Makosa ya wazi ya CHADEMA!

Makosa ya wazi ya CHADEMA!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Sasa ni dhahiri kuwa CHADEMA ni chama kikuu cha upinzani nchini na tishio kwa CCM yetu kama chama tawala Tanzania tangu uhuru. Sasa pia,watanzania wanabadilika kwa kasi mno. Wanajiandaa kubadili siasa za Tanzania hapo 2014 na 2015 katika Chaguzi za Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu. Wananchi wa Tanzania wanajiandaa kuwachagua watu na si vyama. Watachagua wachapakazi na si waharibu demokrasia na maamuzi ya wananchi.Wananchi wako tayari.

Sasa siasa za CHADEMA na CCM ni zile za halali mtu hadi kukuche.Hatua njema sana. Hatua vutizi za kidemokrasia.Yanayotokea Bungeni pia ni kiashiria cha mabadiliko ya kifikra na kimapambano hasa ya kisiasa. Jambo jema linaweza kushadidiwa hata na vijimambo vibayavibaya. Kikubwa ni kuwa demokrasia,kama jambo kubwa na jema, inaimarika. Na wale wanaojaribu kuzuia makuzi ya demokrasia nchini,watakiona cha mtema kuni!

CHADEMA,katika harakati zake za kujitangaza na kujiaminisha kwa watanzania,wanafanya kosa moja kubwa. Wanajiegemeza hasa kwenye mikoa michache nchini. Mikoa mingine inatengwa.Inatembelewa kwa nadra sana. Mikoa inayosahaulika itatumiwa na chama chetu cha CCM isivyo halali kwenye chaguzi. Itatangazwa kuwa CCM imeshinda kwa mbali katika mikoa husika. Hatari kidemokrasia!

CHADEMA wangejielekeza katika hasa mikoa ambayo hata hawana Mbunge hata mmoja. Mikoa kama Mtwara,Pwani,Lindi,Kusini Magharibi,Kaskazini Magharibi na mingineyo ya aina hiyo yaweza kukodolewa macho zaidi. Hakuna haja kila mara kupitia (namaanisha viongozi waandamizi wa chama na makada mahiri) katika mikoa ambayo tayari wameijua na kuikubali CHADEMA. Mikoa hiyo ni kama Mbeya,Arusha,Kilimanjaro,Mara,Manyara,Iringa,Mwanza na Shinyanga,

CHADEMA iliwahi kufanya Operesheni Sangara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa. Operesheni hii ikatoa matunda matamu sana kwa CHADEMA. Kanda ya Ziwa ndiyo inayoongoza kutoa Wabunge wengi kwa CHADEMA. Kwanini Operesheni kama hii isifanywe kwingineko? Kanda za kichama hazitoshi. Lazima zaidi kifanyike. Demokrasia ikiimarika,watanzania tutachagua watu bora zaidi.Tutaendelea. CHADEMA fanyeni jambo.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Ni kweli mzee Tupatupa, mi nashauri waanze haraka,tena sio mijini tu,wajikite vijijini ambako ccm inatumia ujinga wa wananchi kuwahadaa na viberiti,chumvi na tshirts...watanzania sasa ni wepesi wa kung'amua vitu na kufanyia kazi
 
Mtwara hivi sasa hakuingiliki mpaka martial law ifutwe.
 
Ni kweli Mkuu Jasusi. Lakini iko mikoa haina martial law
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli mkuu, chadema wajitaidi wajiimarishe mikoa kama ruvuma, morogoro, iringa, rukwa na hata dodoma. Pia wasisahau mikoa ya tanga,pwani na mtwara, bila kupita huko ccm itashindia hukohuko!
 
Ingawa naunga mkono hoja hii kwa sehemu fulani lakini naelewa vema kuwa lazima uwe strategic planner (malengo ya kimkakati) kwenye maisha na/au siasa. Hiyo mikoa ambayo Bw. VnV aliyotaja haijatengwa wala/au kupuuzwa la! Ila ukweli ni kuwa kupanga ni kuchagua. Kwenye mchezo wa namba (hesabu) lazima ujue utaanzia wapi na pia utamalizia wapi. Pia ni lazima uende kwa malengo na utaratibu mahsusi na hilo ndilo CHADEMA wanalofanya hapo.

Kuna mifano mingi, mmoja ni mfano huu: Mahitaji makuu ya msingi ya binadamu yanatajwa kuwa ni chakula, mavazi na malazi. Swali, je! mtu asiye na chakula & mavazi hivi atapambana kujenga nyumba kwanza au atajipanga amudu kupata chakula kisha mavazi kwanza huku lengo la kupata nyumba likisubiri nalo kufikiwa?
 
Mzee Tupatupa umenena kweli na ninakuunga mkono kabisa..mm natokea shinyanga..ni moja ya mikoa ambayo chadema imejiimarisha sana hasa hasa maeneo ya mjini lakini bado chadema wakitaka kuja wanakuja shinyanga mjini tu eneo ambalo kwa sasa hata liwekwe gogo kwa upande wa chadema kitashinda..
wanasahau kujiimarisha vijijini wanakuwa wanaishia mijini tuki kitu ambacho kinaweza kuwagarimu kwenye chaguzi zijazo maeneo ya vijijini..simaanishi kuwa chadema haipo vjjn no ipo tena sana ila tatizo linakuja watu hawa wanakuwa wanaipenda chadema kwa sababu tu wamechoshwa na maisha magumu wanayokumbana nayo ila si kwa influence ya viongozi wa chama..Hii inasababisha baadhi ya watu waliopo vijijini wakati mwingine kukata tamaa na mageuzi kwa sababu ya kukosa msukumo wa viongozi wa chama mwisho kuamiua kukipigia kura ccm.
tatizo jingine ni hilo la viongozi wakuu wa chama kuzuru mikoa kama mbeya tu na kuacha mikoa ambayo

hawajajiimarisha zaidi. hii inasababisha chama kutokukaa mioyoni mwa watu wa mikoa hiyo na mwisho wa siku inakuwa ni rahis kwao kurudi kwenye ccm...bt all in all ni ushaur mzuri ambao viongozi hasa hasa wa ngazi za juu za chama inatakiwa waufanyie kazi
 
Japo siku ni chache ila CHADEMA wanasonga kwa kasi sana, mie ninapiga kampeni kwa nguvu zangu zote kondoa CCM
 
Sasa ni dhahiri kuwa CHADEMA ni chama kikuu cha upinzani nchini na tishio kwa CCM yetu kama chama tawala Tanzania tangu uhuru. Sasa pia,watanzania wanabadilika kwa kasi mno. Wanajiandaa kubadili siasa za Tanzania hapo 2014 na 2015 katika Chaguzi za Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu. Wananchi wa Tanzania wanajiandaa kuwachagua watu na si vyama. Watachagua wachapakazi na si waharibu demokrasia na maamuzi ya wananchi.Wananchi wako tayari.

Sasa siasa za CHADEMA na CCM ni zile za halali mtu hadi kukuche.Hatua njema sana. Hatua vutizi za kidemokrasia.Yanayotokea Bungeni pia ni kiashiria cha mabadiliko ya kifikra na kimapambano hasa ya kisiasa. Jambo jema linaweza kushadidiwa hata na vijimambo vibayavibaya. Kikubwa ni kuwa demokrasia,kama jambo kubwa na jema, inaimarika. Na wale wanaojaribu kuzuia makuzi ya demokrasia nchini,watakiona cha mtema kuni!

CHADEMA,katika harakati zake za kujitangaza na kujiaminisha kwa watanzania,wanafanya kosa moja kubwa. Wanajiegemeza hasa kwenye mikoa michache nchini. Mikoa mingine inatengwa.Inatembelewa kwa nadra sana. Mikoa inayosahaulika itatumiwa na chama chetu cha CCM isivyo halali kwenye chaguzi. Itatangazwa kuwa CCM imeshinda kwa mbali katika mikoa husika. Hatari kidemokrasia!

CHADEMA wangejielekeza katika hasa mikoa ambayo hata hawana Mbunge hata mmoja. Mikoa kama Mtwara,Pwani,Lindi,Kusini Magharibi,Kaskazini Magharibi na mingineyo ya aina hiyo yaweza kukodolewa macho zaidi. Hakuna haja kila mara kupitia (namaanisha viongozi waandamizi wa chama na makada mahiri) katika mikoa ambayo tayari wameijua na kuikubali CHADEMA. Mikoa hiyo ni kama Mbeya,Arusha,Kilimanjaro,Mara,Manyara,Iringa,Mwanza na Shinyanga,

CHADEMA iliwahi kufanya Operesheni Sangara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa. Operesheni hii ikatoa matunda matamu sana kwa CHADEMA. Kanda ya Ziwa ndiyo inayoongoza kutoa Wabunge wengi kwa CHADEMA. Kwanini Operesheni kama hii isifanywe kwingineko? Kanda za kichama hazitoshi. Lazima zaidi kifanyike. Demokrasia ikiimarika,watanzania tutachagua watu bora zaidi.Tutaendelea. CHADEMA fanyeni jambo.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Nakukubali sana wewe Vutankuvute am sure Chadema watakusikia na watafanya kazi .
 
Tatizo kubwa ninaloliona kwa chadema ni kupishana kimtazamo na wananchi. Chadema kwa upande mmoja wanataka wananchi wachukue hatua dhidi ya kero zinazowakabili (peoples power) wananchi kwa upande wao wanataka chama au serikali inayotatua kero zao. Bila kutimiza matamanio ya wananchi chadema yaweza kupoteza hata majimbo inayoyashikilia kwa sasa. Kuna siku nilishaandika juu ya kero zinazosababisha wananchi wa kawaida waisijihusishe na chadema jijini dar es salaam. Kwa ufupi, hizi ni barua za serikali za mitaa kutoka wenyeviti wa mitaa ambao ni ccm. Kwa vile mwenyekiti hawezi kuwajua wananchi wote anamuuliza mjumbe. Huyo mjumbe ni balozi wa ccm. Balozi akiku-lebel we chadema basi ujue utakoma utakapo hitaji huduma yake. Kwa hali hii wananchi wa kawaida wanapoteza ari kwa chadema maana kuwa chadema kwao ni kukosa huduma za serikali za mitaa. Kwa hiyo ni jukumu la chadema kuoanisha kauli mbiu yao na matazamio ya wananchi.
 
Unafiki wangu upi Mkuu? Wengine ni akina nani hasa?

NI kweli lakini mbona wameshafanya operation nyingi mikoa ya Lindi na Mtwara na baada ya hapo ndipo likaibuka saga la gas mkuu? Na walipotaka kwenda tena wakakataliwa kwa minajili ya hali ya usalama siyo nzuri. Unakumbuka?
 
Mh vuta umetoa ushauri mzuri sana kwa cdm. ambao hata ccm na vyama vingine wanaweza kuutumia.

Mimi ningependa kuongezea ushauri huu kwa kunukuu mstari wa biblia unaosema,"shika sana ulicho nacho asije muovu akakunyang'anya."
 
Mzee Tupatupa umenena kweli na ninakuunga mkono kabisa..mm natokea shinyanga..ni moja ya mikoa ambayo chadema imejiimarisha sana hasa hasa maeneo ya mjini lakini bado chadema wakitaka kuja wanakuja shinyanga mjini tu eneo ambalo kwa sasa hata liwekwe gogo kwa upande wa chadema kitashinda..
wanasahau kujiimarisha vijijini wanakuwa wanaishia mijini tuki kitu ambacho kinaweza kuwagarimu kwenye chaguzi zijazo maeneo ya vijijini..simaanishi kuwa chadema haipo vjjn no ipo tena sana ila tatizo linakuja watu hawa wanakuwa wanaipenda chadema kwa sababu tu wamechoshwa na maisha magumu wanayokumbana nayo ila si kwa influence ya viongozi wa chama..Hii inasababisha baadhi ya watu waliopo vijijini wakati mwingine kukata tamaa na mageuzi kwa sababu ya kukosa msukumo wa viongozi wa chama mwisho kuamiua kukipigia kura ccm.
tatizo jingine ni hilo la viongozi wakuu wa chama kuzuru mikoa kama mbeya tu na kuacha mikoa ambayo

hawajajiimarisha zaidi. hii inasababisha chama kutokukaa mioyoni mwa watu wa mikoa hiyo na mwisho wa siku inakuwa ni rahis kwao kurudi kwenye ccm...bt all in all ni ushaur mzuri ambao viongozi hasa hasa wa ngazi za juu za chama inatakiwa waufanyie kazi
Ukweli ni kuwa hadi sasa CHADEMA kipo katika kiwango cha Kanda, hawajafika katika kiwango cha kufikia kila jimbo ili hatimaye waende kila kata na baadaye kijiji na kitongoji. Nadharia za kufanya hivyo zipo, lakini utekelezaji wake ni slow. Nimesoma leo katika moja ya nyuzi humu JF kuwa Mbowe ameanza kwenda kata kwa kata, kijiji kwa kijiji na anakusudia kwenda hadi kitongoji kwa kitongoji na hatimaye kila kaya! Huyu ni Mbowe, mwenyekiti. Anafanya jambo jema kwa jimbo lake ingawa ilikuwa inatakiwa kuwa iwe hivyo katika kila jimbo la uchaguzi hasa kule ambako CDM hawana wabunge!. Chadema wasipofanya hivyo sasa, matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwakani unaweza kuwapa matokeo ya kuwakatisha tamaa!!
 
Ki ukweli namuunga mkono tupa tupa, nami huwa sielewi kwa nini zoezi la kwenda vijijini ndani linashindikana, japokuwa kanda ya ziwa kuna mtu anaitwa Mawazo ambaye kiukweli anajitahidi kwa kufanya kazi ya ziada kuzunguka vijijini. Sielewi hata M4C imeishia wapi maake ni mikoa kama michache sana imefanyika kama sikuachwa nyuma na habari. Kweli CDM fanyeni kazi kwa kumaanisha, mkianza mission hakikisheni mnaikamilisha msikubali kucheza ngoma ya Magamba.
 
Ni kweli mzee Tupatupa, mi nashauri waanze haraka,tena sio mijini tu,wajikite vijijini ambako ccm inatumia ujinga wa wananchi kuwahadaa na viberiti,chumvi na tshirts...watanzania sasa ni wepesi wa kung'amua vitu na kufanyia kazi

Nilishasahuri jambo hili, lakini naona wenzetu makao makuu wamejikita mjini tu. Kwa muda uliobaki wangeelekeza nguvu vijijini mambo yangekuwa magumu zaidi kwa ccm.
 
Back
Top Bottom