Mama yangu ana matatizo sana, anavuruga familia yetu

Mkuu Mungu atusaidie Sana. Ni hatari Sana. Ni changamoto. Inafika point unachukua Likizo unatamani uende home ukutane na washkaji, marafiki wa utotoni na ufurahie zile flashback za street na Wana. Lakini ukiwaza unaona unaenda kutafuta maumivu unaamua kutafuta machimbo mengine!
Ndugu @ummtama mula, kwanza nikupe POLE kaka, kwa haya mazito uliyoyabeba moyoni kwa kipindi chote hiko.

Na la pili, NIKUPONGEZE kwa ujasiri huu uliokuwa nao, uliokupelekea wewe kufika hatua ya kuja hapa jukwaani na kufunguka hayo mazito uliyoyabeba moyoni kwa muda mrefu. Kwanini nasema huo ni "ujasiri", kwasababu UKWELI ni kwamba aina hiyo ya changamoto ya mzazi tena wa kike, imekumba vijana wengi sana katika jamii zetu hizi za kiafrika. Lakini 85% ya vijana hao wamebaki wakilia na kusononeka kwa uchungu vyumbani kwao, huku wakishindwa hata kutoka nje na kuongea kwa uwazi yanayowasibu, ili waweze kusaidiwa. Na hii yote imetokana na kasumba iliyopo kwenye jamii zetu, kuona wazazi hasa wa kike ni WATAKATIFU SANA, hivyo kijana chochote atakachokieleza juu ya *****, ataishia kuenekana yeye ndio mpumbavu na wengine watafika mbali zaidi na kumuona kama kalaanika! Wahanga wa hii psychological torture ni wengi sana.

Ila la tatu, naomba nikupe ASANTE kubwa kama ilivyo hapo, maana umenigusa au kunisemea moja kwa moja, ingawa tunatofautiana kwa kiasi fulani.

Kiukweli nami pia nina changamoto kama yako ya mzazi, tena afadhali wewe unaye baba, dada na bibi wa kukufariji.
Mwenzio hapa nilipo faraja yangu ni mke wangu tu. Maana baba, bibi na babu walishatanguliaga mbele za haki over ten years ago, wadogo zangu nao ndio tumesha sambaratishwa kila mmoja kona yake (hakuna maelewano) na ndugu nao ndio hawashikiki. Yaani taflani tupu....

Ila yote na yote, maisha lazima yaendelee kaka. Kikubwa ni kumuomba Mungu atufanyie wepesi, huku tukizidi kupambana na harakati zetu za kimaisha, ingawa mioyo inavuja damu. Kama kuna siku kutatokea mabadiliko, basi tutashukuru kwa hilo.

Ila kwa upande wako, kama asilimia kubwa ya wadau walivyokushauri humu, kwamba wewe jitoe kwa anayehitaji mkono wako. Nami nakazia hapo hapo, haya masuala mengine..... jitaidi kuyaweka kando, kumbuka TUNAISHI MARA MOJA TU.

Tchao
 
Duh,pole sana mkuu...viatu vyako vizito sana,siwezi kuvivaaa.


ILA KWA MLOLONGO HUO,AMUA CHAKUFANYA AMBACHO UNADHANIA SAHIHI ILA USIMDHARAU MAMA YAKO NA USIMSAHAU BIBI YAKO(MAANA BIBI AKO NDIO MWENYE KUSHIKA BARAKA ZAKO,ILA SIO MAMA AKO )


NB: HAPO NMEJIFUNZA KUWA BABA AKO HAJAKOSEA KUONDOKA,ALIJIONEA MAAJABU MENGI.


TUNAKUOMBEA NDUGU YETU
Shukrani mkuu
 
Pole sana aiseee naelewa maumivu unayopitia, nimeishi kwenye familia yenye tatizo Kama lako hakika ni changamoto sana. Mama kila kijana ake aioa mama hawakubali wakwe zake atafanya kila mbinu waachane. Watoto wake wamekuwa kila siku ni kuzaa na kila mwanamke na kuwa na idadi kubwa ya watoto wasio na matunzo kabisa lakin chanzo ni mama.
Ndugu yangu ni hatari Sana. Yaani mpaka naamua kuja mbele yenu wadau ni kama nilikuwa naelekea kupasuka. Atleast busara zenu na experiences zenu zinanipa relief wazee. Shukrani Sana.
 
Mkuu Mungu atusaidie Sana. Ni hatari Sana. Ni changamoto. Inafika point unachukua Likizo unatamani uende home ukutane na washkaji, marafiki wa utotoni na ufurahie zile flashback za street na Wana. Lakini ukiwaza unaona unaenda kutafuta maumivu unaamua kutafuta machimbo mengine!
Acha tu kaka, hii scenario inaumiza sana...!
 
Bibi ana maeneo makubwa Sana hadi leo almost hata 40 acres hivi. So nilichofanya Mimi ilikuwa ni kuhakikisa kila mwezi namtumia fedha kwa ajiri ya matumizi ya kawaida, na hiyo hela namtumia kupitia majirani.na kwenye hili namshukuru Mungu. Kwani wakati nagangaika mtaani nilikuwa nawaza itakuwaje Bibi akifariki bila kula hata senti yangu. Ila Mungu ni mkubwa Hilo nililitimiza mkuu!
Mungu ampe maisha marefu sana Bibi yako. Yan nimempenda kwa kweli
 
aisee. Mkuu.. mimi kama mimi huyo mtoto wa dada ningekata huduma. Mama ningekata mawasiliano nae kwanza. Ningedeal na bibi tu na ndugu zangu wanaonioenda. Kuhusu ada angekuja hapo ofisini afurahie show maana tabia zingine zinaonyesha no uchawi kabisa. Huyo mama yako si mzima. Ana elemebts za uchawi. Wachawi wanapenda umasikini. No wonder babako aliondoka aisee. Kama mumewe alimshindwa usijishangae. Fungamana na wanaokupa amani. Siku akajisikia kujirudi hewala
Unaongea tuu kwa sababu ayajakukuta mama ni kitu kingine wewe...
 
Mkuu tunatamani Sana. Kukaa na kuzungumza lakini tatizo tunakosa mtu anayeweza kusimama katikati. Mama amegombana na kila mtu mtaani, tangu arudi happy nyumbani hata majirani hawakanyagi tena wakati zamani palikuwa hapaukaukiwi watu, kwakuwa Bibi ni mtu alikuwa anapenda Sana watu.
Kanisani haendi kwakuwa aligombana na Mkurugenzi wa Kanisa. Mama na Bibi wanakaa wawili tu lakini huwezi amini kila mtu ana chungu chake.
Shida kubwa ni huyo mtoto wa nje yeye hataki ni mhudumie Kama mwanangu, na Mimi siwezi,ukizingatia historia ya maisha yangu. Lakini pia hamtaki mke niliyeamua kumuoa japo hajawahi kumuona na Wala hamjui. Ugomvi upo apo. Japo kuanzia zamani sikuwahi kuwa a favauritw kid kwake, lakini pia huwa anasema Bibi ametulea vibaya. Badala ya kumshukuru yeye anamnanga. Kwa ufupi na umri huu, kunifokea na kuniita mjinga kwake ni jambo la kawaida Sana!
Mimi naisi umemuendekeza wewe kuna vitu unavifanya ndyo maana anazidi kuwa mwiba kwako vp ukimchukua mwanao vp ukiwa unamtumia Bibi pesa kama kumpa mama awe anampa yeye Bibi vp ukijiweka mbali naye kama kumjulia Hali mtumie SMS au usimpigie kabisa muulizie kupitia dada yako mkubwa usingoje Mambo yaaribike maana mwanao ataona humjali na pale alipo labda mama yako atakuwa anamnyanyasa Hali itakayomplelekea ashindwe kusoma au kuishi Kwa furaha Kwa umri ulionawo ni wakati wa kuamua mlee Bibi yako Acha kujipa mawazo yatakayokuumiza nafsii utajiuwa mapemma kijana wazazi wetu wanakosea Ila Kwa busara jiweka mbali naye wala usimjibu Una dada anayeelewana naye basi Mpe pesa Ampe na muulize kupitia yeye ukienda home wala usijiweka karibu naye sana
 
Mwanaume mwenzio..baba yako alimkimbia mama yako unadhani ni mjinga! Mwanaume alikimbia tena unavyosema alikuwa mjeshi aliyeenda kumtwanga Nduli Amini, lakini kwa mama yako mjeshi kakimbia. Unaonekana kama ni mwenyeji wa Kigoma uenda mama yako ni Mhutu. Hawa wadada wa Kihutu hawana utu kabisa. Kaa mbali na huyo mama mtunze kwa kadri ya uwezo wako. Mtafute mjeshi mwanaume mwenzio ongea nae na mshirikishe tabia za mama yako atakachokujibu uje utupe mrejesho.
 
Dah pole sana mkuu.
Huyo ni mama yako na atabaki kuwa mama yako.
Kuna mdau ameshauri hapo jumbe brown una umuhimu sana.
 
Pole sana
Issue kama hizi ndio unaona watu hawaendi kwao kusalimia sababu wazazi wanawaongelea baya tu
Muhimu jiweke mbali naye tu hiyo ndio solution
 
Ni sahihi mkuu nami nilikuwa najitahidi kufanya hivo. Lakini shida ni kwamba anaanza na kumshawishi Bibi kidogo kidogo, ukizingatia Sasa Bibi ni Mzee Sana. Kinachoniumiza ni hicho. Asije aka mu induce na Bibi maana ndoo faraja yetu pekee ilikuwa imebaki.
I feel you
 
Nimesoma testimony yako na kugundua kwamba shule haijakukomboa. Kimsingi ulienda kusomea ajira.

Tueleze ni wapi ktk sheria ya ndoa unalazimishwa kumsomesha mtoto wa nduguyo?

Je ukiwasiliana na bibi na ukawa unamtumia matumizi utakufa?

Hii ishu ukimueleza baba yako anakushaurije?

Mkeo anakushaurije?

Kiongozi wako kiimani amekushaurije?

Kwa nini ukimbilie mitandaoni kabla ya watu wako wa karibu?

Uache ujinga dogo
Mmmh
 
Mungu kwanza. Mama anafata mpende muombee hata akiwa chizi ni mama yako. Mapungufu yake ni stress mpekeke kwa Yesu kwa Maombi. Tubu kwa kuzaa nje ya ndoa la na mwanao ataendelea hivo
 
Pole sana ndugu yangu, ipo siku yataisha.

Msamehe mama, usimuwazie sana, ila hakikisha bibi hapungukiwi na kitu.
 
Back
Top Bottom