Ncha Kali
JF-Expert Member
- Sep 19, 2019
- 14,523
- 27,016
Aisee leo nimepanic kwa ghadhabu, hata nimesahau kuwasalimia.
Nina vijana wangu watatu wa kiume wote, umri wao ni miaka 13, 12 na 8 ambao nawalea mwenyewe [singo dadi] baada ya kutelekezwa na mama zao. Ni vijana watulivu kwa tabia, wenye heshima japo utundu ni kawaida na changamoto za hapa na pale kwa sababu ya makuzi.
Basi bwana leo yamenikuta, ile kujifanya mpekuzi, nimefukunyua moja ya sanduku lao nikaibuka na mshangao na butwaa. Nikafurusha ‘vinguo vya kike’ katika moja ya ‘zip’ vilivyokunjwa na kuhifadhiwa kwa ustadi mkubwa.
Ni kiblauzi na kisketi, makadirio labda binti wa miaka 12 hivi umbile la wastani, nimesikitika na kukaa Irina kwa wakati mmoja.
Nikafanikiwa kujizuia na kuvirudishia kama vilivyokuwa, nipate kwanza utulivu na ushauri wa mbinu gani nitumie ili kujua ukweli.
Kwa haraka haraka nimewaza hawa madogo wameshaanza kutafuna, na je hizi nguo wamepora kwa binti wa watu wamepewa au wamenunua kwa lengo la kupeleka zawadi..?
Maswali ni mengi sana wakuu, nimefanikiwa kudhibiti ghadhabu yangu hadi hapa sijasema kitu, natafuta namna bora kabisa ya kujua ukweli wa hili.
Hebu tupeane mawili matatu, napenda sana utani ila linapokuja suala la watoto nasimama juu ya mstari, sina uzoefu zaidi na malezi ila napambana kwa kila namna ninayoweza na inayofaa hivyo nakubali mapungufu.
YAMENIFIKA HAPA.
Nina vijana wangu watatu wa kiume wote, umri wao ni miaka 13, 12 na 8 ambao nawalea mwenyewe [singo dadi] baada ya kutelekezwa na mama zao. Ni vijana watulivu kwa tabia, wenye heshima japo utundu ni kawaida na changamoto za hapa na pale kwa sababu ya makuzi.
Basi bwana leo yamenikuta, ile kujifanya mpekuzi, nimefukunyua moja ya sanduku lao nikaibuka na mshangao na butwaa. Nikafurusha ‘vinguo vya kike’ katika moja ya ‘zip’ vilivyokunjwa na kuhifadhiwa kwa ustadi mkubwa.
Ni kiblauzi na kisketi, makadirio labda binti wa miaka 12 hivi umbile la wastani, nimesikitika na kukaa Irina kwa wakati mmoja.
Nikafanikiwa kujizuia na kuvirudishia kama vilivyokuwa, nipate kwanza utulivu na ushauri wa mbinu gani nitumie ili kujua ukweli.
Kwa haraka haraka nimewaza hawa madogo wameshaanza kutafuna, na je hizi nguo wamepora kwa binti wa watu wamepewa au wamenunua kwa lengo la kupeleka zawadi..?
Maswali ni mengi sana wakuu, nimefanikiwa kudhibiti ghadhabu yangu hadi hapa sijasema kitu, natafuta namna bora kabisa ya kujua ukweli wa hili.
Hebu tupeane mawili matatu, napenda sana utani ila linapokuja suala la watoto nasimama juu ya mstari, sina uzoefu zaidi na malezi ila napambana kwa kila namna ninayoweza na inayofaa hivyo nakubali mapungufu.
YAMENIFIKA HAPA.