Mambo bado si shwari ndani ya CCM

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Msekwa akosa uvumilivu kwa Warioba

2008-09-30 11:37:50
Na Simon Mhina

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Pius Msekwa, ameshangaa madai ya Jaji Joseph Warioba kwamba vikao vya chama hicho vimejaa visasi na kukomoana na kumtaka aache kile alichokiita `usongombwingo`.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu kutoka Tarime jana, Msekwa alihoji kwa kusema: ``Wewe Mwandishi unajua maana ya Usongombwingo? Usongombwingo ni umbea uliojaa uzushi na uongo.``

Akifafanua, Msekwa alisema kwa vile vikao anavyolalamikia Warioba vya Umoja wa Wanawake (UWT) vilikuwa vya siri, na wala yeye hakuwa mjumbe, kwa vyovyote alipelekewa taarifa za vikao hivyo na wambea na hivyo kujikuta anajiingiza kwenye usongombwingo bila kujijua.

Msekwa alisema ameshangazwa na kauli ya Warioba kwamba Baraza Kuu la UWT lilitumika kumkomoa mmoja wa wanachama wake aliyeomba kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa, Halima Mamuya na kumpa alama `E`.

Alisema ameshangaa kuwa Warioba amepata wapi habari za Mamuya kupata alama `E` wakati vikao vya UWT vinahudhuriwa na wanawake watupu.

``Mimi nimeshangaa kama kweli Warioba katoa shutuma hizo kapata wapi taarifa za vikao vya UWT?

Vikao vile ni vya wanawake watupu, yeye alikuwepo? Hata wewe wa Nipashe unaponiuliza pia nakushangaa, mimi ni mwanaume hivyo huko UWT sikuwepo, labda muulize huyo huyo aliyetoa shutuma, labda yeye alikuwepo siwezi kujua mimi niko Tarime,`` alisema Msekwa huku akiangua kicheko.

Kikao cha Baraza Kuu la UWT kilichopitisha majina hayo na kumpa Mamuya alama E kilikuwa chini ya Mwenyekiti wake, Anna Abdallah ambaye ni mke wa Msekwa.

Msekwa pia alisema kisheria mtu anayetoa tuhuma ndiye anayetakiwa athibitishe.

Alisema kwa vile yeye bado hajapata taarifa rasmi juu ya madai hayo, hawezi kuzungumzia `usongombwingo` kwa vile akifanya hivyo atakuwa anajiingiza katika mambo asiyoyajua.

Alisema kimsingi Chama hakiwezi kuingilia maamuzi ya vikao vya jumuiya zake, kabla ya kuletewa taarifa zilizorasmi.

``Tunaziamini jumuiya zetu na taratibu zao, hatuwezi kuwaingilia kwa kutoa maamuzi kabla hawajatuletea taarifa rasmi juu ya vikao vyao na yale waliyojadili na kuamua,`` alisema Msekwa.

Kuhusu Nape Nnauye ambaye naye amepewa alama `E` katika mchujo huo kwenye Jumuiya ya Vijana (UVCCM), Msekwa alisema hata kwenye jumuiya hiyo, taarifa za vikao vya mchujo hazikufika rasmi.

Havi karibuni Warioba alikaririwa na gazeti hili akishutumu tabia iliyoibuka hivi karibuni ya wajumbe wa vikao mbalimbali vya CCM kuvitumia kulipa kisasi na kuwakomoa wanachama wanaoomba kuwania nafasi mbalimbali na kuwapa alama wasizostahili.

Warioba alisema Mamuya na Nape hawakustahili kupata alama `E` inayomaanisha muombaji hajui hata itikadi ya CCM.

SOURCE: Nipashe
 
Ambaye anadhani CCM mambo ni shwari lazima anajidanganya. Huko kuna tatizo ambalo limeanzia kwenye jumuia za chama kama UVCCM, WAZAZI na UWT- hii inalazimishwa kuwa ya Taifa.

Tumeona jinsi gani makundi (waliyodai kuyazikabaada ya 2005) yanavyochipua na kuongezeka hata kama ni kwa siri kubwa. Hivi unadhani kina Warioba na wenzake wanaweza kukaa kimya kuona chama kikubwa kama hiki kinaendekeza majungu na kukumbatia na kuwapa vyeo viongozi ambao kwao uongozi si kitu bali sehemu ya kukamilisha matakwa yao binafsi.

Tutayaona mengi, acha haya ya Mamuya na Nape, subiri Mangula akiamka na kusema(baada ya kuvuna mazo yake huko Iringa)


YAMKINI HALI SI SHWARI TENA- ACHEBE
 
Mpasuko mkali sana unawanyemelea CCM, waangalie kwa sababu wakianguka watasababisha madhara makubwa sana nchini
 
Yote hayo ni matatizo ya uongozi juu kabisa kwenye chama. JK na Makamba wameshindwa kukiongoza chama. Inatakiwa nidhamu pale juu na kwasasa inakosekana kabisa.
 
Mpasuko mkali sana unawanyemelea CCM, waangalie kwa sababu wakianguka watasababisha madhara makubwa sana nchini

Mimi naombea huo mpasuko utokee tu. Hata kama tutayumba kwa mwaka lakini huenda kwa nchi ikawa nafuu CCM wakigawanyika na kutokea makundi mawili. Inatakiwa itokee CCM ya mwalimu na CCM ya mafisadi.
 
Yote hayo ni matatizo ya uongozi juu kabisa kwenye chama. JK na Makamba wameshindwa kukiongoza chama. Inatakiwa nidhamu pale juu na kwasasa inakosekana kabisa.

Mkuu Mtanzania unaweza kufafanua kauli yako hapo juu ? Nidhamu ikisha wekwa ina maana wazibwe mdomo waache kusema mawazo yao au una maanaisha nini mkuu ?
 
Mimi naombea huo mpasuko utokee tu. Hata kama tutayumba kwa mwaka lakini huenda kwa nchi ikawa nafuu CCM wakigawanyika na kutokea makundi mawili. Inatakiwa itokee CCM ya mwalimu na CCM ya mafisadi.

Ni kweli, inabidi wawepo watu wenye courage kama ya kina Bingu wa Mutharika wa Malawi ili CCM ipasuke pasuke. Ikitokea hivyo nadhani tunaweza kuwa na balance of political power kwenye nchi hii ...sasa hivi li-CCM inakuwa ndio kila kitu lenyewe.
 
Mkuu Mtanzania unaweza kufafanua kauli yako hapo juu ? Nidhamu ikisha wekwa ina maana wazibwe mdomo waache kusema mawazo yao au una maanaisha nini mkuu ?

Kuna mtu alisema nidhamu bila uhuru ni utumwa na uhuru bila nidhamu ni fujo. Kinachotakiwa ni balance ya hapo katikati. Kwani ili kutoa hoja lazime utukane/upige watu wengine makofi? Sasa kama wale wanawake mpaka wanashikana mashati hadharani na bado wanaendelea kuwa viongozi, wewe unategemea nini?

Kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake lakini huna haki ya kupiga mtu mwingine au kutukana mtu mwingine. Lakini sasa siasa za TZ zimeanza kujaa ujinga tu.
 
Msekwa pia alisema kisheria mtu anayetoa tuhuma ndiye anayetakiwa athibitishe.


Du naona Msekwa kageuka mwanasheria, sasa kati ya Msekwa na Warioba nani anaweza mfunza mwingine sheria?
 
Du naona Msekwa kageuka mwanasheria, sasa kati ya Msekwa na Warioba nani anaweza mfunza mwingine sheria?


This is a big legal debate. Innocent until proven guilty or vice versa. Naona Msekwa yeye ameamua kuwa burden of proof ni kwa mtoa tuhuma kumbe kwa sheria nyingine mzigo unamwelemea mpewa tuhuma. Sasa Msekwa na Warioba, nani zaidi?

Asha
 
Back
Top Bottom