Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Kuna mwalimu mmoja hapa Tunduma-Mbeya alioa mke ambaye tayari alikwisha zaa watoto wawili na mwanaume mwingine.Asubuhi tulivu,wameamka salama,mke kapokea simu,mara ghafla akadondoka chini,akapoteza fahamu.Alipozinduka,aliangua bonge la kilio cha kinyakyusa.Alipoulizwa kunani,akajibu kuna ndugu wa karibu kafariki nyumbani kyela.Alipoulizwa ni nani kafariki,akajibu,'nitakwambia nikifika'.Kwa kuwe mume hali ya kifedha haikuwa nzuri,akaamua kuuza ng'ombe mmoja wa kisasa,akamkabidhi mkewe nauli na pesa ya matumizi.Baada ya kufika kule kyela,mke akapiga simu kumtaarifu mumewe kwamba mtu aliyefariki ni baba aliyezaa naye wale watoto wawili.Mume aka-panic vibaya na kumwambia aishie huko huko kyela na asirudi tena tunduma.Sijui wakuu mnalionaje hili.