Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Rafiki yangu ni mtoto wa pekee kwa mama yake. Mama yake ni mwenyeji wa Mtwara. Alikua mfanyabiashara na mzigo aliufuata Kariakoo. Katika mahangaiko ya kukusanya mzigo alikutana na mfanyabiashara kutoka Kaskazini. Walianza mahusiano kwakua mama alikua single.
Mzee alikua na familia yake na mama alishagonga 50. Baada ya muda mama akawa anasumbuliwa na afya, ndipo alipogundulika na uja uzito. Alimshukuru Mungu alilea mimba na kujifungua mtoto wa kiume huko kwao Mtwara.
Yule mzee kutoka Kaskazini alipofahamishwa ujauzito alisubiri mpaka mtoto anazaliwa. Kufika Mtwara alijiridhisha kuwa mtoto ni wa kwake. Alituma pesa kila mwezi na mara moja kwa mwaka alikwenda kuwajulia hali.
Mtoto alipofika umri wa miaka nane alimpeleka Nairobi kusoma shule ya boda. Mtoto aliendelea vizuri na masomo. Alifanikiwa kupata ajira. Aliweza kumjengea mama yake nyumba ya vyumba viwili vya kulala wana sebule kijijini bafu choo na jiko nje. Kwakua maji si ya uhakika. Kwa pale kijijini nyumba yao ilikua ni kivutio, iliitwa nyumba yenye chipping.
Mama alifariki ghafla kijana akiwa safari ya kikazi DRC Congo. Kutokana na imani ya dini, wajomba walimzika dada yao aliyeishi kufikia miaka 90+. Baada ya mazishi wajomba wamehamia kwenye nyumba ya dada yao.
Rafiki alifika kuona kaburi na kuwaonea wajomba. Sasa mti umeangukia choo, wajomba wanamtaka alete hela wakitengeneze. Sasa kijana anasema nyuma mnakaa nyinyi mimi ninahusikaje kutengeneza choo ilhali mama yangu ameshaaga dunia!
Mzee alikua na familia yake na mama alishagonga 50. Baada ya muda mama akawa anasumbuliwa na afya, ndipo alipogundulika na uja uzito. Alimshukuru Mungu alilea mimba na kujifungua mtoto wa kiume huko kwao Mtwara.
Yule mzee kutoka Kaskazini alipofahamishwa ujauzito alisubiri mpaka mtoto anazaliwa. Kufika Mtwara alijiridhisha kuwa mtoto ni wa kwake. Alituma pesa kila mwezi na mara moja kwa mwaka alikwenda kuwajulia hali.
Mtoto alipofika umri wa miaka nane alimpeleka Nairobi kusoma shule ya boda. Mtoto aliendelea vizuri na masomo. Alifanikiwa kupata ajira. Aliweza kumjengea mama yake nyumba ya vyumba viwili vya kulala wana sebule kijijini bafu choo na jiko nje. Kwakua maji si ya uhakika. Kwa pale kijijini nyumba yao ilikua ni kivutio, iliitwa nyumba yenye chipping.
Mama alifariki ghafla kijana akiwa safari ya kikazi DRC Congo. Kutokana na imani ya dini, wajomba walimzika dada yao aliyeishi kufikia miaka 90+. Baada ya mazishi wajomba wamehamia kwenye nyumba ya dada yao.
Rafiki alifika kuona kaburi na kuwaonea wajomba. Sasa mti umeangukia choo, wajomba wanamtaka alete hela wakitengeneze. Sasa kijana anasema nyuma mnakaa nyinyi mimi ninahusikaje kutengeneza choo ilhali mama yangu ameshaaga dunia!