Mama mkwe anahatarisha ndoa yangu

Mama mkwe anahatarisha ndoa yangu

Mullocoz

Member
Joined
Feb 10, 2014
Posts
23
Reaction score
2
Mama mkwe amemshawishi mtoto wake aachane na mm na kumuambia km ataendelea kuishi na mimi atamuachia radhi mtoto wake nilipompigia cm mama mkwe akasema ndio nimemwambia nikamuuliza sababu gan akasema sina sababu sitaki tu na mtoto wake kaondoka kweli hii wiki ya 2 sasa hataki kurudi kwa mume wake anasema anaogopa maneno ya mama yake.naomba nisaidieni nifanyaje jamani na bado nampenda mke wangu.?
 
^^
Waache na maisha yao! Hata wewe unaweza kuishi pasipo wao. Jishughulishe na uzalishaji ili baadae wajutie uamuzi wao
^^
 
Mama mkwe wengine nuksi sana

Inawezekana amemtafutia mtoto wake pedeshee, kama wewe ndio mwenzangu na mimi nakushauri

Bora lawama kuliko fedheha

Fumbua macho usilale, akufukuzae hakuambii toka
 
Kama ni ndoa ya haki mbele za Mungu, basi Jua Mungu yu mkubwa kuliko mama mkwe na wewe ndo unapimiwa imani hapo kama kweli mwanadamu anaweza kupiga mkwara na alichounganisha Mungu kikatenganika.

Kazi ya wazazi ni kuwaleta watoto duniani na kuwalea katika mazinigra bora na siyo kuwaharibu. Naamini laana inayokubalika iko automatic kwa matendo mabaya utakayofanya na si mtu kukurupuka kuitamka ilhali hakuna kosa lililofanyika
 
Mama mkwe amemshawishi mtoto wake aachane na mm na kumuambia km ataendelea kuishi na mimi atamuachia radhi mtoto wake nilipompigia cm mama mkwe akasema ndio nimemwambia nikamuuliza sababu gan akasema sina sababu sitaki tu na mtoto wake kaondoka kweli hii wiki ya 2 sasa hataki kurudi kwa mume wake anasema anaogopa maneno ya mama yake.naomba nisaidieni nifanyaje jamani na bado nampenda mke wangu.?

Achana nae ndugu yangu labda mama yake kaenda kumuoa, we endelea na maisha yako akiona umuhimu wako atarudi.

Kama unaweza move on.
 
Mama mkwe amemshawishi mtoto wake aachane na mm na kumuambia km ataendelea kuishi na mimi atamuachia radhi mtoto wake nilipompigia cm mama mkwe akasema ndio nimemwambia nikamuuliza sababu gan akasema sina sababu sitaki tu na mtoto wake kaondoka kweli hii wiki ya 2 sasa hataki kurudi kwa mume wake anasema anaogopa maneno ya mama yake.naomba nisaidieni nifanyaje jamani na bado nampenda mke wangu.?

Mkuu pole sana, wajulishe wazazi wako kuhusu haya mambo. kama mna watoto jitahidi ubaki nao ili wasiende kufundishwa kukuasi na kama mkeo amekubali ushawishi huo ni bora ukubali matokeo ili ujipange kwa maisha mapya.
 
Back
Top Bottom