Kakulwa P
JF-Expert Member
- Feb 8, 2012
- 200
- 72
Ndugu zangu wanaJF Salam,
Nimesikia mwenyewe kauli ya Balozi Sefue akitaja wajumbe wa Tume ya Kuratibu maoni ya Katiba watavyonufaika wakati wa utekelezaji wa kazi zao, alitaja yafuatayo kwa kila mjumbe.
1. Kupewa Gari Jipya
2. Kupewa Nyumba
Lingine nimesikia kuwa wanalipwa posho ya shilingi 450,000/- kila siku.
Ndugu zangu kamati hii ina wajumbe 30 toka maeneo ya Jamhuri yetu ya Muungano, lakini pia hawa wajumbe wametoka kwenye taasisi mbalimbali kunazia bungeni, vyuoni, vyama vya siasa na maeneo mengine ili mradi wamekidhi sifa ambazo Marais wetu aliona zinafaa.
1. Naanza kuhoji juu ya kupewa magari ya tume, mimi ninavyowajua wajumbe wote wa Tanzania bara wanayo magari yao wanayoyatumia kila siku, kwa nini serikali haikupenda kuwawekea mafuta tu ili waweze kwenda kazini kila siku badala ya kuingia gharama kubwa za kununua magari mapya. Hapo tungepunguza fadha nyingi na kuzifanyia shughuli nyingine ya maendeleo ya wananchi wetu.
2. Wajumbe wote waliopo Tanzania bara wanazo nyumba zao wanapoishi, sasa hizi nyumba wanazopewa na serikali hazina ulazima labda kwa wale wajumbe wa Tanzania visiwani ambao watakuja kwa kazi hizi maalum.
3. Posho 450,000/-wa siku ni kiasi kikubwa mno kulingana na maisha duni ya wananchi kwenye nchi hii, nilikuwa na matarajio makubwa kuwa wajumbe hawa wangekataa kiasi hicho kikubwa lakini wamekaa kimya tangu walipotangaziwa wanachokiita NEEMA KWAO.
WanaJF wenzangu kwa mfumo huu wa kutanguliza maslahi manono kwa wajumbe wa Kamati ya Katiba, na mkiangalia muda ambao wameupanga, masaa matatu kila Tarafa kwenye kutoa maoni kutoka kwa wananchi tunatarajia KATIBA YA WATANZANIA? Nalileta hili ambalo mimi nimeona kama kikwazo ili tusaidiane kulisema.
Nimesikia mwenyewe kauli ya Balozi Sefue akitaja wajumbe wa Tume ya Kuratibu maoni ya Katiba watavyonufaika wakati wa utekelezaji wa kazi zao, alitaja yafuatayo kwa kila mjumbe.
1. Kupewa Gari Jipya
2. Kupewa Nyumba
Lingine nimesikia kuwa wanalipwa posho ya shilingi 450,000/- kila siku.
Ndugu zangu kamati hii ina wajumbe 30 toka maeneo ya Jamhuri yetu ya Muungano, lakini pia hawa wajumbe wametoka kwenye taasisi mbalimbali kunazia bungeni, vyuoni, vyama vya siasa na maeneo mengine ili mradi wamekidhi sifa ambazo Marais wetu aliona zinafaa.
1. Naanza kuhoji juu ya kupewa magari ya tume, mimi ninavyowajua wajumbe wote wa Tanzania bara wanayo magari yao wanayoyatumia kila siku, kwa nini serikali haikupenda kuwawekea mafuta tu ili waweze kwenda kazini kila siku badala ya kuingia gharama kubwa za kununua magari mapya. Hapo tungepunguza fadha nyingi na kuzifanyia shughuli nyingine ya maendeleo ya wananchi wetu.
2. Wajumbe wote waliopo Tanzania bara wanazo nyumba zao wanapoishi, sasa hizi nyumba wanazopewa na serikali hazina ulazima labda kwa wale wajumbe wa Tanzania visiwani ambao watakuja kwa kazi hizi maalum.
3. Posho 450,000/-wa siku ni kiasi kikubwa mno kulingana na maisha duni ya wananchi kwenye nchi hii, nilikuwa na matarajio makubwa kuwa wajumbe hawa wangekataa kiasi hicho kikubwa lakini wamekaa kimya tangu walipotangaziwa wanachokiita NEEMA KWAO.
WanaJF wenzangu kwa mfumo huu wa kutanguliza maslahi manono kwa wajumbe wa Kamati ya Katiba, na mkiangalia muda ambao wameupanga, masaa matatu kila Tarafa kwenye kutoa maoni kutoka kwa wananchi tunatarajia KATIBA YA WATANZANIA? Nalileta hili ambalo mimi nimeona kama kikwazo ili tusaidiane kulisema.