Mama Polepole amefika mahakama kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Dar es Salaam

Mama Polepole amefika mahakama kuu ya Tanzania Masjala ndogo ya Dar es Salaam

Its Tesha

Senior Member
Joined
Oct 6, 2025
Posts
168
Reaction score
604
Kesi ya jinai iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Malawi na Cuba Humphrey Polepole kupitia Wakili wake Peter Kibatala, inaendelea leo, Jumatano Oktoba 15.2025, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam

Katika kesi hiyo ambayo inasikilizwa chini ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam Salma Maghimbi, ambayo washtakiwa wake ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) na wenzake imefunguliwa kufuatia kutoweka kwake mazingira tatanishi kwa Polepole

Kutoka Mahakamani hapo, tunakusogezea kuona namna Mama mzazi wa Humphrey Polepole alivyowasili leo kuja kufuatilia mwenendo wa kesi hiyo.
 
Kesi ya jinai iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Malawi na Cuba Humphrey Polepole kupitia Wakili wake Peter Kibatala, inaendelea leo, Jumatano Oktoba 15.2025, Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam

Katika kesi hiyo ambayo inasikilizwa chini ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam Salma Maghimbi, ambayo washtakiwa wake ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) na wenzake imefunguliwa kufuatia kutoweka kwake mazingira tatanishi kwa Polepole

Kutoka Mahakamani hapo, tunakusogezea kuona namna Mama mzazi wa Humphrey Polepole alivyowasili leo kuja kufuatilia mwenendo wa kesi hiyo.
Wampe tu mwili wa mwanae.
 
kupoteza muda tu. unaenda mahakamani kufanya nini,ndugu yako anatekwa then unaenda kuripoti police ili iweje? kuna mtu aliwai saidika na police?.police ndiyo watekaji na wauaji then unaenda kuwashitakia kwao!.
 
Asiwe na wasiwasi kuna siku tutalipiza watesaji wa ndugu yetu .... Mungu mtie nguvu mama yetu najua anapitia wakati mgumu sana km mama
 
Mama mzazi wa Humphrey Polepole, Anna Mary akiwasili Mahakama Kuu ya Tanzania, akiwa na ndugu wa familia hiyo kwa ajili ya kusikilizwa kwa maombi ya kesi ya kudaiwa kutekwa kwa Polepole.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Wakili Peter Kibatala.

Video: Global TV
 
Mungu atatulipia Watanzania kwa haya wanayofanya wahuni wa madarakani kwa sasa. Mateso anayopitia huyu mama, watayalipia wote waliohusika na uhuni waliomfanyia mwanae.
 
kupoteza muda tu. unaenda mahakamani kufanya nini,ndugu yako anatekwa then unaenda kuripoti police ili iweje? kuna mtu aliwai saidika na police?.police ndiyo watekaji na wauaji then unaenda kuwashitakia kwao!.
Hata mimi nisingeenda mahakamani.Sijui Kibatala anawafanyia bure au wanamlipa?Mimi ningedeal na kuongea kila siku na kurusha mitandaoni .Walau ingeleta tension. Yaani kila siku naenda pale nje ya central Polisi ninaongea huku narekodiwa .
 
Back
Top Bottom