Mambo muhimu ya kujua Maishani

Mambo muhimu ya kujua Maishani

FAHAD KING

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2017
Posts
301
Reaction score
377
Vitu vya pekee ambavyo unatakiwa kujua mpaka sasa ni elimu unayoendelea kuipata, maisha halisi na muda wa masomo mpaka uhitimu. Nadhani wote tunafahamu kwamba mahitaji ya wafanyakazi kwenye mashirika mbalimbali ni chache kuliko wanaohitimu masomoni. Hali hii inaweza ikapelekea kuwepo kwa watu wengi mtaani pasipo kuajiriwa na ni burden kwa serikali na jamii kwa ujumla.

Tukianza na..
1:ELIMU UNAYOIPATA
Unapaswa kujua kwamba wakoloni waliharibu mfumo mzima wa elimu ya kujitegemea uliokuwepo Afrika na zaidi wamepandikiza elimu ya kutegemea 'white colar jobs'.Elimu tunayofundishwa mashuleni haina tija kwenye maisha halisi tuishio.Elimu hii lengo lake kubwa ni kumfundisha mwafrika awe mstaarabu,ajue kusoma na kuandika lakini si vinginevyo.Si ajabu sikuhizi kumuona mwenye phd,masters au degree yupo mtaani bila kazi hiyo ni kwasababu elimu aliyoipata si ya maisha halisi(elimu ya kiutafutaji)

WAZO...
Kila kijana ni lazima abadilishe mawazo akilini mwake.Ni lazima ajiwekee malengo yake kufika mbali pasipo kutegemea ajira.Anatakiwa achukue uamuzi mgumu wa kujimegua toka utegemezi kwenda kujitegea mwenyewe na kitu kizuri ni kwamba inawezekana japo ni kitu kigumu kidogo.

2:MAISHA HALISI
Maisha halisi ni kwamba hayahitaji uwe na vyeti ndo utusue maishani.Kitu kinachohitajika ni kwamba how are u going to face your problems with great determinations.Kinacho hitajika ni kivipi unaweza ukatatua changamoto ulizonazo?Elimu tunayotakiwa kuipata mashuleni ni ile ambayo huendana na mazingira halisi lakini jambo hili kwetu halipo ndo maana ukimuuliza mwanafunzi wa kidato cha nne a express kuhusu ohm's law kwenye physics hawezi.Kwahiyo wakati tunasoma tujaribu kuona maisha halisi

3:MUDA WA MASOMO
Assume mtoto ana miaka 7 ndo anaanza darasa la kwanza na miaka 7 baadae anahitimu akiwa na miaka 14.Sekondari anaingia akiwa ana miaka 15 na anafikisha miaka 18 ndo anamaliza.Advance anamaliza akiwa na miaka 21 na chuo inategemea na course yenyewe kwa maana wapo wanaosoma miaka 7 na si chini ya miaka 5.Ukiangalia vizuri utapata kugundua kwamba maisha yetu karibia yote tunayamaliza masomoni na ukilinganisha na life expectancy ya mtanzania ni miaka 54 sasa maisha utayafaudu lini?

Ni mawazo yangu nahitaji maoni yenu tafadhari Thinkertz

c9686035830cebc3954543b53299d544.jpg
 
Wao wanasisitiza tujiajiri, Wao na watoto Wao wanapiga madili kwenye ajira.
Mungu tu, ndiye mtenda haki.
 
Such a rare good points!

Nimekupata sana kiongozi hapo kwenye muda tunaotumia masomoni ni wa kubadilisha kwa kweli.

Ni Tanzania pekee ambapo mtu anatumia miaka 17+ shuleni hili kupata degree
 
Such a rare good points!

Nimekupata sana kiongozi hapo kwenye muda tunaotumia masomoni ni wa kubadilisha kwa kweli.

Ni Tanzania pekee ambapo mtu anatumia miaka 17+ shuleni hili kupata degree

Mie hayo mambo ya degree yalinishinda kitambo.
 
3:MUDA WA MASOMO
Assume mtoto ana miaka 7 ndo anaanza darasa la kwanza na miaka 7 baadae anahitimu akiwa na miaka 14.Sekondari anaingia akiwa ana miaka 15 na anafikisha miaka 18 ndo anamaliza.Advance anamaliza akiwa na miaka 21 na chuo inategemea na course yenyewe kwa maana wapo wanaosoma miaka 7 na si chini ya miaka 5.Ukiangalia vizuri utapata kugundua kwamba maisha yetu karibia yote tunayamaliza masomoni na ukilinganisha na life expectancy ya mtanzania ni miaka 54 sasa maisha utayafaudu lini?
Ni mawazo yangu nahitaji maoni yenu tafadhari Thinkertz

Wakati wao wazungu huanza shule na miaka mitano hadi sita primary school, wanasoma miaka 6, miaka 12 anaanza sec, miaka 18 anaanza chuo, miaka 21 au 22 anamaliza anaanza kazi. Na hata asipofanikiwa kufika high school bado wanafundishwa elim za ufundi, kilimo elim amabayo inakuwa practical kulinganisha na sisi na elim yetu ambayo haiko practical kabisa. nakuelewa sana mkuu, labda masomo ya sayansikim yafundishwe tena ki ufasaha, mashule ya ufundi kama Iyunga Tec, zipewe kipaumbele zaidi.

c9686035830cebc3954543b53299d544.jpg
[/QUOTE]
 
Back
Top Bottom