Makuwadi wa DP wanahaha kutaka Mkutano wa Kutetea Bandari zetu usifanikiwe

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,566
41,082
Kati ya watu wamekuwa mstari wa mbele kuupigia debe mkataba wa kishenzi wa bandari, kwa upande wa wanahabari, ni bwana Kitenge. Huyu jina lake linajitokeza miongoni mwa wanaotajwa kupokea hongo ili kuusifia mkataba wa hovyo wa bandari. Na muda mwingi amegharamiwa na DP safari zake kwenda huko Dubai.

Katika kila uovu dhidi ya Taifa, ili uweze kufanikiwa, na lazima uwepo usaliti wa ndani. Hivyo haishangazi kuona katika huu uharamia wa kuporwa kwa bandari za Tanganyika, tunao wasaliti wa ndani.

Jana usiku, Kitenge kwenye online blog yake kaweka taarifa eti kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa amepiga marufuku mkutano ulioandaliwa na CHADEMA kuzungumzia uhovyo wa mkataba wa bandari.

Huyu bwana, sijui ni kutokana na kupofushwa, uelewa mdogo au kuna sababu nyingine, hajui hata mamlaka ya Msajili wa Vyama vya Siasa. Hajui kuwa kuruhusu au kuzuia mikutano ya vyama vya siasa siyo miongoni mwa mamlaka ya msajili wa vyama vya siasa.

Watu wajinga wasiojua sheria, waliopofushwa iwe kwa rushwa, upendeleo au fadhila, tuwapuuze kwa sababu hawajitambui.

Kitenge anahangaika ili sauti za Watanganyika zisisikike, bila shaka kwa nia ya kumridhisha anayemkuwadia kuwa amefanya kazi kubwa na amefanikiwa kuwafanya Watanganyika wote kuwa wajinga, na sasa wanashangilia mkataba wa hovyo.

Makuwadi na mawakala hawatashinda katika vita hii ya kulinda rasilimali za Taifa letu. Watu wema wanaopigania ulinzi wa Taifa letu, hakika watashinda. Twende kwenye mikutano, huu na mingine mingi itakayofanyika, bila ya kujali imeandaliwa na nani, tukaoneshe umoja wetu katika kupambania Utaifa na heshima ya Taifa letu. Tutaendelea kuwakaribisha wawekezaji lakini tutazuia waporaji wa rasilimali zetu.

Tunamwomba Mungu wetu azidi kutuimarisha katika mapambano haya ya kulinda kile ambacho Mungu alitujalia hapa Duniani, kwa maisha yetu na yale ya wale watakaokuja. Na awalaani makuwadi na mawakala wote wa uovu dhidi ya rasilimali za Taifa letu. Tunaomba, laana ya Mungu ikawe juu yao, wana wao na wana wa wana wao.
 
F1UiZJxXsAEko7V.jpeg
 
Hiyo Kitenge ajibu hizi hoja
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Hiyo Kitenge ajibu hizi hoja
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

Majibu yake yanahitaji IQ Kubwa…
 
Siku zinavyozidi kusogea ndio nazidi kumuona Kitenge alivyo mpuuzi, mwanzo nilimchukulia kama opportunist, lakini sikufikiri kama anaweza kwenda mbali kiasi hiki, amefikia hatua haioni tena thamani ya ardhi yake, na rasilimali zake, mbele ya vipande vya fedha.
Watu wa namna hii ya Kitenge ni hatari sana. Hawa ndiyo watu ambao huwa wapo tayari hata kuondoa uhai wa mtu kwa sababu ya vipande vya fedha.
 
Sawa tap unakuja soon wote wanaouza bandari ....shaba tuuu.....Hakuna kupepesa macho
 
Tutaendelea kupigania mkataba wenye manufaa kwa Tanganyika, ama wakishindwa waachane nao.
 
Hapa ni kuendelea kuwaminya sehemu nyeti hadi wazitapike hizo walizopewa - Bandari yetu pendwa haiendi popote, bora tufe maskini ila watukuu wetu waikute.
 
Naona clips kuhusu waziri alipewa pesa kibao!
Hivi huyu waziri aliyechukua USD 2 Milioni na kununua appartments Mikocheni ni nani!
 
Back
Top Bottom