’ na ‘Maamuzi Jamii’ kwa ajili ya ‘Usovereini Jumuifu’.


(4/8) Yabanayo Hali na Uweza na Fursa katika Hayo


- Elimu na Mapambano; jamvi la ‘tega nikutege’ kwa ‘Statusi Kwou’ ilivyo ni ‘Mkosi kwa Jamii’. Mapinduzi ilivyo ni ‘sarakasi na mkate’ kwa sura, sifa na hadhi ya mageuzi jamii ikiwa wanajamii wenyewe hawajiongezi ili ‘Kujua ilivyobora’.


- Mashirika, Ushirika na Ulanguzi; mchezo na michezo ya wanajamii wenyewe ilivyo ni ‘Mauti yao ya Kiroho’. Dola na Mifumo katika Utamaduni Globali, muamuzi wa ‘Mchongo’ kwa hatma ya kweli ya Utu na Ustawi.


- Kujikwamua Kiakili na Kiroho; silaha ya mwisho dhidi ya mabatili na madhalimu ya mifumo ya maisha, kujichagulia na ustawi wa Kweli wa Jamii na UTU. Kujichagulia na Machaguo yanayoshirikisha Dhamira na Nia za wengi wenye Kujichagulia katika ‘Uzima na Ukweli wa Mambo’ ni ‘Mwamba wa Mageuzi’ na ‘Hukumu’ dhidi ya ‘Siasa za Uongo na Kweli za Uliberali wa kidemokrasia’ na ‘Sanaa za Tawala’.


(5/8) Duara, Pembetatu na Mraba ya Uzima wa Mambo


- Kila kitu katika maisha ilivyo ni (1) Pembetatu ya Utendaji, (20 Duara la Uzazi, na (3) ‘Mraba wa Msalaba’ wa Mazazi; ambavyo Uadilifu, Maadili na Miiko ni muktadha akilifu wa Maisha na kujichagulia kulingana na Ushiriki na tena Ushirika wa yale yenye Uthamani kwa Ujamii na Utamaduni, wakati mmoja hata mwingine.


- Maisha, Ushawishi, Majaribu na Mikingamo ya mapana ya ustawi ilivyo ni finomena ya ‘Riziki’, ‘Matamanio ya Kimwili/Kiroho’, na ‘Kutafuta Kujitambua’; kupitia (x) Mahusiano ya kijamii na (y) Mazuri/mabovu ya mapana ya Ustawi wa Jamii.


- Nasibu ya Mageuzi ya Kijamii kwa miundo ya utendaji kama Ndoa, Kaya, Jamii, Taifa n,k kufanania na maingiliano ya stawi na tamaduni kutoka nje ya Sayari ya Dunia. Hivi vyote vinakwenda kubadilika sana karne hii ya 21 na kusonga; ambavyo ‘Hekima kwa Maaarifa na Maarifu ya Uzima wa Milele’ yataongozea kule kuibuka kwa Ukaya, Ndoa, Jamii na Taifa wenye kufuatisha ‘Mitindo ya Maisha’ inayofananiana na watu wa sifa, uweza, utayari na umahiri tofauti tofauti katika mazingira ya nchi na utamaduni.

(6/8) Kuita Uwepo wa Jicho lenye Kuona Kote na Mote


- Intelijensia ilivyo ni kiini cha Ufahamu na Mafahamu katika Mtu/Mwanajamii ama hata pia Ujamii na Mazingira yake ya Ustawi. Intelijensia isipokuwa na mizizi ya ufahamu na mafahamu kwa yote yaliyo katika ‘Mazingira’ na ‘Mazingara’ ni mwanzo wa ubabaishaji wa ‘Kheri na Ukweli’ juu ya kudumu na kustawi kwa jamii yeyote; kwa kuwa ‘Mrejesho wa tafsiri ya Matendo/Kujichagulia’ katika Halmashauri ya Akili na Utambuzi. ‘Shauri Kuu’ la Ujumuishi wa Kheri ya Ujamii itakosa ‘vina sahihi vya tafsiri’ kwa udhibiti wa ‘Sura na Mwenendo wa Jamii’ katika muktadha akilifu wa Mazingira ya Ndani na pia Mazingira ya Nje ya Ustawi wake.

- Metafanusi na Utendaji wa Juu Kiroho ilivyo ni ufunguo wa ‘Intelijensia’ yenye mashiko zaidi na madhubuti kwa ukweli wa mambo na asili ya matendo ya Wanajamii; ambavyo ‘Utayari’ ni kutengeneza nafasi ya utendaji wenye kina na mizizi katika ‘Nuru ya Ufahamu’ kwa ajili ya kutafuta ‘USAHIHI wa KIMIFUMO’ ili kuandama kheri na Uzima wa Jamii—Jamii yenye kujitafuta katika Dhamira na nia ya Kushiriki ‘Mema ya Nchi’.


- Maarifa na Maarifu ilivyo ni tunda la fahamu na Ufahamu kwa ajili ya ‘kujichagulia’; kutokana na mwangaza ujao na ‘Nuru ya Ufahamu’ katika ‘Usahihi wa Kimifumo’ na tena kwa ajili ya mapito na kuongoza ule mwenendo katika mapito ya safari ya jamii – jamii na ujamii kwenye mapana ya nasibu ya ‘fahari ya Utu Bora’. ‘Nuru ya Ufahamu’ ni fanusi ya Jicho lenye Kuona Kote na Mote kwa yeyote yule mwenye ‘kuchagua fungu jema’ la UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI.


(7/8) Kushikiza Msumari wa katikati kwenye Msalaba wa Muundo wa Mazazi Bora


- Dhamira na Nia ilivyo ni Msalaba wa ‘Shika Neno, Tenda Neno’ -- ilivyo daima ni msalaba wenye kuhitaji Mraba kwa ‘Muundo wa Mazazi Bora’ : ‘Shauri Kuu’ kwa kule kudumisha ‘Uhuru na Umoja’ kwa ‘Wake na Waume’.


- Ukosefu wa Mraba wa ‘Muundo wa Mazazi Bora’ unavyoiponza Elimu na Visomo vyake isiwe ‘Ufunguo wa kweli wa Maisha’.


- Uono na Ufikirifu Mifumo ilivyo ni msumari wa kushikiza (1) Mraba wa Muundo wa Mazazi Bora na (2) Utendaji wote wa UTU/Ubinadamu; ubinadamu wenye Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu. Trizania ilivyo ni fremukazi, kwa ajili ya Uono na Ufikirifu Mifumo, yenye mwangaza zaidi kwa mahusiano ya dhana za maisha na kujichagulia; kuakisi mapana ya uhitaji wa utu/mwanajamii kimatiriali, kiroho na Kiuwepo. Kujamiana ilivyo ni sehemu ya ‘Utendaji wa Asili’ kwa yote yenye kuitika ‘Shauri Kuu’ la Uzima wa Mambo : “Zaeni Mkaongezeke...”


(8/8) Uchumi Mama kwa Neema na UJAZI


- Adha ya fedha kuwa mzizi mkuu wa fitina kwa (x) Riziki na (y) Uchumi Mbovu wa Dunia; ambavyo ‘Ulanguzi’ ni kiini cha Ubepari usiyotenganisha mipaka ya (1) Uhitaji wa kweli wa bidhaa na mali, na (2) Tamaa ya Mali na Mahodhi ya Njia Kuu za Uchumi kwa ajili ya ‘Utawala wa Uchumi na Fedha’. Ubeberu ni zao la harakati za ‘Utawala wa Uchumi na Fedha’; bidishi kwa hata ‘intelijensia ya mazingira’ ya kuongoza ama hata kuhadaa umma kwa ‘Elimu za Mchongo’ na ‘Taasisi za Mazabe ya Kiuchumi wa Fedha’--kudumisha Utamaduni wa ‘wenye macho kujua kula vizuri na vipofu’.

- Masahihisho ya Kiuchumi wa Fedha na Ulanguzi yanavyoweza kugeuzwa kwa ‘Usanisi wa Ujasiriamali wa Kijamii’; kwa kuzingatia ‘Maarifa na Maarifu’ yanayohusisha ulandanifu wa konstrakti za fahamu na mafahamu ya UTU na UZIMA – “Mti wa Uzima”.

- UJAZI, ilivyo ni dhana inatotangamanisha WAKATI na UHITAJI; huku ikiengua nasibu ya ‘Tamaa/Wivu’ ama/na ‘Disonia ya Maslahi Binafsi dhidi ya Maslahi ya Umma’. Utangamano wa maslahi ni ‘Sala na Kazi’ kwa ‘Mapenzi Mema’; ambavyo ‘fizikia na metafizikia’ ya Ustawi wa jamii ni ‘Dhahiri na Dhihiri’ ya Utendaji katika ‘Mazingira na Mazingira’ ya Usentienti-Konsayansi-Nuru ya Ufahamu. Tekinokrasia na Meritokrasia, katika USAHIHI WA KIMIFUMO, inaweza ‘kupanga na kupangua’ yote ya (1) ‘Siasa Chafu’ na (2) Mifumo Mibovu ya Miundo ya Tawala na Utendaji katika Jamii ili kukadirisha ‘UHAI MPYA’ wa Jamii, Ustawi na Maendeleo.


UHAI MPYA katika Mapana ya ustawi wa Jamii ni UFUFUKO wa MIILI YA UTENDAJI kwa Nuru ya Ufahamu yenye kujinasibu na ‘Maarifa na Maarifu’ yaliyobora na tena kuakisi kode za ‘SHAURI LILILO KUU’.
SHAURI-NGUVU-UZURI-UPENDO

Katika LIBERITI na HARAMBEE, AFRIKA : UTU NA KAZI !

“ TUUNGANE PAMOJA,

TUSHEHEREKEE PAMOJA,

USHINDI KWA UKOMBOZI WETU...”​
 

Attachments

  • Kujichagulia.png
    Kujichagulia.png
    132.4 KB · Views: 26
Back
Top Bottom