gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,274
- 20,673
Hodi wana jf nakuja kwenu kwa mara ya kwanza nikiwa nimetingwa na lillonisibu mchana huu juu ya malezi ya wanetu.
naomba mnisaidie majibu hasa ya kunielewesha manake kama shule basi basi nimeshafeli.
niko nyumbani hapa na wanangu wawili mmoja ana miaka 6 na mwingine miaka 3 wote ni wa kiume. sasa walikuwa wanacheza na toys hapa, huyu mkubwa akawa anamsumbua mdogo wake mara kwa kumtuma tuma. mara amwambie chukua gari hili weka hapa mara leta treni ieke hapa, mara leta ufagio mimi kama mama nikakwazika. ndipo nilipomwambia mwanangu mkubwa usimchoshe mwanangu. nakiri kwamba nilisema maneno haya kwa lugha ya ukali kidogo napia huyu mdogo hakuwa amechukia japo ndiye aliyekuwa anatumwa.
sikujua kama kaka mtu kakasirika kwa maneno niliyo mwambia ghafla alikaa kimya na mimi sikumzingatia, ndipo aliponiuliza hivi mama kwani mimi siyo mwanao? nikashtuka nikamjibu ni wanangu tena mkubwa akasema kwanini sasa unasema nisimchoshe mwanao? inamaana wewe unampendelea tu HUYO MWANAO KULIKO mimi.
jamani nimeumizwa sana na haya maneno. hebu nisaidieni wana jf na wajuzi wa malezi, nataka niwalee wote kwa usawa. kwani wote nime wazaa mimi na kwa baba mmoja.
naomba mnisaidie majibu hasa ya kunielewesha manake kama shule basi basi nimeshafeli.
niko nyumbani hapa na wanangu wawili mmoja ana miaka 6 na mwingine miaka 3 wote ni wa kiume. sasa walikuwa wanacheza na toys hapa, huyu mkubwa akawa anamsumbua mdogo wake mara kwa kumtuma tuma. mara amwambie chukua gari hili weka hapa mara leta treni ieke hapa, mara leta ufagio mimi kama mama nikakwazika. ndipo nilipomwambia mwanangu mkubwa usimchoshe mwanangu. nakiri kwamba nilisema maneno haya kwa lugha ya ukali kidogo napia huyu mdogo hakuwa amechukia japo ndiye aliyekuwa anatumwa.
sikujua kama kaka mtu kakasirika kwa maneno niliyo mwambia ghafla alikaa kimya na mimi sikumzingatia, ndipo aliponiuliza hivi mama kwani mimi siyo mwanao? nikashtuka nikamjibu ni wanangu tena mkubwa akasema kwanini sasa unasema nisimchoshe mwanao? inamaana wewe unampendelea tu HUYO MWANAO KULIKO mimi.
jamani nimeumizwa sana na haya maneno. hebu nisaidieni wana jf na wajuzi wa malezi, nataka niwalee wote kwa usawa. kwani wote nime wazaa mimi na kwa baba mmoja.