Mambo matatu ya kurekebisha ndani ya CHADEMA

Mambo matatu ya kurekebisha ndani ya CHADEMA

Sikuwahi kufikiri mwanachadema anaweza kuathirika kwa propaganda zinazotengezwa mtaa wa Lumumba.

Mkuu Salary Slip hatuendi hivyo hata siku moja, Huwezi kucheza ngoma inayopigwa na mpizani. wako na kufuatisha midundo yake na mirindimo yake huku ukipiga mruzi na macho umeyafumba huku ukidhani eti unapambana naye... Hakika utatumbukia shimoni..!!! Hiyo unayodai tuifuate ni Demokrasia ya woga na ni ubaguzi wa waziwazi usio na kificho ambao katu sikudhani unaweza kukukumba mtu kama wewe.. Inashangaza kwa kweli..!!!!

Tambua mwisho wa Propaganda hii ndio mwanzo wa Propaganda nyingine.. Kamwe kwenye siasa propaganda si kitu cha kukikwepa kwa kufuata namna mpiga propaganda anavyoieneza (Umeamkia wapi leo mkuu?) Hapa ilipo. Chadema imepigwa propaganda kadha wa kadha na za hatari kuliko hizo unazodai eti tuzitende ili kuepukana nazo...!!! Mpaka wapiga propaganda wenyewe ilifikia kipindi wakajiaminisha sasa Chadema INAKUFA..!! Naam walijiaminisha kwamba itakufa kabla ya mwaka 2013 lakini je iko wapi??

Chadema ilidaiwa ni chama cha kikristo (Propaganda hii imewaathiri sana cuf mpka leo) IKAPITA SALAMA..
Chadema ilidaiwa ni chama cha Ukanda wa kaskazini... IKAPITA. SALAMA...
Kama vile haitoshi Chadema ilidaiwa ni chama cha Kigaidi...IKAPITA SALAMA.....!!!!!

Kumbuka propaganda zote hizo kila zinapoibuliwa na wapigaji zinakuwa na matukio kadha wa kadha ya kuisindikiza ili iweze kukubaliwa na wasikilizaji (wananchi) kamwe haivumishwi hivi hivi. Watakudanganyaje kwamba hiki ni chama cha Kigaidi?? Naam hapo watawakamata viongozi kadahaa wa chama na kuwahusisha na matukio hayo... Hapa wenye akili fupi watakubaliana na wapigaji..!!


Kuna watu huwa wanadai chama hiki ni Mpango wa Mungu..... Naam si bure ni kutokana na kuluka vihunzi,Mashimo,Makorongo na kila aina ya Mitego na mpaka tunavyoongea hapa mimi na wewe na wewe kuja na Mada yako hii ni kwamba Chadema ndicho chama kinachoshika nafasi ya pili kwa kuwa na wenyeviti wengi wa Mitaa kiliko chama chochote hapa Tanzina...!!! (Na hii ni baada ya kuungana na vyama vingine vinavyounda UKAWA pamoja na uchakachuaji mkubwa tuliouona ktk uchaguzi huo)

Kwa maoni yangu mimi ningesema.....

HAPO ILIPOSHIKA (CHADEMA) KATU ISIACHIE IENDELEE KUKAZA ZAIDI.

BACK TANGANYIKA
Kamanda Nakumbuka yale maneno ya Kamanda Chademakwanza watu walimshambulia huku ndani lakini nayaona yalikua na maana kubwa sana maana rangi za watu zinaanza kuonekana
 
Last edited by a moderator:
Sikuwahi kufikiri mwanachadema anaweza kuathirika kwa propaganda zinazotengezwa mtaa wa Lumumba.

Mkuu Salary Slip hatuendi hivyo hata siku moja, Huwezi kucheza ngoma inayopigwa na mpizani. wako na kufuatisha midundo yake na mirindimo yake huku ukipiga mruzi na macho umeyafumba huku ukidhani eti unapambana naye... Hakika utatumbukia shimoni..!!! Hiyo unayodai tuifuate ni Demokrasia ya woga na ni ubaguzi wa waziwazi usio na kificho ambao katu sikudhani unaweza kukukumba mtu kama wewe.. Inashangaza kwa kweli..!!!!

Tambua mwisho wa Propaganda hii ndio mwanzo wa Propaganda nyingine.. Kamwe kwenye siasa propaganda si kitu cha kukikwepa kwa kufuata namna mpiga propaganda anavyoieneza (Umeamkia wapi leo mkuu?) Hapa ilipo. Chadema imepigwa propaganda kadha wa kadha na za hatari kuliko hizo unazodai eti tuzitende ili kuepukana nazo...!!! Mpaka wapiga propaganda wenyewe ilifikia kipindi wakajiaminisha sasa Chadema INAKUFA..!! Naam walijiaminisha kwamba itakufa kabla ya mwaka 2013 lakini je iko wapi??

Chadema ilidaiwa ni chama cha kikristo (Propaganda hii imewaathiri sana cuf mpka leo) IKAPITA SALAMA..
Chadema ilidaiwa ni chama cha Ukanda wa kaskazini... IKAPITA. SALAMA...
Kama vile haitoshi Chadema ilidaiwa ni chama cha Kigaidi...IKAPITA SALAMA.....!!!!!

Kumbuka propaganda zote hizo kila zinapoibuliwa na wapigaji zinakuwa na matukio kadha wa kadha ya kuisindikiza ili iweze kukubaliwa na wasikilizaji (wananchi) kamwe haivumishwi hivi hivi. Watakudanganyaje kwamba hiki ni chama cha Kigaidi?? Naam hapo watawakamata viongozi kadahaa wa chama na kuwahusisha na matukio hayo... Hapa wenye akili fupi watakubaliana na wapigaji..!!


Kuna watu huwa wanadai chama hiki ni Mpango wa Mungu..... Naam si bure ni kutokana na kuluka vihunzi,Mashimo,Makorongo na kila aina ya Mitego na mpaka tunavyoongea hapa mimi na wewe na wewe kuja na Mada yako hii ni kwamba Chadema ndicho chama kinachoshika nafasi ya pili kwa kuwa na wenyeviti wengi wa Mitaa kiliko chama chochote hapa Tanzina...!!! (Na hii ni baada ya kuungana na vyama vingine vinavyounda UKAWA pamoja na uchakachuaji mkubwa tuliouona ktk uchaguzi huo)

Kwa maoni yangu mimi ningesema.....

HAPO ILIPOSHIKA (CHADEMA) KATU ISIACHIE IENDELEE KUKAZA ZAIDI.

BACK TANGANYIKA

Hivi wewe unafikiri watanzania wanaohongwa kanga na vitenge wana uelewa kama wako?

Kuna ugumu gani wa kufanya hayo mabadiliko?

Tusitoe mwanya wa propaganda kwa mambo ambayo si ya lazima na yanayoweza kuepukika.
 
Last edited by a moderator:
Hatutaki kuendeshwa na propaganda, Mhe Mbowe tawala milele Baba, ilimradi tu nchi yetu ipate ukombozi wa 2, demokrasia tuwaachie Democratic na republic huko America, hapa sisi tunataka ukombozi kwa kuiondoa CCM madarakani.


UKOMBOZI KWANZA DEMOKRASIA BADAE
 
Mkuu Sakary Slip heshima kwako!propagnda ni propaganda tu, wakimaliza wachaga watakuja wakurya, then wambulu, then wamasai... usichokijua wewe ni kwamba mbaguzi ni mbaguzi tu, Kwenye taifa changa lenye wajinga wengi kuwatawala kwa propaganda ni kazi rahisi sana..lakini tujiandae kwa maangamizi, kwa taarifa yako prpaganda pekee ya kuimaliza chadema ni udini... umebuma wanakuja na ukanda, uchaga( Bila kujua mchaga yupo kila mahali na karibu vyama vyote vyenye nguvu upinzani mchaga ni ama mwenyekiti au katibu mkuu? ) kwahiyo kuanza kuzungumzia uchaguzi wa chama kabla ya 2019 ni kutaka kuvuka daraja kabla ya kulifikia.
2. Hoja ya katiba ya chama ina msingi ukitegemea unaish katika nchi gani! Kwa Tanzania kulea chama cha siasa si kama kupka chapati kila mtu anaoana..hata marekani wenyewe kuna vitu kwao havijadiliki au vinajadiliwa na watu wachache saaana kwa manufaa ya nchi yao....wataongea mengi lakini marekani bado na itaendelea kuwa super power... n hao CCM umesikia lini wakipelekana mahakamani kama na wewe prop hazijakuingia kichwani...kama unabisha muulize EL,BM nk
3. Nikutakie maandalizi mema ya kuingoa CCM 2015
 
Chadema kijipange tu,kwasasa kuwa chama cha upinzani ndio jadi yake.Magogoni bado sana.
 
Japokua umejita wewe nimwanachadema na nilikua nakuona humu ndani ukipambania chama lakini nimeanza kukutazama kwa jicho la tato jitafakari kama hayo uliyoyandika yana Afya kwa chama?

Tukumbuke sisi tunafanikiwa kutokana na makosa ya CCM na tutambue kuwa hata wapinzani wetu watafanikiwa kutokana na makosa yote.

Siasa ni kama football,ukifanya kosa mwenzako anakupiga bao.

CCM leo hii inaangamia kwa kuwa viongozi wake ni watu "rigid" na kukataa kujirekebisha.

CHADEMA wamefika pazuri lanini safari bado haijafika mwisho.

Wana-CHADEMA sisi sio malaika.
 
Naona wana-CHADEMA taratibu mnaanza kufunguka macho japo wapo watakaoleta u-radical!! Hata hivyo, Salary Slip niseme wazi hizo sio propaganda bali ni ukweli uliotengenezwa na CHADEMA kama chama na kisha kushabikiwa na wana-CHADEMA wenyewe! Ukija kwenye suala la ukomo wa uongozi, kila mwenye akili yake anafahamu kwamba kipengele cha ukomo kiliondolewa, mbaya zaidi kiliondolewa kinyemela wakati walikuwa na uwezo wa kukiondoa kipengele husika kwa kufuata taratibu coz', kwa jinsi ambavyo Mbowe alikitengeneza chama, lazima angepata support hata kama wangeamua kubadilisha kwa kufuata taratibu! Leo hii ukisema CCM wanapenda kujilimbikizia madaraka kwa sababu Rais wa Nchi kupitia CCM lazima apewe Uenyekiti wa chama; hiyo haitakuwa propaganda kv ndivyo ilivyo!!! Leo hii ukisema CHADEMA kuna udikteta kwa sababu inazuia wanachama kwenda mahakamani, hiyo sio propaganda kwa sababu ndio ukweli wenyewe uliosimikwa na katiba lakini ukisema CCM nako ni madikteta kwa sababu katiba yao haioneshi kwamba mwanachama anaweza kuwa mahakamani, hiyo ni propaganda kwa sababu, ingawaje katika mlolongo wa mwanachama kutafuta hali yake hakuna inaposema anaweza kwenda mahakamani, lakini pia haijakataza kwenda mahakamani!!!

Miongoni mwa uliyosema, propaganda hapo ni moja tu... ya CHADEMA na Uchaga!! Hata hivyo, lakini pia ukweli unabaki pale pale kwamba, ingawaje CHADEMA kama CHADEMA hakijinasibishi na Uchaga lakini Wachaga wengi tu wanajinasibisha na CHADEMA... hawa ni wale ambao bila shaka waliingiwa na propaganda za CCM kwamba CHADEMA ni chama cha Wachaga, sawa na baadhi ya Waislamu walipoingiwa barabara na propaganda kama hizo na hatimae kujinasabisha na CUF! Ni mpuuzi tu anayeweza kukataa kwamba Waislamu hawajinasibishi na CUF!!!
 
Last edited by a moderator:
Hatutaki kuendeshwa na propaganda, Mhe Mbowe tawala milele Baba, ilimradi tu nchi yetu ipate ukombozi wa 2, demokrasia tuwaachie Democratic na republic huko America, hapa sisi tunataka ukombozi kwa kuiondoa CCM madarakani.


UKOMBOZI KWANZA DEMOKRASIA BADAE

Parties' Power.
 
Umejiuliza ni watanzania wangapi wenye uelewa kama wako?

Ni wangapi wenye uwezo wa kuchambua pumba na mchele?

Mtu asie na uwezo wa ku-reason akitajiwa alianza Mtei akafuaya Bob Makani na sasa Mbowe wote wakiwa ni wachaga ni rahisi sana kuamini hizo propaganda.

Tusiotoe mwanya wa watu kutengeneza propaganda.

Mh. sana Salary slip Bob Makani hakuwa mchaga wala hakutoka kaskazini, propaganda zingine muwe mnaulizana vizuri kabla hamjapost!!
 
Don't allow others to set the agenda for you. We must continue to put them on the defense. We must not take instructions from them. Yaani unashauri tumwachishe Mbowe kugombea tena uenyekiti kwa sababu tu za kikabila?

It is not possible to be a little bit pregnant. Aidha CDM ina principles always au haina at all.

Tushukuru UKAWA have stopped this political hemorrhage momentarily otherwise we would have been talking other things right now.Don't be too stubborn to admit it,don't give CCM something to talk about!
 
Hatutaki kuendeshwa na propaganda, Mhe Mbowe tawala milele Baba, ilimradi tu nchi yetu ipate ukombozi wa 2, demokrasia tuwaachie Democratic na republic huko America, hapa sisi tunataka ukombozi kwa kuiondoa CCM madarakani.


UKOMBOZI KWANZA DEMOKRASIA BADAE

Nitambua si kila propaganda ina nguvu lakini hizi ninazozisema zimetukali vibaya.

Hebu niambie propaganda ya ugaidi ina nguvu gani kwetu na imetuathiri nini.

Propanda ya ugaidi wengi wameipuuza na wala haina mashiko lakini sio hizo nilizozisema ambazo si za kupuuza hata kidogo.
 
Hatutaki kuendeshwa na propaganda, Mhe Mbowe tawala milele Baba, ilimradi tu nchi yetu ipate ukombozi wa 2, demokrasia tuwaachie Democratic na republic huko America, hapa sisi tunataka ukombozi kwa kuiondoa CCM madarakani.


UKOMBOZI KWANZA DEMOKRASIA BADAE
te teh teh ama kweli nimeamini misukule iko mingi
 
Alichozungumza Salary Slip sio propaganda ni ukweli mtupu kuna tatizo la muundo wa katiba na uongozi CDM
 
Last edited by a moderator:
Hoja zako ni za msingi sana ila imezitoa bila msingi.
Chama kinaweza kutekeleza hayo mambo kwa kuangalia haja na msingi wake na sio kwa ajili ya kujilinda na propaganda.
Halafu hoja yako ya nne ni dhaifu.Haikutakiwa kutolewa na mtu wa kaliba ya #SalarySlip .You are better by far than this.
Then hitimisho lako nalo ni la woga sana! Wewe ni kamanda,angalau tunakujua kidogo,hupaswi kujihami kwa kuegemea kwenye fallacy.
Nashauri chama kiangalie mantiki ya hoja bila kujali msingi wa mwasilishaji.
 
Napenda kuwashauri CHADEMA watekeleze mambo matatu yafuatayo ili kuondoa propaganda chafu zinazosambazwa na CCM na ambazo zinaweza kuwa na athari mbaya kwa chama chetu.

Wana-CHADEMA,tunapaswa kutambua kuwa watu tunatofautiana katika uelewa wa mambo na katika mapokeo ya taarifa tunazoletewa au kuzisoma.

Kwa maana hiyo basi,mambo haya nashauri yatazamwe upya.
1.Ukomo wa kugombe uongozi urudishwe katika katiba ya chama na ikiwezekano ukomo uwe ni vipindi vitatu vya miaka mitano mitano.

2.Wanachama waruhusiwe kwenda mahakamni na mtu akishindwa kesi aruhusiwe kuendelea na uanachama wake.

3.Mh.Mbowe,kipindi chako cha sasa kikiisha,nakushauri usigombee tena na utoe fursa kwa wengine kugombea na wewe kama kiongozi, ujikite katika kuhakikisha chama kinapata mrithi bora,wa kuamimika na mwenye viwango.

Mchango ndani wako ndani ya chama ni mkubwa na wa kuthaminiwa sana ila ni vizuri sasa ukatoa nafasi kwa wengine ili kukinusuru chama na propaganda hizi.

4.Japo hatuchagu kiongozi kwa kuangalia kabila lake, lakini ikiwezekana katika uchaguzi wa mwenyekiti ajae jambo hili likaangaliwa kwa mapana na marefu yake.

Wenye akili na upeo wa kuona mbali watanielewa, ila wenye kukariri kuwa chama hakihitaji ushauri wa aina hii, watakuja hapa na vijembe na kejeli.

Yangu ni hayo tu.
Mbowe hawezi kukubali kabisa wachezee chama chake.

Lakini jambo la kufurahisha pro-Chadema taratibu mnaanza kujitambua.

Chadema wapo kama FIFA ukipeleka kesi mahakamani ni kosa halafu wanajiita chama demokrasia.
 
Tukumbuke sisi tunafanikiwa kutokana na makosa ya CCM na tutambue kuwa hata wapinzani wetu watafanikiwa kutokana na makosa yote.

Siasa ni kama football,ukifanya kosa mwenzako anakupiga bao.

CCM leo hii inaangamia kwa kuwa viongozi wake ni watu "rigid" na kukataa kujirekebisha.

CHADEMA wamefika pazuri lanini safari bado haijafika mwisho.

Wana-CHADEMA sisi sio malaika.
Nafikiri ungetumia busara si mahali pake hapa kuyaleta hayo kuna vikao vya chama, katiba ya chama inasemaje? Tusitete yale yote yaliyokatazwa na katiba katiba ndio chombo cha mwisho kimamuzi ndani ya chama

Asante
 
Hoja zako ni za msingi sana ila imezitoa bila msingi.
Chama kinaweza kutekeleza hayo mambo kwa kuangalia haja na msingi wake na sio kwa ajili ya kujilinda na propaganda.
Halafu hoja yako ya nne ni dhaifu.Haikutakiwa kutolewa na mtu wa kaliba ya #SalarySlip .You are better by far than this.
Then hitimisho lako nalo ni la woga sana! Wewe ni kamanda,angalau tunakujua kidogo,hupaswi kujihami kwa kuegemea kwenye fallacy.
Nashauri chama kiangalie mantiki ya hoja bila kujali msingi wa mwasilishaji.
Hivi nikuuluze kwa mfano,watanzania walipokataa mfumo wa vyama vingi walikuwa na sababu gani za msingi zaidi ya propaganda za CCM?
 
Back
Top Bottom