Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Mama wa kijana aitwaye Taramaeli Emanuel, anayedaiwa kumuua mke wake Martha Pius mkoani Arusha, ameongea kwa huzuni kubwa akieleza mawasiliano yake ya mwisho na mwanae
Amesema mara ya mwisho walizungumza, mwanae alimwambia azidi kumuombea. Baada ya tukio la mauaji kutokea, mama huyo alipokea ujumbe mfupi wa maandishi kutoka kwa Taramaeli akimjulisha kuwa aje nyumbani kwani yeye na mkewe “tayari wameshatangulia kwa baba.”
Tukio hilo limezua simanzi kubwa miongoni mwa familia, ndugu, na majirani, huku uchunguzi wa polisi ukiendelea kubaini chanzo na mazingira ya mauaji hayo.
Amesema mara ya mwisho walizungumza, mwanae alimwambia azidi kumuombea. Baada ya tukio la mauaji kutokea, mama huyo alipokea ujumbe mfupi wa maandishi kutoka kwa Taramaeli akimjulisha kuwa aje nyumbani kwani yeye na mkewe “tayari wameshatangulia kwa baba.”
Tukio hilo limezua simanzi kubwa miongoni mwa familia, ndugu, na majirani, huku uchunguzi wa polisi ukiendelea kubaini chanzo na mazingira ya mauaji hayo.