BashiriOnline
Senior Member
- Nov 5, 2012
- 127
- 44
Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa leo hii nchini Malaysia kwa ajili ya uchaguzi wa kwanza katika historia ya taifa hilo kuwepo kwa uwezekano wa mabadiliko ya serikali, kutokana na utawala huo uliyodumu kwa miongo kadhaa ukipambana kuuzuwia upinzani unaotaka kufanya mabadiliko. Vituo vya kupiga kura vimefunguliwa mapema asubuhi baada ya kuhitimishwa kampeni ya vuta nikuvute hapo jana ambapo wapinzani walionesha shaka kwa kuwepo kwa udanganyifu na kukiukwa kwa taratabu kwa serikali ya muungano inayotawala taifa hilo ambayo pia imekanusha kuwa na malengo yeyote ya kufanya wizi wa kura.
Vituo vya kupigia kura vitafungwa saa 11 jioni na kwamba matokeo yanatarajiwa kuanza kutolewa saa chache baada ya kuhitimishwa zoezi hilo
Vituo vya kupigia kura vitafungwa saa 11 jioni na kwamba matokeo yanatarajiwa kuanza kutolewa saa chache baada ya kuhitimishwa zoezi hilo