Mama hamtaki mchumba wangu

Asante.. nashukuru brother kwa ushauri.
 
Mkuu unaweza kupiga makofi vizuri?
Mama anataka upate sweetmangi! Wachaga wengi hua wanapenda ivyoo... SIO WOTE LAKINI
 
Mkuu unaweza kupiga makofi vizuri?
Mama anataka upate sweetmangi! Wachaga wengi hua wanapenda ivyoo... SIO WOTE LAKINI
Kila mtu anachaguo lake la moyo.. lakini sasa kama ndio hivyo anataka mwanamke wa kichaga.. na mimi hao nafahamu tabia zao..
kama bi mkubwa ana interest zake why iwe ngumu kusema?
 
Huyo mama vipi, kwan anaoa yeye au wew? Her interest should not interfear your interest. Mwambie hauoi kwa ajir ya kumfurahisha yeye
 
Mkuu naomba kudeclare interest mama yupo right unacho ongea mm kilinitokea 2010 na mbaya zaidi mpenz alikuwa mjamzito wa miez 7 bi mkubwa alichoniambia its similar to urz but its 4years now naamin what she was saying ni true but life lipo na litaendelea mkuu
 
Mama yako anataka kitu kimoja anajua wewe ndio utakuwa nguzo ya familia baadae lazima uwe katika sehemu mzuri kiuchumi sasa akiangalia elimu ya msichana Na tabia za msimamo Wake anajua kabisa utkuwa Na uzaifu Fulani kwa mwanamke Na kushindwa kusimamia familia anajua wewe ndio utakuwa baba baadaye je utauweza kuongoza familia mama yako anakujua udhaifu wako ndio maana anataka upate mke unayemzidi msimamo ili usipotee baadaye ukashindwa kuwa baba Wa familia Bora
 
mkuu ni kawaida mama kuonyesha (chuki?) wasiwasi kwa mawanamke mwingine anayeingia kwenye teritory yake kwani naye hutaka undivided attention. Usihofu we jifanye kama haujali anza taratibu za ndoa kisha oa.Kisha mpe ujauzito haraka baada ya kujifungua utashangaa wanakuwa maswahiba wa kutosha.Cha kufanya kama unaishi kwa mama yako ondoka haraka katafute sehemu nyingine ya kuishi.Ni usijaribu kumuambaia mchumba wako kwamba mama yako anamchukia, nae ataanza jitihada za kupigania attention yako.
 
Mama hataki ubebe mzigo. Anajua familia yote itakuelemea wewe.
Refer uzi huu:- Ukioa mwanamke masikini, tambua kuwa umeoa familia nzima
 
Some times kuna kitu anaweza akawa ameona, muulize vizuri.
kuna wengine baadae mkiwa pamoja likatokea tatizo anakwambia mimi nilishaliona hili ndo maan nikasita. anaweza (anaweza) akawa sahihi. muulize vizuri.
 
Usijaribu, nasema usijaribu kabisa kwenda against mama ama mzazi wako. KUna hadithi nyingi tu za watu walioharibikiwa kwa kutokuwasikiliza wazazi wao, wazazi Mungu kawapa kipawa cha kuona mbali sana kuhusiana na watoto wao. wameshauri hapa wakina uso wa nyoka nadhani ni ushauri mzuri kidogo tafuta mashangazi wako ama mtu ambae mama yako anamuheshimu sana Muombe akaongee na mama kuhusu suala hilo, nenda taratibu kaka usichukulie pupa.
 
Kila mtu anachaguo lake la moyo.. lakini sasa kama ndio hivyo anataka mwanamke wa kichaga.. na mimi hao nafahamu tabia zao..
kama bi mkubwa ana interest zake why iwe ngumu kusema?
Shida ya wazazi wetu hawataki kwenda na mabadiliko ya utandawazi...
 
Kama una mapenzi ya dhati kwake, mtakua pamoja haijalishi nini
 
Siendi kwenda against her... thats why natafuta solution kwa nguvu zote. Because nina hope kuwa anakitu ila hakisemi.
Nitajarib hiyo njia ua kutafuta mtu wa kuongea nae...
 
Kwanza pole braza. Lakin ningependa kujua nini kilikutokea...? nataka nijifunze kutokana na story yako. Unaweza kunitumia inbox
 
Nitalifanyia kazi ... lakin braza.. kama anamchukia sasa hivi akiwa hana mimba...? Atamkubali akiwa anayo?
Na pia kama hamkubali... vikao vya ndoa vitafanyika kweli?
 
yesuuu na maria wachaga tunaogopeka aisee ....jaribu kumshirikisha baba au ndugu wengine pia jarbu kumwambia mama yako hayo ni mambo ya zamani siku hizi dunia imebadilika
 
Some times kuna kitu anaweza akawa ameona, muulize vizuri.
kuna wengine baadae mkiwa pamoja likatokea tatizo anakwambia mimi nilishaliona hili ndo maan nikasita. anaweza (anaweza) akawa sahihi. muulize vizuri.
Mr jose.. uko right. I need to dig more deep.. mpaka nipate jibu sahihi ..na niweze kufanya maamuzi sahihi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…