Mambo 10 ya kustaajabisha kwenye uchaguzi huu

Mambo 10 ya kustaajabisha kwenye uchaguzi huu

screpa

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2015
Posts
10,916
Reaction score
15,974
Uchaguzi huu umekumbwa na matukio mengi ya kustaajabisha kiasi kwamba yanaweza kukuacha mdomo wazi, haya ni baadhi ya mambo ambayo binafsi yamenishangaza sana;

1. Mama Anna Tibaijuka kuchaguliwa tena ubunge na wana Muleba

2. Wenje na Kafulila kukosa ubunge

3. Tume ya Zanzibar kulalamika uchaguzi haukua huru na wa haki (badala ya wagombea)

4. January Makamba kushangazwa na kinachoendelea Zanzibar

5. 'MAKAMANDA' wa CHADEMA kumkaribisha Lowasa kwenye chama chao na kumnadi kama mgombea wao wa urais (mtu waliyetuaminisha kwamba ni Fisadi Kwa miaka 8)

6. Wakazi wa Mwanza kudeki lami ili Lowassa apite ila cha ajabu kwenye sanduku la kura wamemuangusha na kumpa kura nyingi Magufuli

7. CHADEMA kumuona Lowasa kama mkombozi wao na Dr. Slaa kuitwa msaliti

8. Mgombea Maalim Seif kujitangazia matokeo kana kwamba yeye ni tume

9. Mbatia kutumia mda mwingi kuisemea UKAWA na CHADEMA kuliko chama chake

10. CCM 'chama dola' kulalamika kwamba kuna majimbo manne wameonewa
 
kweli ni screpa; maana ya screpa na kazi ya screpa si unaijuaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!
 
Other names and nick names they are equivalent to who u are,totally direct proportional to ur thinking capacity,,,,
 
kweli ni screpa; maana ya screpa na kazi ya screpa si unaijuaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!
Kazi yake ni kuuzwa kama chuma chakavu. Lakini hii screpa mbona imesema ukweli mtupu !! Hebu fikria Tume inalalamika kuwa uchaguzi haukuwa huru na kaki ilhali ishatangaza matokeo karibia yote; CDM kumsafisha na kumtangaza EL kama mgombea wao ilhali walisha sema kuwa ni mchafu Na. 8; CCM kulalamika kuwa wamibiwa kura katika majimbo manne, nani mwenye uwezo wa kuafanya hilo kwa chama tawala !!! Unatakiwa kuchambua mambo Critically nje ya box kama Great Thinker ukiwa mtu huru kama alivyofanya screpa bila kufungwa na mahaba ya upande fulani .
 
Duuuuh sasa kumbe umezunguka kooote ila point yako ni 5,6 na 7 yani kumshambulia lowasa
 
Ahsante sana csrepa umesema ukweli mtupu tatizo jamaa zetu wale wanaopenda kusifiwa tuu hata walipoteleza
 
ngoja nisikilize matokeo nikanywe biere
 
Uchaguzi huu umenikumbusha enzi tunacheza mpira, timu ya mwenye mpira ikifungwa anachukua mpira na kuweka kwenye kwapa na kuondoka...zenj!
 
Asante sawabho tatizo kuna upande Fulani humu JF hawapendi kuambiwa ukweli
 
Last edited by a moderator:
Other names and nick names they are equivalent to who u are,totally direct proportional to ur thinking capacity,,,,

Inawezekana ni kweli, but kipi nilichokisema cha uongo hapo?
 
11. Mawakala wa vyama vya siasa kama wawakilishi kuchelewa kufika na kwenda lunch na usiku kuondoka kwenda kulala na kuacha shughuli yao kwa wasimamizi wa tume

12. Majimbo ya mjini kwenye miundombinu yote kuchukua mpaka siku 3 kutangaza washindi na figisufigisu za kutaka kurudia kuhesabu ilhali usalama wa maboksi ya kura unatia shaka

13. Watangazaji matokeo kuchukua muda mrefu kutangaza wakijiua hiyo inazua sintofahamu kwa wapiga kura wanazi
 
Uchaguzi huu umenikumbusha enzi tunacheza mpira, timu ya mwenye mpira ikifungwa anachukua mpira na kuweka kwenye kwapa na kuondoka...zenj!

Hatari sana, pole kwake Maalim
 
Duuuuh sasa kumbe umezunguka kooote ila point yako ni 5,6 na 7 yani kumshambulia lowasa

what if point yangu ilikuwa 1,4 na 10 (kuishambulia ccm )?
 
Back
Top Bottom