Malcom X: Ni kipi kirefu cha hiyo 'X'?


Jina halisi la Malcolm X ni Malcolm little
Malcolm ni Black american,wakati ubaguzi wa rangi ulivyokuwa umeshamiri kule Marekani
wazungu[slave's masters wa wakati ule]walikuwa na kawaida ya kuwapa majina ya kejeli na dharau watoto wa Ki-negro,mathalani
Little ina maana ya kitu kidogo au dhaifu

Baada ya kuona hivyo,Malcolm akaamua kuondoa Jina la 'little' na kuweka X

Nini maana ya herufi X?
X kwa kawaida hutumika kuwakilisha kitu kisichojulikana au usichokijua
Malcolm alichagua herufi X kuwakilisha Jina la Babu au mababu zake kutoka Afrika,ambayo yeye alikuwa hayajui.
Pia X inatumika kuonyesha asili ya mtu mweusi ambayo imepotezwa na utandawazi

Oya nafikiri umenielewa,Btw karibu sana mkuu!
JI ndiyo jukwaa pendwa hapa JF.
 
Last edited:
Very clever...na wale wamejipa majina ya kiswahili kama akina Karenga,Cheo,Mfalme Kabisa,Zuri Jones,etc

Hawa jamaa wananifurahishaga,wanakumbuka sana kwao

Hewa mmoja kama Marion "Suge" Knight anasema hataki waitwe African Americans kwani anaamini hawajatoka Africa neccesarily,duh..huyu jamaa kilaza sana
 

Kwa upande mwingine yuko sahihi kwa sababu African Americans wengi sana wamechanganya damu.

Wengi wamechanganya damu na Wazungu na Wahindi wekundu.

Hivi hujawahi kugundua kwamba hata kimuonekano wako tofauti kwa kiasi flani na Waafrika?

Ukimwona Michelle Obama huoni kama ana features kama kachanganya damu?

Ukimwona Whitney Houston huoni kwamba kachanganya damu?

Mwangalie tu hata Martin Luther King Jr., Malcolm X, W.E.B. DuBois, na wengineo.

Kwa hiyo, huyo Suge kusema hivyo ana hoja ya msingi kabisa.

Kwa nini waitwe tu African Americans tu wakati wana na heritage ya Ulaya na Wahindi wekundu?
 
Hata mimi umenifungua macho nilikuwa cjui
 
Umemjibu vizuri sana, kuna Mwl wangu flani wa History Alijibu Hivi Hivi nikiwA secondary!
 


Kula like za kutosha
 
Hata mi nimeelewa vizuri sana
 
Safi sana, umefafanua vizuri mno
 

= wananifurahisha

Wakati wewe ndiyo kwanza umejipa id ya majina hayo wanayoyakataa hao wanaokufurahisha. Unanshangaza!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…