Makonda wote akili zao ni sawa?

Makonda wote akili zao ni sawa?

Wakuu,salamu ziwafikie...

Nimeamua kuja hapa jamvini ili niweze kuwapa tabia na uwezo wa kufikiri(akili ya kufikiri) kwa hawa ndg.zetu(makonda) kulingana na utafiti nilioufanya kwa muda wa miezi 7 katika majiji 5(Mwanza,Arusha,Mbeya,Tanga na kisha kumalizia na Dar es Salaam),manispaa 6 za miji(Morogoro,Moshi,Musoma,Dodoma,Iringa na Tabora)..

Kulingana na utafiti nilioufanya nimebaini/kugundua kuwa makonda wote sio wa Dar,Mbeya hata kule Musoma akili zao huongozwa na:-

1:Matukio kulingana na uendeshaji na mapenzi ya dereva.
kama derva akiendesha mwendo wa taratibu nao humshangilia dereva hata kama abiria wanalalamika kuchelewa kufika.Vivyo hivyo na kama dereva ataongeza mwendo zaidi na abiria kulalamikia mwendo pamoja na uhai wao,utasikia konda akipayuka"suka(dereva),kaza mguu zaidi tumechelewa pesa"

2:Ni wahamasishaji sana wa kutaka pesa za watu kabla ya safari kuanza au katikati ya safari lakini ni wagumu sana kutoa za kwao wakati wote(yeye na abilia)wamo ndani ya gari..cha kusikitisha zaidi wao(makondakta) huwa wagumu kwenye kurudisha "change" au kufidia abilia ajari zinapotokea.

3:Makonda wote sio wa Dar,Morogoro hata Dodoma ni watalaam sana wa matusi na kujifanya wababe wakati hamnazo.Huwa wakipita kuchangisha nauli,hutoa kauli tata,zenye maudhi,matusi hata pasipostahili kutusi.Nilijaribu kumuhoji kondakta mmoja,je huwa wanaenda kupata mafunzo ya matusi na kuigiza ni wababe wakati sio?majibu niliyapata ni kwamba"ukishajiingiza na kufanya kazi ya ukonda ndani ya chama cha makonda,ni lazima utafundwa na watangulizi wako(viongozi wa makondakta)"konda huyo alijibu.

Je,kwa utafiti wenu huko mliko,makonda wenu wakoje?

umetumia lugha ya kificho si ajabu hata makonder mwenyewe hatojua kama umemsengenya yeye. safi sana mtoa post
 
Kwani makonda ndo nani ? Mi niko dar maana nasikia sikia makonda hivi ni nani?
uko Dar sehemu gani mkuu?mbona makonda wapo kila daladala hapo Dar?mbezi-kimara-ubungo kuna makonda wengi,ubungo-mwenge-makumbusho wapo pia,mwenge-kawe-tegeta-bagamoyo pia wapo,ubungo-k/koo-posta utawapata,ubungo-buguruni-temeke hadi chanika mbona wapo,....mkuu labda we uko Dar ya magazetini..
 
Wakuu,salamu ziwafikie...

Nimeamua kuja hapa jamvini ili niweze kuwapa tabia na uwezo wa kufikiri(akili ya kufikiri) kwa hawa ndg.zetu(makonda) kulingana na utafiti nilioufanya kwa muda wa miezi 7 katika majiji 5(Mwanza,Arusha,Mbeya,Tanga na kisha kumalizia na Dar es Salaam),manispaa 6 za miji(Morogoro,Moshi,Musoma,Dodoma,Iringa na Tabora)..

Kulingana na utafiti nilioufanya nimebaini/kugundua kuwa makonda wote sio wa Dar,Mbeya hata kule Musoma akili zao huongozwa na:-

1:Matukio kulingana na uendeshaji na mapenzi ya dereva.
kama derva akiendesha mwendo wa taratibu nao humshangilia dereva hata kama abiria wanalalamika kuchelewa kufika.Vivyo hivyo na kama dereva ataongeza mwendo zaidi na abiria kulalamikia mwendo pamoja na uhai wao,utasikia konda akipayuka"suka(dereva),kaza mguu zaidi tumechelewa pesa"

2:Ni wahamasishaji sana wa kutaka pesa za watu kabla ya safari kuanza au katikati ya safari lakini ni wagumu sana kutoa za kwao wakati wote(yeye na abilia)wamo ndani ya gari..cha kusikitisha zaidi wao(makondakta) huwa wagumu kwenye kurudisha "change" au kufidia abilia ajari zinapotokea.

3:Makonda wote sio wa Dar,Morogoro hata Dodoma ni watalaam sana wa matusi na kujifanya wababe wakati hamnazo.Huwa wakipita kuchangisha nauli,hutoa kauli tata,zenye maudhi,matusi hata pasipostahili kutusi.Nilijaribu kumuhoji kondakta mmoja,je huwa wanaenda kupata mafunzo ya matusi na kuigiza ni wababe wakati sio?majibu niliyapata ni kwamba"ukishajiingiza na kufanya kazi ya ukonda ndani ya chama cha makonda,ni lazima utafundwa na watangulizi wako(viongozi wa makondakta)"konda huyo alijibu.

Je,kwa utafiti wenu huko mliko,makonda wenu wakoje?
hata makaonda mkuu wa mkoa yuko kama hao??
 
Back
Top Bottom