helo team tusiokuwa na viburudisho ! hebu kujeni hapa tupige story leo wkend kama unaona haikuhusu naomba upotezee!
najua wengi wetu tuna makovu kwenye miili yetu madogo kwa makubwa! wengine waliungua udogoni..wengine wamepigwa mapanga kwa ujambazi wengine mafumanizi nk!
leo naomba tupige story kila mtu amwage kisa cha kovu lake hapa
mimi ninalo kwenye bega sema kwa ajili ya unene huu na kukua naona limeishia ishia limebaki kwa mbaali sana ila linanikumbusha mbali sana
story yangu ilikuwa hivi
nikiwa mdogo kuna siku mama yangu akanituma buchani nyama nusu kilo! akanipa elfu kumi ndo zimetoka toka nadhani nilikuwa sijawai kuiona tena! sio hii ya sasa hivi ....nusu kilo ya nyama nadhani ilikuwa elfu au mia tano hivi.
sasa kule buchani yule muuza bucha akanipa nyama na chenji wakati mimi nilikuwa sijampa hata hela huyooo nikaishia zangu... so ile elfu kumi ya mama ikawa yangu mi nikampa mama chenji yake .
kuna ndugu yangu tumefatana ila kanizidi miaka 4 nikamueleza jinsi nilivopata hilo zali asubuhi asubuhi hao tukaenda kufunga mtaa kwa pipi gololi na biscuit za bibi!ila kumbe mwenzangu roho ilimuuma ..so ikatokea sasa mama akitaka kumtuma mtu buchani anagombania sana na mimi sikubali ikawa ni vita vita! siku moja katika kupigana na akanibamiza ukutani ule ukuta una chuping sijui mafundi wanaita wenyewe ukanichumbua ndo source ya kovu langu!