Makundi haya kuamua mstakabali wa CCM Dodoma

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,273
Chama cha mapinduzi kinapita kwenye kipindi kigumu kuliko watu wengi wanavyofikiri, hii ni kwakuwa watu wengi wamenyimwa uhuru wakupata habari...

Chama kimegawanyika makundi matatu makubwa ambayo huenda yakazaa enzi mpya baada ya 23/7/2020...

Lipo kundi la Wahafidhina ambalo linaamini kuwa Chama kwa sasa kinahitaji kiongozwe na mwenyekiti mwenye historia ya uzoefu katika siasa na uongozi,

Kundi la pili ni lile la Wafadhiri wa Chama ambalo tangu kuasisiwa kwa mfumo wa wizi ndani ya ccm, lenyewe lilijipa jukumu la kusaidia chama kupitia mlango ya wizi ikiwemo ukwepaji kodi. Hili tayari limeshajeruhiwa na utawala wa Magufuli, na limejidhatiti kuhakikisha linakwenda na kura ya veto kuzuia chama kisikabidhiwa kwa Magufuli, Sababu kuu inaelezwa kuwa kundi hili liligharimia chama mabilioni ya pesa ambapo ilitakiwa kundi hilo lilipwe baada tu ya Rais kuingia madarakani, lakini kinyume na matarajio yao, Rais amezuia malipo hayo na kwamba hayo ni madeni ya chama sio ya nchi.

Kundi la Tatu hili ni mtandao imara wa Mh Lowassa, huu umekaa katikati, kazi yake ni kuwapa elimu ya uraia wanaccm kuwa "jamani ehee, chama ni cha hiyari, mkiona mnanyanyaswa njooni huku aliko mzee wetu, hamuoni anavyoishi vizuri siku hizi?" Furahi ya kundi hili ni kuona ccm inavurugana iwe kwa kupewa JPM uenyekiti ama kwa njia yoyote ile....

Kwa vigezo vyovyote vile vya utawala na uongozi, Rais John Magufuli "anatawala" zaidi kuliko kuongoza, Kokote kule duniani, siasa huongozwa sio hutawaliwa, Hatuna historia ya Uongozi wa aina yoyote wa kisiasa wa John Pombe Magufuli,

Lakini kwenye kutawala tumemuona akihudumu katika Wizara na katika Urais sasa kwa miezi kadhaa, anatawala kwakutilia mkazo zaidi maamuzi yake katika nyanja zote za maisha ya Watanzania kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Hili linafanya kwa wadadisi wa siasa na uongozi aonekane kuwa kero kwenye mizani ya kisiasa na kidemokrasia, sio kwa wapinzani tu bali kwa taifa kwa ujumla, huenda ni ugeni wake katika uongozi ama ni aina yake ya kupendelea kutawala kuliko kuongoza.

Tofauti ya mtawala na kiongozi nikuwa, Kiongozi huongoza kwa kusikiliza anaowaongoza zaidi, na mtawala hutawala yale ayaaminiyo yeye kuwa ni sahihi, yaani zidumu fikra za mkubwa....

Pamoja na takwa la kikatiba nikuwa Rais akabidhiwe uenyekiti, Bado mkutano mkuu unaoketi kesho unayo fursa ya kutengua matakwa hayo ya kikatiba kwa maslahi ya chama na taifa.

Kwamaoni yangu ccm isimpe uenyekiti Magufuli angalau kwa miaka miwili mbele kuelekea 2020.
 
Yericko nani atakuelewa na undumila kuwili wako na kujitoa ufahamu kwako? Mwaka jana uliendesha kampeni ya 'zuia jambazi kwenda ikulu' leo hii jambazi ndiyo muungu wako na unaliita 'mheshimiwa...'. Waacheni CCM wafanye yao, mwaka jana mlisema CCM inaenda kufia Dodoma, haikuwa hivyo, leo tena kelele ni zilezile. Kuweni na busara na fanyeni yenu, isitoshe CCM ikisambaratika ndiyo furaha kwa Vyama Vya Upinzani (VVU), hivyo mpigieni debe Magufuli awe Mwenyekiti ili akiue chama mpate wepesi.
 
Yericko nani atakuelewa na undumila kuwili wako na kujitoa ufahamu kwako? Mwaka jana uliendesha kampeni ya 'zuia jambazi kwenda ikulu' leo hii jambazi ndiyo muungu wako na unaliita 'mheshimiwa...'. Waacheni CCM wafanye yao, mwaka jana mlisema CCM inaenda kufia Dodoma, haikuwa hivyo, leo tena kelele ni zilezile. Kuweni na busara na fanyeni yenu, isitoshe CCM ikisambaratika ndiyo furaha kwa Vyama Vya Upinzani (VVU), hivyo mpigieni debe Magufuli awe Mwenyekiti ili akiue chama mpate wepesi.
Huna haki ya kuzuia watu wasitoe maoni yao mkuu
 
Magufuli atapewa tu.. Huyo asie toa kura kwake atalimia meno..!! Au tuta enjoy wote na huu ugumu wa maisha
 
acha upuuzi wewe!! mshauri mbowe kwanza na lowassa wako na mafisadi waliyokimbilia chadema!!! ngoja nikwambie kitu!! nchi inatakiwa iwe itawaliwe na kuongozwa pia! kwa hiyo mtu Wa sifa zote mbili!! kiongozi aweza kuwa mzuri au mbaya .kama atasikiliza na kuchekea ubaya huyo ni mbaya!! Tanzania imejaa maskini wengi kiuchumi na kiakili na kundi LA wajanja matajiri wachache ambao ndo wameharibu taifa letu kupitia vyama vyao !; hao ukiwasikiliza na kuwachekea taifa haliwezi kusonga mbele!; miaka zaidi ya hamsini ya Uhuru lakini bado nchi hii ni maskini kwa sababu yakulea ujinga na wajanja mpaka ka nchi kama Rwanda kanatucheka na kutudhihaki!! ebu tuwe serious Mr yeriko!!! acha kupotosha watu!! jengeni chama chenu si kwa kutegemea makosa ya CCM au rais!!
 
Tena wewe mnafiki mkubwa
Mikutano ya Ccm ndio huwa mnapata yakuandika
Cdm hampati,


"Kataa lowassa"
"Kataa lowassa"
Nijizi !!!
Hayo maneno mbona hujayafuta !
 
Yericko nani atakuelewa na undumila kuwili wako na kujitoa ufahamu kwako? Mwaka jana uliendesha kampeni ya 'zuia jambazi kwenda ikulu' leo hii jambazi ndiyo muungu wako na unaliita 'mheshimiwa...'. Waacheni CCM wafanye yao, mwaka jana mlisema CCM inaenda kufia Dodoma, haikuwa hivyo, leo tena kelele ni zilezile. Kuweni na busara na fanyeni yenu, isitoshe CCM ikisambaratika ndiyo furaha kwa Vyama Vya Upinzani (VVU), hivyo mpigieni debe Magufuli awe Mwenyekiti ili akiue chama mpate wepesi.

Huyu mtu ni zaidi ya Mnafiki
Full kuchumia tumbo
Ila kwa kiasi Fulani kaanza kuwa na heshima.

Nilitegemea aje na story za Bavicha
Kwenda Dodoma
Sasa anakuja na porojo
 
lini ukaipenda ccm wewe Yericko? yaani wewe wakuishauri CCM? leo unatoa ushauri eti ccm isimpe magufili KITI? aliekutuma mwambie pole ccm ni ile ile, Magufuli saivi anapanga safu yake maridadi kabisa ili azidi kuwapoteza mazima mmbaki tu mitandaon, bora wewe umejiongeza saivi unauza vitabu
 
Chama cha mapinduzi kinapita kwenye kipindi kigumu kuliko watu wengi wanavyofikiri, hii ni kwakuwa watu wengi wamenyimwa uhuru wakupata habari...

Chama kimegawanyika makundi matatu makubwa ambayo huenda yakazaa enzi mpya baada ya 23/7/2020...

Lipo kundi la Wahafidhina ambalo linaamini kuwa Chama kwa sasa kinahitaji kiongozwe na mwenyekiti mwenye historia ya uzoefu katika siasa na uongozi,

Kundi la pili ni lile la Wafadhiri wa Chama ambalo tangu kuasisiwa kwa mfumo wa wizi ndani ya ccm, lenyewe lilijipa jukumu la kusaidia chama kupitia mlango ya wizi ikiwemo ukwepaji kodi. Hili tayari limeshajeruhiwa na utawala wa Magufuli, na limejidhatiti kuhakikisha linakwenda na kura ya veto kuzuia chama kisikabidhiwa kwa Magufuli, Sababu kuu inaelezwa kuwa kundi hili liligharimia chama mabilioni ya pesa ambapo ilitakiwa kundi hilo lilipwe baada tu ya Rais kuingia madarakani, lakini kinyume na matarajio yao, Rais amezuia malipo hayo na kwamba hayo ni madeni ya chama sio ya nchi.

Kundi la Tatu hili ni mtandao imara wa Mh Lowassa, huu umekaa katikati, kazi yake ni kuwapa elimu ya uraia wanaccm kuwa "jamani ehee, chama ni cha hiyari, mkiona mnanyanyaswa njooni huku aliko mzee wetu, hamuoni anavyoishi vizuri siku hizi?" Furahi ya kundi hili ni kuona ccm inavurugana iwe kwa kupewa JPM uenyekiti ama kwa njia yoyote ile....

Kwa vigezo vyovyote vile vya utawala na uongozi, Rais John Magufuli "anatawala" zaidi kuliko kuongoza, Kokote kule duniani, siasa huongozwa sio hutawaliwa, Hatuna historia ya Uongozi wa aina yoyote wa kisiasa wa John Pombe Magufuli,

Lakini kwenye kutawala tumemuona akihudumu katika Wizara na katika Urais sasa kwa miezi kadhaa, anatawala kwakutilia mkazo zaidi maamuzi yake katika nyanja zote za maisha ya Watanzania kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Hili linafanya kwa wadadisi wa siasa na uongozi aonekane kuwa kero kwenye mizani ya kisiasa na kidemokrasia, sio kwa wapinzani tu bali kwa taifa kwa ujumla, huenda ni ugeni wake katika uongozi ama ni aina yake ya kupendelea kutawala kuliko kuongoza.

Tofauti ya mtawala na kiongozi nikuwa, Kiongozi huongoza kwa kusikiliza anaowaongoza zaidi, na mtawala hutawala yale ayaaminiyo yeye kuwa ni sahihi, yaani zidumu fikra za mkubwa....

Pamoja na takwa la kikatiba nikuwa Rais akabidhiwe uenyekiti, Bado mkutano mkuu unaoketi kesho unayo fursa ya kutengua matakwa hayo ya kikatiba kwa maslahi ya chama na taifa.

Kwamaoni yangu ccm isimpe uenyekiti Magufuli angalau kwa miaka miwili mbele kuelekea 2020.
Ni busara kukaa kimya kama huna cha kuandika.
 
Yeriko ziko bilioni 3 za lowassa zimekupita naona siku hizi unabeep mtandaoni tu. Ccm siyo VVU kaka kaeni mtulie neema yaja. Nyie chama mmeshamkabidhi shetani kwa sababu mlisema safari ya ikulu hata shetani akiwapeleka ruksa
 
lini ukaipenda ccm wewe Yericko? yaani wewe wakuishauri CCM? leo unatoa ushauri eti ccm isimpe magufili KITI? aliekutuma mwambie pole ccm ni ile ile, Magufuli saivi anapanga safu yake maridadi kabisa ili azidi kuwapoteza mazima mmbaki tu mitandaon, bora wewe umejiongeza saivi unauza vitabu
Kutoa maoni kuna kizuizi?
 
Yericko nani atakuelewa na undumila kuwili wako na kujitoa ufahamu kwako? Mwaka jana uliendesha kampeni ya 'zuia jambazi kwenda ikulu' leo hii jambazi ndiyo muungu wako na unaliita 'mheshimiwa...'. Waacheni CCM wafanye yao, mwaka jana mlisema CCM inaenda kufia Dodoma, haikuwa hivyo, leo tena kelele ni zilezile. Kuweni na busara na fanyeni yenu, isitoshe CCM ikisambaratika ndiyo furaha kwa Vyama Vya Upinzani (VVU), hivyo mpigieni debe Magufuli awe Mwenyekiti ili akiue chama mpate wepesi.
VVU ni Virusi Vinavyosababisha Ukimwi hiyo ishapita siku nyingi tafuta ufupisho mwingine ili kutowachanganya wasomaji
 
Story za vijiweni hizi...

Chama kilichoshinda uchaguzi mkuu just recently, tena kwa mara ya tano mfululizo, kukiita kinapita kwenye wakati mgumu ni kujitoa akili...
Inapendeza ukisema "kilichotangazwa"
Kushinda
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom