SoC03 Malezi ya Mtoto hutoa mwelekeo katika maisha yake

Stories of Change - 2023 Competition

Thomson001

New Member
Jul 23, 2023
1
1
Mtoto ni hazina ya taifa.
Malezi ya mtoto huanza pale anapozaliwa na kuanza kujenga uhusiano baina ya mtoto na mzazi au mlezi wake.
Naposema malezi bora aidha kutoka kwa mzazi wake au mlezi hupelekea mwelekeo au dira ya mtoto kama wahenga walivyosema "mtoto umleavyo ndivyo akuavyo" hapa tunaongelea jinsi malezi yanaweza kuchagiza kwa namna fulani katika maendeleo yake ukubwani ikiwa pamoja na kiakili, kijamii, kibayolojia, kisaikolojia na kiafya.
Hii inasaidia kwenye kumjengea mtoto uwezo wa kujiamini, kujielezea mbele ya umati, kushirikiana na wenzake katika kazi za kijamii, kuweza kuelezea mambo yanayomsibu ama anayokumbana nayo kwenye maisha yake.
Mara nyingi baadhi ya wazazi au walezi wanaopewa mtoto ili wamlee wamekuwa wanatengeneza uhusiano usio sahihi baina yake na mtoto mfano kumfokea bila sababu ya msingi, kumtukana na pengine kumpa vitisho vikali.
Hii inamjengea saikolojia ya uwoga, hofu na wasiwasi pale anapotaka kumueleza mzazi au mlezi wake mambo yanayomsibu.

Kwanini baadhi ya watoto wanajiamini na wana ujasiri mkubwa kuliko wengine?

Je, nini kifanyike?

Watoto ni taifa la kesho, hivyo ni jukumu letu sote kama jamii kujenga taifa bora!!!.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…