Malipo ya pensheni mwezi August 2022 - PSSSF

Malipo ya pensheni mwezi August 2022 - PSSSF

Jaylee

Member
Joined
Apr 15, 2009
Posts
66
Reaction score
96
Imekuwa kama kawaida malipo ya pensheni ya kila mwezi kwa mfuko wa PSSSF yanakuwa tayari kila tarehe 24 ya mwezi. Mfuko pia unatuma ujumbe(sms) unaompa taarifa mstaafu kuwa malipo hayo yameshatumwa benki.

Hii ni tofauti na mwezi huu wa Agosti ambapo malipo hayafanyika na taarifa iliyozoeleka pia haijatumwa. Je, kuna tatizo au ndiyo fedha za wastaafu zilizopigwa kama ilivyoripotiwa kwenye vyombo vya habari hivi karibuni? Au je, kuna uhusiano na tozo mpya za mabenki?

Idadi kubwa ya wastaafu wana marejesho ya mikopo ya benki yanayokatwa moja kwa moja kupitia mafao yao ya kila mwezi. Kama ni kweli kuna tatizo je, mabenki yatalichukuliaje jambo hili ukizingatia kuwa tatizo halijasababishwa na wateja wao?
 
Pension imeshalipwa.

Hilo la makato ya mikopo naamini halina mabadiliko makubwa
 
Imekuwa kama kawaida malipo ya pensheni ya kila mwezi kwa mfuko wa PSSSF yanakuwa tayari kila tarehe 24 ya mwezi...
Nilisoma kichwa cha habari kwenye gazeti moja kwamba hela za wastaafu zimechotwa na Mwigulu kutoka hazina! Labda ni kweli?
 
Imekuwa kama kawaida malipo ya pensheni ya kila mwezi kwa mfuko wa PSSSF yanakuwa tayari kila tarehe 24 ya mwezi...
Hivi siku hizi kuna makato ya wastaafu kupitia pensheni? Wanakopesha mwisho muda gani? Na ni benki zipi?
 
Imekuwa kama kawaida malipo ya pensheni ya kila mwezi kwa mfuko wa PSSSF yanakuwa tayari kila tarehe 24 ya mwezi...
Inawezekana haukujihakiki, kama ni hivyo nenda kajihakiki na malipo mwisho wa mwezi wa tisa.
 
Imekuwa kama kawaida malipo ya pensheni ya kila mwezi kwa mfuko wa PSSSF yanakuwa tayari kila tarehe 24 ya mwezi...

Malipo gani hayo hayajalipwa? Malipo yalishalipwa kuanzia tarehe 22/08, sasa kama hujalipwa basi kuna tatizo kwenye akaunti yako. Nenda kawaone PSSSF.
 
Nilisoma kichwa cha habari kwenye gazeti moja kwamba hela za wastaafu zimechotwa na Mwigulu kutoka hazina! Labda ni kweli?

Hilo litakuwa moja ya yale magazeti ya kufungia maandazi!
 

Attachments

  • IMG-20220825-WA0044.jpg
    IMG-20220825-WA0044.jpg
    90.8 KB · Views: 37
Sasa kama pension imelipwa huyu mdau mbona analalamika? Watu wengine wakoje lakini?

Atakuwa anaishi porini huyo! Ameenda benki akakuta hela zake hazipo? Na kwa nini hela zake hazipo wakati wengine walishalipwa tangu 22/08?
 
Imekuwa kama kawaida malipo ya pensheni ya kila mwezi kwa mfuko wa PSSSF yanakuwa tayari kila tarehe 24 ya mwezi. Mfuko pia unatuma ujumbe(sms) unaompa taarifa mstaafu kuwa malipo hayo yameshatumwa benki.

Hii ni tofauti na mwezi huu wa Agosti ambapo malipo hayafanyika na taarifa iliyozoeleka pia haijatumwa. Je, kuna tatizo au ndiyo fedha za wastaafu zilizopigwa kama ilivyoripotiwa kwenye vyombo vya habari hivi karibuni? Au je, kuna uhusiano na tozo mpya za mabenki?

Idadi kubwa ya wastaafu wana marejesho ya mikopo ya benki yanayokatwa moja kwa moja kupitia mafao yao ya kila mwezi. Kama ni kweli kuna tatizo je, mabenki yatalichukuliaje jambo hili ukizingatia kuwa tatizo halijasababishwa na wateja wao?
imelipwa
 
Mkuu na wewe unadoea pesa za urithi za mzazi

Mkuu huna akili, Kelele kibao kumbe unachungulia pensheni ya mzazi kila mwezi

Hiyo ni pesa ya Mzee acha ajilie, Watoto wa siku hizi hamna maana

Mtu unafuatilia pension ya mzazi kama yako

Teh Teh teee, Jamii F psychological unatambua miserable behaviour za watu wengi kama wewe mfuatilia pension ya mzazi kama yako
 
Imekuwa kama kawaida malipo ya pensheni ya kila mwezi kwa mfuko wa PSSSF yanakuwa tayari kila tarehe 24 ya mwezi. Mfuko pia unatuma ujumbe(sms) unaompa taarifa mstaafu kuwa malipo hayo yameshatumwa benki.

Hii ni tofauti na mwezi huu wa Agosti ambapo malipo hayafanyika na taarifa iliyozoeleka pia haijatumwa. Je, kuna tatizo au ndiyo fedha za wastaafu zilizopigwa kama ilivyoripotiwa kwenye vyombo vya habari hivi karibuni? Au je, kuna uhusiano na tozo mpya za mabenki?

Idadi kubwa ya wastaafu wana marejesho ya mikopo ya benki yanayokatwa moja kwa moja kupitia mafao yao ya kila mwezi. Kama ni kweli kuna tatizo je, mabenki yatalichukuliaje jambo hili ukizingatia kuwa tatizo halijasababishwa na wateja wao?

Wewe ni mstaafu kweli? Au unanyemelea hela za aliyestaafu hapo? Maana kama hela hujaziona si uendee ofisi za PSSSF zilizo karibu na wewe watakueleza? I doubt kama kweli wewe ni pensioner maana hela zilitoka tangu 22/08.
 
Back
Top Bottom