Mama hamtaki mchumba wangu

Mama hamtaki mchumba wangu

Jay_the_analyst

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
206
Reaction score
151
Habari za asubuhi ndugu zangu, natumai mmeamka salama.

Lengo la kuleta hii mada ni kuomba ushauri kwa ajili ya jambo linalo nisumbua kwa muda mrefu.

Mimi ni kijana mwenye miaka 25, nimemaliza chuo miaka miwili iliyopita na namshukuru Mungu maisha yanaenda vizuri. Ndugu zangu nimekuwa kwenye mahusiano kwa miaka miwili na mchumba wangu. Tumesaidiana mengi na ameonesha mapenzi ya kweli kwangu kwani amejitoa kwa mengi nami nampenda sana kutoka moyoni.

Tatizo ni kwamba toka nilipomtambulisha kwa mama, mama ameonesha chuki waziwazi kwake. Nilijaribu kukaa na mama na kuongea nae lakini sasa hana sababu maalumu ya kumkataa.

Niliwahi kumuuliza pole pole lakini akasema kuwa hajisikii amani moyoni mwake kuhusu mchumba wangu. Nikamuuliza kwanini hajisikii amani? Akakosa jibu akanipotezea.

Sasa mchumba wangu ameumia mno kiasi kwamba anataka tuvunje mahusiano baada ya kujua mama hampendi. Kwakweli nimejaribu kila njia katika kusuluhisha hili jambo lakini naona naelemewa.

Ndugu wa mwanamke wananielewa sana na imetokea kwao wamenikubali sana, haswa mama yake na baba yaani wakiniona wanafurahi. Lakini mama yangu mimi hamtaki na hana sababu maalumu ya kumkataa.

Nifanyaje wadau? Naombeni ushauri wenu.
 
Nafkiri unahitaj kuwa serious ktk hili kumuuliza mama vzr sababu za kutompenda mchumba wako.pia mueleze kinagaubaga namna uuhusiano wenu ulivyo mpk sasa,hivyo unahitaj kufanya uamuz sahih juu ya hilo cuz time inaenda na hakujawa na linaloeleweka especially upande wako.endelea kumpliz mchumba wako akuvumilie wkt unafatilia ilo swala..
 
Swali Chokozi"
Mama yako ana ushosht na mama diamond?

Inanibidi umuoneshe kama unamini kile kilichopo moyoni mwako.
Mama Mpe nafasi moyo wako upe nafasi kubwa zaidi ya ile uliyompa mama.
 
TULIA KWANZA!!Maana Umepanic..Kama Mama Kagoma Hamna Uhusiano Hapo Mkuu,Kunywa Maji anza Kusaka Upya Bottom Line!!!
 
wewe ndo mtoto pekee kwa mama yako?

Baba yako yuko wapi?
 
Habari za asubuhi ndugu zangu.. natumai mmeamka salama.
Lengo la kuleta hii mada.. ni kuomba ushauri kwa ajili ya jambo linalo nisumbua kwa muda mrefu.

Mimi nikijana mwenye miaka 25, nimemaliza chuo miaka miwili iliyopita na namshukuru Mungu maisha yanaenda vizur.
ndugu zangu nimekuwa kwenye mahusiano kwa miaka miwili na mchumba wangu .. tumesaidiana Mengi, na ameonyesha mapenz ya kweli kwangu.. kwani amejitoa kwa Mengi.. nami nampenda sana kutoka moyoni.
Tatizo ni kwamba toka nilipomtambulisha kwa mama, mama ameonyesha chuki wazi wazi kwake.. nilijaribu kukaa na mama na kuongea nae lakini sasa hana sababu maalumu ya kumkataa.
Niliwah kumuuliza pole pole ...lakin akasema kuwa hajisikii amani moyoni mwake kuhusu mchumba wangu.. nikamuuliza kwanini hajisikii amani , akakosa jibu.. akanipotezea...
Sasa mchumba wangu ... amaeumia mno kiasi kwamba anataka tuvunje mahusiano.. baada ya kujua mama hampendi. Kwa kweli nimejaribu kila njia katika kusuluisha hili jambo lakini naona naelemewa..
Ndugu wa mwanamke wananielewa sana.. na imetokea kwao wamenikubali sana , haswa mama yake, na baba.. yaani wakiniona wanafurahi.
Lakin mama yangu mimi hamtaki.. na hana sababu maalumu ya kumkataa.. nifanyaje wadau? Naombeni ushauri wenu.
Kabla sijakupa dozi sahihi toa maelezo yako kwa tabibu mimi kwa kunijibu maswali haya yafuatayo....

1÷wewe kwenu mumezaliwa wangapi

2÷wewe kwenu ni kijana wa kiume wa pekee

3÷mama yako amekulea katika malezi gani...single mom au kuna baba pia

4÷mpenzi wako ana umri gani je pia mpenzi wako ana mtoto kazaa na mwanaume mwingine

5÷imani ya mpenzi wako na wee iko sawa...yako ni siku moja au tofauti

6÷mpenzi wako elimu yake iko aje na ametoka katika familia ya kitajiri au kimaskini kuliko familia yako

7÷mpenzi wako ni kabila gani

8÷mpenzi wako anavaa au swag za aina gani

9÷mpenzi wako anaishi mtaa mmoja na wewe

10÷familia yako na ya mpenzi wako wameishawahi kuwa na tofauti au morogoro ya sina yoyote.

Jibu maswali yangu nikupe ushauri mujarabuu kabisa.
 
Tafuta mama zako wadogo au wakubwa au hata wajomba zako uwaombe wamuulize,akiendelea kujibaraguza na kushindwa kutoa jibu LA kueleweka, achana nae na uendelee na Mipango yenu. Kama ni ndoa,ni yako wewe na mchumba wako,mahaba ya mama Kwa mkwewe ni swala secondary na lisilo na uzito labda kama bado mama anakulisha. Hujamtaja baba yako,msimamo wake yeye ukoje?
 
Sasa ni wivu wa nn hasa hasa,kwa kua ke wa mtoto wake ni mzuri au
Anaona attention itahama kutoka kwake kwenda kwa mkamwana...anawaza mambo mengi,pengine hutamjali kama mwanzo..mapenzi yatapungua..atakuwa hakupati kwa muda nk.Most of them wanakuwa changamoto kwa wakwe zao wa kike.
 
Tafuta mama zako wadogo au wakubwa au hata wajomba zako uwaombe wamuulize,akiendelea kujibaraguza na kushindwa kutoa jibu LA kueleweka, achana nae na uendelee na Mipango yenu. Kama ni ndoa,ni yako wewe na mchumba wako,mahaba ya mama Kwa mkwewe ni swala secondary na lisilo na uzito labda kama bado mama anakulisha. Hujamtaja baba yako,msimamo wake yeye ukoje?
Nitafanya hivyo ndugu.
Msimamo wa baba hana noma kabisa. Nilishawahi kumwambia na akasema tu niwe makini. Lakini mama ndio amekuwa kikwazo?
 
Vp ushirikina upo kwenu au kwao binti?
Ushirikina hakuna kabisa upande wetu... wala hakuna matukio ya ushirikina katika ukoo. Vile vile pia kwa mwanamke ni watu waliookoka na wana msimamo katika wokovu na mama wa mwana mke ni mchungaji.. hata baba naenameokoka.
 
Kabla sijakupa dozi sahihi toa maelezo yako kwa tabibu mimi kwa kunijibu maswali haya yafuatayo....

1÷wewe kwenu mumezaliwa wangapi

2÷wewe kwenu ni kijana wa kiume wa pekee

3÷mama yako amekulea katika malezi gani...single mom au kuna baba pia

4÷mpenzi wako ana umri gani je pia mpenzi wako ana mtoto kazaa na mwanaume mwingine

5÷imani ya mpenzi wako na wee iko sawa...yako ni siku moja au tofauti

6÷mpenzi wako elimu yake iko aje na ametoka katika familia ya kitajiri au kimaskini kuliko familia yako

7÷mpenzi wako ni kabila gani

8÷mpenzi wako anavaa au swag za aina gani

9÷mpenzi wako anaishi mtaa mmoja na wewe

10÷familia yako na ya mpenzi wako wameishawahi kuwa na tofauti au morogoro ya sina yoyote.

Jibu maswali yangu nikupe ushauri mujarabuu kabisa.

Kujibu maswali yako.. nianze na hili.
- nyumbani mimi ndie wa kwanza
-nyumbani tumezaliwa watatu, wakiume wawili ,wakike mmoja
-nimelelewa katika malezi ya baba na mama.. na but mostly mama kwa sababu baba alikuwa hakai nyumban mara nyingi kutokana na kazi yake.
-imani ya mpenzi wangu na mimi viko sawa, kwani wote huwa tunaenda kanisani pamoja.
-mpenz wangu ana swag zankawaida tu.. ni mtu muelewa sana.. alaf mpole but ana msimamo sana.
-mpenz wangu hakai mtaa mmoja na mimi
-kabila lake ni mkuria... mimi mchaga
-familia yangu na ya mpenzi wangu hawajawahi kugombana kwa sababu hawafahamiani na wala hawaja wahi kuonana.
-umri wa mpenz wangu ni 22.
 
Kujibu maswali yako.. nianze na hili.
- nyumbani mimi ndie wa kwanza
-nyumbani tumezaliwa watatu, wakiume wawili ,wakike mmoja
-nimelelewa katika malezi ya baba na mama.. na but mostly mama kwa sababu baba alikuwa hakai nyumban mara nyingi kutokana na kazi yake.
-imani ya mpenzi wangu na mimi viko sawa, kwani wote huwa tunaenda kanisani pamoja.
-mpenz wangu ana swag zankawaida tu.. ni mtu muelewa sana.. alaf mpole but ana msimamo sana.
-mpenz wangu hakai mtaa mmoja na mimi
-kabila lake ni mkuria... mimi mchaga
-familia yangu na ya mpenzi wangu hawajawahi kugombana kwa sababu hawafahamiani na wala hawaja wahi kuonana.
-umri wa mpenz wangu ni 22.

bado hujajibu swali la elimu na uwezo wa familia zenu mbili kiuchumi....nisaidie jibu tafadhali.
 
Back
Top Bottom