mamaudaku
JF-Expert Member
- Nov 24, 2016
- 706
- 465
Hayo makontena hayawezi kuuzika endapo Muhusika ni Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa DSM.
Madalali wapo kwenye mkoa wake, matajiri na wanunuzi wapo mkoani kwake, Bandari ipo mkoani kwake. Na pia Inasadikiwa na inaaminika kuwa ni rafiki wa karibu wa mkuu wa nchi.
Mnada huo kwa vyovyote lazima udode mana mtuhumiwa ameshika makali na alishatoa onyo kuwa atakayethubutu kuyanunua atapata laana mbaya. Laana mbaya yaweza kuwa jambo lolote baya.
Vinginevyo waje wanunuzi toka Kenya lakini sio Dar es salaam.
Akitumbuliwa makonda hayo makonteina hayakai hata dk watu wanaogopa kutumiwa watu wasiojulikana