Malezi ya baba yameniathiri, napata tabu sana kuishi na watu

B love

JF-Expert Member
Jul 20, 2022
244
567
Kama ilivyokuwa kwa familia nyingi za kikwetu inapoanza migogoro ya kindoa haijawahi waacha watoto salama.
Nikiwa kinda sana kwenye miaka ya 1995/96 wazee waliingia mtafaruku na kujikuta wameachana hivyo kusababisha mgawanyiko wa watoto kimalezi mana MAMA alibakia na baadhi ya watoto na BABA alichukua baadhi ya watoto nikiwemo mimi (Kwa kipindi hicho nilikuwa kama na miaka 5 a 6).

BABA alidhamiria kutulea watoto wake mwenyewe mpaka tulipofikisha umri flani ivi wa kujielewa kisha akaja kuowa mwanamke mwingine, hivyo asilimia kubwa ya malezi, tabia na mafunzo tumeyapata mikononi kwa BABA.

BABA alikuwa ni aina ya watu wenye IQ kubwa, majasiri, wenye misimamo na sio mwenye kutawaliwa na hisia. Alikuwa akitupa kazi/majukumu anawekea na deadline ya kutekeleza majukumu hayo, alipenda tufanye kazi kwa speed na ubora na si kulipua wala kulala lala. Hakuamini kwenye kumuonea mtu huruma ispokuwa kumpa stahiki yake, hakuamini kwenye kumuonesha mtoto mapenzi hivyo hakuna aliyejua kama anapendwa pia hakuwa na muda mwingi wa story na watu muda mwingi huwa mwenyewe na kazi zake kitu kilichopelekea kuogopwa na majirani na wanakijiji kwa ujumla na kusababisha hata sisi wanawe kuogopwa na watoto wenzetu na kukosa marafiki na hata walojitoa kuwa karibu na sisi walifokewa na wazazi wao pia hawakuwa wana enjoy urafiki coz mipaka ilikuwa mingi hivyo hawakuwa huru kuja home wala kucheza na sisi labda muda tukiwa shule pekee. Mzee alikuwa aina ya wale WAZEE ambao wakiingia nyumbani panakuwa kama kuna msiba yani panapoa na kila mtu anachukua position yake akisubiri kuitwa kuhojiwa kwa maendeleo ya shule au kama kuna mashtaka dhidi yake. Hakuamini kwenye kuombaomba, kukopeshwa wala kumuhadithia mtu changamoto zake hivyo alikuwa anakomaa nazo kisabuni.

Kupitia malezi hayo tulijikuta tuki Adapt baadhi ya tabia kila mmoja wetu pasi na sisi kujijua. Kwa upande wangu toka nikiwa shule nikawa mtu naependa vitu vilivyonyooka , sipendi ku reason wala kulalamika hovyo, nikawa nijukuta nina marafiki wachache mno na nisio dum nao. Nikawa muda mwingi napenda kuwa mwenyewe na kutafakari. Napenda tukikubariana kufanya jambo tulifanye kwa wakati na ubora na sipendi kuweka masihara kwenye vitu sereous.

Kwa sasa napitia changamoto katika kuishi na watu hasa jamii zetu za asili maana natafsiriwa kama mtu nisiejali, mkorofi, nina maswali mengi, amri nyingi na najiskia. Nimechumbia zaidi ya mara 4 naghairi na kwingine nakuwa nimekwisha lipa na mahali kabisa ila nina samehe, sababu kubwa ni wenza hao kushindwa kuvumilia speed yangu ya utendaji, kutokuwa na muda nao mwingi wa kuongea nao au kuwa nao pamoja kulingana na hali yangu ya kujali mambo yangu zaidi. Mapenzi ndio kabisa yalinishindaga kitambo toka nipo advnc sijawahi kudum na Mwanamke miezi 6 kisa kuonekana sijali na m binafsi sana.

Kazini napitia changamoto za migogoro na wenzangu kwa tabia za kutaka mambo yalionyoka, sipendi braabraa na huwa si mtu wa story sana nikiona tabia za mtu zitaniathiri kwenye mambo yangu nitamwambia mara moja tu mtu ajirekebeshe kwa yale ninayoamini mimi anakosea, japo nakuwa napendwa sana na mabosi kwa utendaji na u sereous wangu kitu ambacho najihisi nakuwa chanzo cha kugombanisha watumishi na mabosi zao kwa upande mmoja kunichukia kuona najipendekeza na kujiona mimi najua huku upande mwingine kuwaona wenzangu hawafanyi kazi yao ipasavyo kwa kulinganisha na mimi. Tatizo hili limenifanya niache kazi mara kadhaa mana huwa sipendi migogoro.

Kwa kifupi mwenzenu napitia changamoto hizo hasa nikiwa nyumbani Afrika mana kwa shughuli zangu nafanyia nje zaidi. Kwa aliyepitia aina hii ya malezi na hayuko kama mimi naomba anisaidie nini cha kufanya na ambao mnapitia challenge kama zangu naomba tupeane uzoefu.
 
Buuu huuu huuu,acha kulia lia mkuu,hata Jiwe linajua kuadapt na nature,sembuse wewe mwenye utashi?ushajua janga lilipoanzia,unashindwaje kujijengea ufalme wako,Mzee wako kafanya kazi yake,na wewe Anza kufanya yako.Acha kumsingizia Mzee.
 
Aisee kama mzee wangu tu.

Nimekua nikiona picha ya mwanaume au Baba kuwa kama na tabia hizo ulizotaja tena bahat mbaya mimi nimeshuhudia baba yangu akipigana mara kibao na watu tena mpambank haswa.

nimeshuhudia baba yangu akipiga watu mabapa ya panga na kichapo hevi. na ilipelekea mimi kuwa na tabia hizi

1.Mkali na siyo kuchekacheka na ujinga

2.Ujasiri wa hali ya Juu(Naweza nkarusha ngumi mahali ambapo palitakiwa kuongea.)
Nakumbuka nilishawahi kumpiga ngumu shemasi wa kanisa katikat ya ibada kwasababu ya kumfinya mwanangu

3.Uonevu na kupenda ugomvi kupitiliza. yani nkipita sehemu nkakuta ugomvi huwa natamani kuiingilia

4. Huwa siogopi mtu na kama hanionyeshi heshima siwez kumheshimu hata awe na umri gani.

5.Hasira za mara kwa mara(Mke wangu anajitahidi kunirekebisha ila mdogomdogo lbda ntabadilika)

6.naamini hakuna mtu anaweza kunirekebisha wala kunizidi uwezo wa akili ndo mana sishirikishi mtu jambo langu.

7.Sina rafiki hata mmoja.(nakufa na shida zangu)

8.Sijawahi kujishusha zaidi ya upande wa MUUMBA

9.Sitaki mazoea ya kipumbavu

10.Sina ndugu yyte zaidi ya wazazi na siblings.(wapo ila sina muda nao na sitaki kujuana)

11.Sina unafiki ukinikera nakuchana popote napokuona na upende usipende utajua wewe.

12.Narudia tena. NAPENDA KUPIGANA Na kuna muda namiss pambano kbsa.

13.Sura iko serious muda wote baadhi ya watu wanamuuliza wife kama nachekaga au laa
wengine wanajua mimi ni mwanajeshi kumbe siyo

-mpka leo mama yangu anasikitika kuwa nimekuwa copy and paste ya mzee.

-Nilishawahi kupigana na madereva bajaji 3 nikiwa nimelewa wakanitandika sawasawa ila mmoja wao nilimvunja mbavu ya chini kushoto


NAHISI NAHITAJI MTAALUM WA SAIKOLOJIA ILI NIBADILIKE
 
Buuu huuu huuu,acha kulia lia mkuu,hata Jiwe linajua kuadapt na nature,sembuse wewe mwenye utashi?ushajua janga lilipoanzia,unashindwaje kujijengea ufalme wako,Mzee wako kafanya kazi yake,na wewe Anza kufanya yako.Acha kumsingizia Mzee.

Mwanadamu ni mwanafunzi kwenye kila hatua
AJifunze
 
Aisee kama mzee wangu tu.

Nimekua nikiona picha ya mwanaume au Baba kuwa kama na tabia hizo ulizotaja tena bahat mbaya mimi nimeshuhudia baba yangu akipigana mara kibao na watu tena mpambank haswa.

nimeshuhudia baba yangu akipiga watu mabapa ya panga na kichapo hevi. na ilipelekea mimi kuwa na tabia hizi

1.Mkali na siyo kuchekacheka na ujinga

2.Ujasiri wa hali ya Juu(Naweza nkarusha ngumi mahali ambapo palitakiwa kuongea.)
Nakumbuka nilishawahi kumpiga ngumu shemasi wa kanisa katikat ya ibada kwasababu ya kumfinya mwanangu

3.Uonevu na kupenda ugomvi kupitiliza. yani nkipita sehemu nkakuta ugomvi huwa natamani kuiingilia

4. Huwa siogopi mtu na kama hanionyeshi heshima siwez kumheshimu hata awe na umri gani.

5.Hasira za mara kwa mara(Mke wangu anajitahidi kunirekebisha ila mdogomdogo lbda ntabadilika)

6.naamini hakuna mtu anaweza kunirekebisha wala kunizidi uwezo wa akili ndo mana sishirikishi mtu jambo langu.

7.Sina rafiki hata mmoja.(nakufa na shida zangu)

8.Sijawahi kujishusha zaidi ya upande wa MUUMBA

9.Sitaki mazoea ya kipumbavu

10.Sina ndugu yyte zaidi ya wazazi na siblings.(wapo ila sina muda nao na sitaki kujuana)

11.Sina unafiki ukinikera nakuchana popote napokuona na upende usipende utajua wewe.

12.Narudia tena. NAPENDA KUPIGANA Na kuna muda namiss pambano kbsa.

13.Sura iko serious muda wote baadhi ya watu wanamuuliza wife kama nachekaga au laa
wengine wanajua mimi ni mwanajeshi kumbe siyo

-mpka leo mama yangu anasikitika kuwa nimekuwa copy and paste ya mzee.

-Nilishawahi kupigana na madereva bajaji 3 nikiwa nimelewa wakanitandika sawasawa ila mmoja wao nilimvunja mbavu ya chini kushoto


NAHISI NAHITAJI MTAALUM WA SAIKOLOJIA ILI NIBADILIKE
Sidhani kama wewe ni nunda. Bondia huwa haonei bali anatetea, wewe unaoea yaani ni muonevu. Wewe ni msela mavi na mshamba tu fulani.
 
Buuu huuu huuu,acha kulia lia mkuu,hata Jiwe linajua kuadapt na nature,sembuse wewe mwenye utashi?ushajua janga lilipoanzia,unashindwaje kujijengea ufalme wako,Mzee wako kafanya kazi yake,na wewe Anza kufanya yako.Acha kumsingizia Mzee.
Sawa. Ila tambua kwamba me naona nikosawa ispokuwa watu wanaonizunguka kuna vitu wanaona siwatendei haki kulingana na misimamo yangu. Na ukiangalia most of behaviors sio mbaya ila napata tabu kuishi na jamii ambayo ipo kinyume changu.
 
Wewe unatakiwa kuwa CEO , hustahili kufanya kazi na wafanyakazi wenzako. Unatakiwa uwe na kampuni yako ili uwaendeshe wafanyakazi wako vile unataka.
Pamoja na kuwa CEO wa tu miradi twangu kadhaa ila bado pia nafanya kazi na mashirika na serikali na nakuwa chini ya watu. Sijawahi jutia hili
 
Aisee kama mzee wangu tu.

Nimekua nikiona picha ya mwanaume au Baba kuwa kama na tabia hizo ulizotaja tena bahat mbaya mimi nimeshuhudia baba yangu akipigana mara kibao na watu tena mpambank haswa.

nimeshuhudia baba yangu akipiga watu mabapa ya panga na kichapo hevi. na ilipelekea mimi kuwa na tabia hizi

1.Mkali na siyo kuchekacheka na ujinga

2.Ujasiri wa hali ya Juu(Naweza nkarusha ngumi mahali ambapo palitakiwa kuongea.)
Nakumbuka nilishawahi kumpiga ngumu shemasi wa kanisa katikat ya ibada kwasababu ya kumfinya mwanangu

3.Uonevu na kupenda ugomvi kupitiliza. yani nkipita sehemu nkakuta ugomvi huwa natamani kuiingilia

4. Huwa siogopi mtu na kama hanionyeshi heshima siwez kumheshimu hata awe na umri gani.

5.Hasira za mara kwa mara(Mke wangu anajitahidi kunirekebisha ila mdogomdogo lbda ntabadilika)

6.naamini hakuna mtu anaweza kunirekebisha wala kunizidi uwezo wa akili ndo mana sishirikishi mtu jambo langu.

7.Sina rafiki hata mmoja.(nakufa na shida zangu)

8.Sijawahi kujishusha zaidi ya upande wa MUUMBA

9.Sitaki mazoea ya kipumbavu

10.Sina ndugu yyte zaidi ya wazazi na siblings.(wapo ila sina muda nao na sitaki kujuana)

11.Sina unafiki ukinikera nakuchana popote napokuona na upende usipende utajua wewe.

12.Narudia tena. NAPENDA KUPIGANA Na kuna muda namiss pambano kbsa.

13.Sura iko serious muda wote baadhi ya watu wanamuuliza wife kama nachekaga au laa
wengine wanajua mimi ni mwanajeshi kumbe siyo

-mpka leo mama yangu anasikitika kuwa nimekuwa copy and paste ya mzee.

-Nilishawahi kupigana na madereva bajaji 3 nikiwa nimelewa wakanitandika sawasawa ila mmoja wao nilimvunja mbavu ya chini kushoto


NAHISI NAHITAJI MTAALUM WA SAIKOLOJIA ILI NIBADILIKE
Vitu kama hivi vinakuwaga kwenye gene. Sijui unafanyaje tuu sasa kuviepuka. Binafsi hakuna kitu sipendi kama ugomvi. Uwe wa kurushiana ngumi ama wa maneno.
 
Vitu kama hivi vinakuwaga kwenye gene. Sijui unafanyaje tuu sasa kuviepuka. Binafsi hakuna kitu sipendi kama ugomvi. Uwe wa kurushiana ngumi ama wa maneno.
Halafu anajisifia kuwa ni muonevu.
 
Aisee kama mzee wangu tu.

Nimekua nikiona picha ya mwanaume au Baba kuwa kama na tabia hizo ulizotaja tena bahat mbaya mimi nimeshuhudia baba yangu akipigana mara kibao na watu tena mpambank haswa.

nimeshuhudia baba yangu akipiga watu mabapa ya panga na kichapo hevi. na ilipelekea mimi kuwa na tabia hizi

1.Mkali na siyo kuchekacheka na ujinga

2.Ujasiri wa hali ya Juu(Naweza nkarusha ngumi mahali ambapo palitakiwa kuongea.)
Nakumbuka nilishawahi kumpiga ngumu shemasi wa kanisa katikat ya ibada kwasababu ya kumfinya mwanangu

3.Uonevu na kupenda ugomvi kupitiliza. yani nkipita sehemu nkakuta ugomvi huwa natamani kuiingilia

4. Huwa siogopi mtu na kama hanionyeshi heshima siwez kumheshimu hata awe na umri gani.

5.Hasira za mara kwa mara(Mke wangu anajitahidi kunirekebisha ila mdogomdogo lbda ntabadilika)

6.naamini hakuna mtu anaweza kunirekebisha wala kunizidi uwezo wa akili ndo mana sishirikishi mtu jambo langu.

7.Sina rafiki hata mmoja.(nakufa na shida zangu)

8.Sijawahi kujishusha zaidi ya upande wa MUUMBA

9.Sitaki mazoea ya kipumbavu

10.Sina ndugu yyte zaidi ya wazazi na siblings.(wapo ila sina muda nao na sitaki kujuana)

11.Sina unafiki ukinikera nakuchana popote napokuona na upende usipende utajua wewe.

12.Narudia tena. NAPENDA KUPIGANA Na kuna muda namiss pambano kbsa.

13.Sura iko serious muda wote baadhi ya watu wanamuuliza wife kama nachekaga au laa
wengine wanajua mimi ni mwanajeshi kumbe siyo

-mpka leo mama yangu anasikitika kuwa nimekuwa copy and paste ya mzee.

-Nilishawahi kupigana na madereva bajaji 3 nikiwa nimelewa wakanitandika sawasawa ila mmoja wao nilimvunja mbavu ya chini kushoto


NAHISI NAHITAJI MTAALUM WA SAIKOLOJIA ILI NIBADILIKE
Hapa baba hana haja ya DNA unakuta baba mkorofi mtoto mpole, yaani hamu endani kabisa. Unajua hii mbegu sio yanguuuu
 
Back
Top Bottom