utaifakwanza
JF-Expert Member
- Feb 1, 2013
- 14,193
- 2,815
Mama mzazi wa Naibu katibu mkuu wa CHADEMA Zitto Kabwe, amenusurika kutekwa. Waliomvamia wamemtishia kumuua huku wakimtaka awape laptop,simu na mawasiliano yake mengine...
Habari zaidi magazeti ya leo.
=========
*Anusurika kuuawa kwa bastola nyumbani kwake
*Wauaji wamdai laptop, flash na simu yake ya kiganjani
*Amtambua mmoja, adai ni kada wa Chadema
SHIDA Salum, mama mzazi wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, amenusurika kuuawa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake na watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, wakiwa na silaha za moto.
Habari zilizolifikia MTANZANIA Jumatano kutoka kwa watu walio karibu na mama huyo zilieleza kuwa, vijana hao walifanikiwa kumfikia akiwa katika sebule ya nyumbani kwake na kumuelekezea bastola kichwani, huku wakimlazimisha awakabidhi baadhi ya vifaa vyake vya kufanyia kazi na simu yake ya kiganjani.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, tukio hilo lilitokea Ijumaa ya Aprili 19, majira ya saa moja na nusu asubuhi.
Akizungumza na MTANZANIA Jumatano kupitia simu yake ya kiganjani kuhusu tukio hilo, mama yake Zitto alisema ni kweli lilitokea na amekwisharipoti katika kituo cha Polisi cha Buguruni.
Mama Zitto alisema siku kadhaa kabla ya tukio hilo alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa mwanachama wa Chadema wa Tawi la Tabata Relini na kumuomba msaada wa mifuko miwili ya saruji kwa ajili ya kukarabati jengo la ofisi yao.
Alisema alikubali kuwasaidia vijana hao kwa kuwataka wafike nyumbani kwake mapema siku ya Ijumaa ya wiki iliyopita, kwa sababu alikuwa na ratiba ngumu na ndefu siku hiyo.
"Nilikubaliana nao hivyo, bila kuwa na fikra kwamba wanaweza kuwa watu wabaya, hivyo walipokuja nyumbani kwangu baada ya kuruhusiwa na mlinzi niliwakaribisha ndani na kuwaeleza kuwa nitawapatia Sh 20,000 na Sh10,000 waongeze wenyewe.
"Lakini niliposimama kuelekea chumbani kuwachukulia kiasi hicho cha fedha, mmoja wao alitoa bastola na kunielekezea kichwani huku akieleza kuwa hawana shida na pesa, bali wanataka laptop yangu, flash na simu yangu ya mkononi kwa sababu zina mambo muhimu," alisema mama Zitto.
Alieleza zaidi kuwa alipowauliza ni kwa nini wanataka vitu vyake hivyo, walieleza kuwa anajua sababu na hata siri yake ya kutumia nafasi yake ya uongozi wa chama cha walemavu kuzunguka nchi nzima akimnadi mwanaye Zitto kwa wana Chadema kuwa anafaa kuwa mwenyekiti wa chama hicho na rais wa Tanzania inafahamika.
"Nilijua kuwa ninakufa, sikuona haja ya kubishana nao sana, nikamwita dereva wangu, Mtana, alete simu yangu niliyokuwa nikiichaji chumbani na flash ili niwapatie, wakati akielekea kuvichukua aliwaona walivyokuwa wameniwekea bastola, akakimbia moja kwa moja chumbani akajifungia na kuanza kupiga kelele, wakatoka haraka wakakimbia," alisema.
Alipoulizwa iwapo hawakupata upinzani wowote kutoka kwa mlinzi aliyekuwa getini au majirani walishtushwa na kelele za dereva wake, alisema wakati wanatoka geti lilikuwa wazi na mlinzi alikuwa akiosha gari nje, hivyo ilikuwa rahisi kutoka na gari lao na kutokomea.
Alisema anaweza kuwatambua watu hao akiwaona na kwamba mmoja wao si mgeni machoni mwake, kwa sababu aliwahi kumuona mkoani Tanga katika moja shughuli za chama hicho.
Mama Zitto alieleza zaidi kuwa kabla ya tukio hilo, amekuwa akiulizwa na baadhi ya wafuasi wa chama na hata watu wengine mahali anakopata fedha za kuzunguka mikoani kumnadi mwanaye, Zitto kwa ajili ya kugombea urais na uenyekiti wa chama.
Alisema kwa sababu ya kuhofia maswali ambayo amekuwa akiulizwa mara kwa mara, alimfikishia taarifa Kaimu Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Ahmed Sagula, lakini katika hatua ambayo hakuitegemea, naye alimhoji mahali anakopata fedha za kuzunguka mikoani kumnadi Zitto, kabla ya kumuahidi kushughulikia malalamiko yake.
Sagula mwenyewe hakuweza kupatikana jana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake kutopatikana kila ilipopigwa.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, naye hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo na hata Mkuu wa Kituo cha Polisi Buguruni, mahali ambako Mama Zitto ameripoti tukio hilo naye hakuweza kupatikana.
Chanzo: Mtanzania
Habari zaidi magazeti ya leo.
=========
*Anusurika kuuawa kwa bastola nyumbani kwake
*Wauaji wamdai laptop, flash na simu yake ya kiganjani
*Amtambua mmoja, adai ni kada wa Chadema
SHIDA Salum, mama mzazi wa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, amenusurika kuuawa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake na watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, wakiwa na silaha za moto.
Habari zilizolifikia MTANZANIA Jumatano kutoka kwa watu walio karibu na mama huyo zilieleza kuwa, vijana hao walifanikiwa kumfikia akiwa katika sebule ya nyumbani kwake na kumuelekezea bastola kichwani, huku wakimlazimisha awakabidhi baadhi ya vifaa vyake vya kufanyia kazi na simu yake ya kiganjani.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, tukio hilo lilitokea Ijumaa ya Aprili 19, majira ya saa moja na nusu asubuhi.
Akizungumza na MTANZANIA Jumatano kupitia simu yake ya kiganjani kuhusu tukio hilo, mama yake Zitto alisema ni kweli lilitokea na amekwisharipoti katika kituo cha Polisi cha Buguruni.
Mama Zitto alisema siku kadhaa kabla ya tukio hilo alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa mwanachama wa Chadema wa Tawi la Tabata Relini na kumuomba msaada wa mifuko miwili ya saruji kwa ajili ya kukarabati jengo la ofisi yao.
Alisema alikubali kuwasaidia vijana hao kwa kuwataka wafike nyumbani kwake mapema siku ya Ijumaa ya wiki iliyopita, kwa sababu alikuwa na ratiba ngumu na ndefu siku hiyo.
"Nilikubaliana nao hivyo, bila kuwa na fikra kwamba wanaweza kuwa watu wabaya, hivyo walipokuja nyumbani kwangu baada ya kuruhusiwa na mlinzi niliwakaribisha ndani na kuwaeleza kuwa nitawapatia Sh 20,000 na Sh10,000 waongeze wenyewe.
"Lakini niliposimama kuelekea chumbani kuwachukulia kiasi hicho cha fedha, mmoja wao alitoa bastola na kunielekezea kichwani huku akieleza kuwa hawana shida na pesa, bali wanataka laptop yangu, flash na simu yangu ya mkononi kwa sababu zina mambo muhimu," alisema mama Zitto.
Alieleza zaidi kuwa alipowauliza ni kwa nini wanataka vitu vyake hivyo, walieleza kuwa anajua sababu na hata siri yake ya kutumia nafasi yake ya uongozi wa chama cha walemavu kuzunguka nchi nzima akimnadi mwanaye Zitto kwa wana Chadema kuwa anafaa kuwa mwenyekiti wa chama hicho na rais wa Tanzania inafahamika.
"Nilijua kuwa ninakufa, sikuona haja ya kubishana nao sana, nikamwita dereva wangu, Mtana, alete simu yangu niliyokuwa nikiichaji chumbani na flash ili niwapatie, wakati akielekea kuvichukua aliwaona walivyokuwa wameniwekea bastola, akakimbia moja kwa moja chumbani akajifungia na kuanza kupiga kelele, wakatoka haraka wakakimbia," alisema.
Alipoulizwa iwapo hawakupata upinzani wowote kutoka kwa mlinzi aliyekuwa getini au majirani walishtushwa na kelele za dereva wake, alisema wakati wanatoka geti lilikuwa wazi na mlinzi alikuwa akiosha gari nje, hivyo ilikuwa rahisi kutoka na gari lao na kutokomea.
Alisema anaweza kuwatambua watu hao akiwaona na kwamba mmoja wao si mgeni machoni mwake, kwa sababu aliwahi kumuona mkoani Tanga katika moja shughuli za chama hicho.
Mama Zitto alieleza zaidi kuwa kabla ya tukio hilo, amekuwa akiulizwa na baadhi ya wafuasi wa chama na hata watu wengine mahali anakopata fedha za kuzunguka mikoani kumnadi mwanaye, Zitto kwa ajili ya kugombea urais na uenyekiti wa chama.
Alisema kwa sababu ya kuhofia maswali ambayo amekuwa akiulizwa mara kwa mara, alimfikishia taarifa Kaimu Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Ahmed Sagula, lakini katika hatua ambayo hakuitegemea, naye alimhoji mahali anakopata fedha za kuzunguka mikoani kumnadi Zitto, kabla ya kumuahidi kushughulikia malalamiko yake.
Sagula mwenyewe hakuweza kupatikana jana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake kutopatikana kila ilipopigwa.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, naye hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo na hata Mkuu wa Kituo cha Polisi Buguruni, mahali ambako Mama Zitto ameripoti tukio hilo naye hakuweza kupatikana.
Chanzo: Mtanzania
Zitto said:Nimekuwa naulizwa kuhusu Habari za mama yangu Mzazi Bi. Shida kuvamiwa na kutishiwa bastola. Nawajibu watu Kwa ujumla kwamba
"Moja, mie sio msemaji wa familia. Ni basi tu katika watoto wa mama yetu mie najulikana zaidi na hivyo mama anaitwa Mama Zitto. Kwetu Kigoma haitwi hivyo, ama Ni mama Salum au mama Lulu.
Pili, hili Ni suala la polisi. Lipo polisi na linashughulikiwa na polisi. Nisingependa kulisemea wakati Ni suala linalochunguzwa na polisi. Mama yangu Ni mama wa kawaida wa kitanzania kama mama mwingine yeyote yule. Matukio ya namna hii yamezagaa nchi nzima. Hivyo suala lake litashughulikiwa kama yanavyoshughulikiwa masuala mengine yote ya Watanzania. Polisi wakimaliza uchunguzi wao naamini hatua mwafaka zitachukuliwa.
Ushauri- tuwe makini na "Agente provocatuers" au in English "provocation agents" nyakati kama hizi. Calmness is the best protection against provocations. Nadhani mmenipata"
Nawatakia Kila la kheri katika kazi za ujenzi wa Taifa letu na kuimarisha Umoja na mshikamano wa Watanzania dhidi ya ufisadi, umasikini na ugandamizaji.
Chamviga,
Tangu nimekuwa mwanachama wa JF au mtandao mwingine wowote daima nimeingia kwa jina langu kamili Dr.W.Slaa. Ni kwa kuwa naamini kutumia jina bandia ni dalili ya uwoga. Yeyote mwenye anaweza kupima ninachoamini kwa kuonyesha identity yangu halisi. Hata hivyo, si vema kuvumilia upotoshwaji na udanganyifu wenye hila mbaya.
1) Leo niliposoma Gazeti la Mtanzania kwa nafasi yangu ya Katibu Mkuu nilimpigia simu Mama Zitto, kwanza kumpa pole na pili kujua hasa yaliyomsibu. Aliyoniambia mama Zitto yanapingana na yote yaliyoandikwa humo, mengine yakidhaniwa yamesemwa na mama Zitto, na mengine yakiandikwa na wachangiaji kwa hisia kali. Ni hatari sana taifa kuachia watu wakifanya utani na mambo yanayohusu maisha ya binadamu. Tutakuwa sio Taifa serious, linalogeuza kila kitu kuwa utani au ushabiki tu! Labda Mama Zitto akiniambia kuwa alinidanganya, na sioni ni kwanini anidanganye!
2) Nataka niweke wazi, mama Zitto hakuzungungumza nami, na wala kwa wakati wowote, sikumwambia amwone Hemedi Sabula. Yeye aliniambia amenitafuta, akanikosa, akamtafuta Sabula akamkosa. Hatimaye alimpata kwa simu ya Tendwa, afisa Ugavi, Makao Makuu. Pili, nimeongea na Mwenyekiti Mbowe, naye amenithibitishia hakuongea na Mama Zitto. Kauli hiyo inalingana na aliyoniambia Mama Zitto kuwa hakuwa amemjulisha Mwenyekiti Taifa. Ni dhahiri kauli zilizoandikwa kwenye mtandao huu zina malengo ambayo ni ya makusudi, na muda si mrefu tutayajua yote, lakini kwa vyovyote, dalili za awali zinaonyesha hazina nia njema na Chadema na viongozi wake.
3) Nimeongea na Afisa wangu Sabula kinachozungumzwa hapa ni kinyume kabisa na alichozungumza na Mama Zitto, na nimethibitisha hayo kwa Mama Zitto Mwenyewe.
4) Nimewasiliana na viongozi wangu wa Jimbo na Kata, kuhusiana na kijiwe chochote kinachojengwa. Taarifa sahihi ni kuwa hakuna kijiwe chochote kinachojengwa na kilichoombewa fedha kwa Mama Zitto. Ila kuna Ofisi ya Kata inakarabatiwa ndiyo iliyoombewa fedha, na wahusika walifika kwa mama Zitto na wakapewa fedha 30,000. Sitaki kuingilia uchunguzi wa Polisi, ninataka tu kuwasaidia walioingia kwenye Mtandao wengi wao kwa ID bandia na kutoa kauli nzito juu ya mambo wasioyoyafahamu na kutoa uhukumu.
Nimetoa taarifa hii kwa wote wanaotaka kujadili kwa nia njema, na sijatoa taarifa kwa mujibu wa majukumu na nafasi yangu kwa kuwa wanaozungumzwa wote ni viongozi ninaowahudumia kwa mujibu wa Katiba ya Chadema. Aidha, ni jukumu langu kulinda jina la Chadema pale ninapoona inataka kuchafuliwa bila msingi, wala utafiti wowote. Mengine nitaendelea kuwajulisha au kuyaweka hadharani kwa kaduri yatakavyokuwa lazima. Naamini kwa wale wenye nia njema haya yatawasaidia kujadili kwa Tija thread hii.