Makonda usipoteze muda wako

Makonda usipoteze muda wako

Hoja yako ya wanandoa kuchepuka ukafungwa miaka thelasini ni mfu na ndoto

Wewe na bashite ni mazumbukuku, badala mboreshe huduma za kijamii mnahangaika na vikojoleo na mioyo isiyowahusu
 
Hoja yako ya wanandoa kuchepuka ukafungwa miaka thelasini ni mfu na ndoto

Wewe na bashite ni mazumbukuku, badala mboreshe huduma za kijamii mnahangaika na vikojoleo na mioyo isiyowahusu
😂😂 vikojoleo ndo nyapu au!
 
3. Mgawanyo wa Shule.
Pawepo na shule za Wasichana na shule za Wanaume pekee yao. Shule za wanawake wafundishe waalimu wa kike pekee. Halikadhalika na shule za wavulana wawepo waalimu wakiume tuu.
Miaka ya Shule za sekondari na shule ya msingi ipunguzwe angalau mwanafunzi amalize kidato cha sita akiwa na miaka kumi na sita

Chuoni pawe na mchanganyiko chini ya uangalizi mkali. Chuoni pawe ndio sehemu ya vijana kutafuta wachumba chini ya uangalizi wa Mshauri wa Wanafunzi.
Hii inachangamoto nyingi lakini sababu za huko juu zitaifanya ifanye kazi hasa mtoto wa kike kutokuolewa endapo hatakuwa na bikra.
👆 hiyo umetoa maoni fake kabisa..!!
 
Makonda yupo sahihi kabisa muacheni afanye hiyo kazi kwanza kabisa ujue amesema atashirikisha wajumbe wa nchi zingine kuona kwamba wao wanafanyaje kushughulikia mambo kama hayo. Ukweli ni kwamba tanzania yetu bado ipo huru sana kufanya mambo ya kijinga hakuna mwanamke anayependa kutapeliwa pili ujue unamnyanyasa mtoto kwanini umpe mtu mimba halafu umtelekeze na mtoto kwanini usimchukue basi mtoto wako kama unaweza ukamtunze wewe? hebu angalia kama marekani ukizaa na mtu lazima utunze mtoto na usipofanya hivyo pesa zako zote zinakatwa na serikali then inaenda kwa mtoto. sasa tanzania yetu lazima serikali ianzishe utaratibu kama huo hasa kwa wale walioajiriwa serikalini na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NGO'S) . Kwa wale ambao hawakuajiriwa wamejiajiri basi serikali iangalie sheria yake mpya ya kuwabana hao.
1.kwa kufanya hivyo ongezeko la watoto mitaani litapungua.
2 Ndoa zitaheshimiwa na idadi ya ndoa zinazovunjika kila kukicha zitapungua kwani ndoa nyingi zinavunjika kwa sababu ya michepuko na watoto wa nje kuongezeka.
wanaume watakuwa waaminifu na pia watakuwa waoga wa kuchepuka kwa kuhofia mimba za nje.
3. Ugomvi wa mali baina ya watoto wa nje na wa ndani ya ndoa utakwisha kwa kupitia sheria hiyo mpya.
4.Ukimwi utaisha kama sio utapungua kwani michepuko imekuwa mingi hadi kuwaambukiza maradhi hata wasiokuwa na hatia
5. Kanisa litakuwa limepata msaada mkubwa kwani ndoa zitadumu hivyo wachungaji nao watapumzika kwa kusuluhisha migogoro ya ndoa kila siku.
6 Ukimpa mtu mimba hata kama usipomuoa lakini lazima utatunza hivyo mtoto hatateseka

Mwisho kabisa nakuomba Muheshimiwa makonda zingatia hili ukifanikiwa tu nitakutafuta nikupe zawadi yako manake hata mimi nimechoshwa kabisa na hizi tabia za watu wasiokuwa waaminifu usiogope wanaokubeza kwani watanzania wengi tumesahau majukumu yetu tumehamia wote kwenye michepuko kama vile ndio kazi iliyobaki. inawezekana maombi ya wanandoa yanakwenda kujibiwa sasa kwa kupitia wewe. Mungu akutangulie ufanikishe hili Makonda wangu
 
kwanza atazuiaje suala la Nyumba ndogo? Pili anajuaje kuwa wadanganyifu wa ndoa ni wanaume pekee? Tatu ni kwa namna gani hiyo database ya ndoa itawaondolea wachumba watarajiwa kutapeliwa? Maana mtu anaweza asiwemo kwenye hiyo kanzi data lakini bado akamliza mchumba wake!
 
Duhhh...Taikon waFasihi hapo aisee......duhh sijawahi kuhisi wewe ni mnoko kiasi hiki....unataka hii nchi iwe kama tupo peponi .

Umeongea vizuri sana ila ushauri wako.....samahani... kwangu mimi nauona wakidikteta sana.


Kuhusu bikira kwa mwanamke inaweza kutoka ata kwa michezo ya kawaida tu na sio kwa zinaa, na sijui kama itasaidia kwa kusema tu...mimi sijawahi kufanya mapenzi, ukaridhika kuwa yupo bikira..na kama utaruhusu utetezi huo basi wale ambao hawana wote wataegemea huko.

Sifikirii pia kama mwanamke atasema hajawahi kufanya mapenzi lakini bikira haipo serikali ianze kupima kama hiyo sehemu ya uke imewahi kupitiwa na mzigo flani hivi....tukifika huko itakuwa ni udhalilishaji......

Mi nasema hivi hiyo kanzu data iwepo kwa wote kama leo hii tunaweza kumuona wakili aliyeruhusiwa kufanya kazi hiyo ndani ya sekunde tu...itakuwa vizuri pia kwa wanandoa ukitaka kujua "Muda wa Ukombozi" kaoa na kamuoa nani majina yatokee na picha zetu namaanisha mimi na mke wangu, halikadhalika iwe hivyo na kwa wanawake pia tukiwapekua tuone hadhi zao pia.

Halafu wakati mwingine mapenzi ni neno ukilinyambua vizuri utakuta kuna upendo ndani yake, na nguvu yake ni kubwa, ukitaka kuleta ubaguzi hapa, mwanamke ukimuhitaji kidogo mara andika barua, mara fuata taratibu wanawake wengi watabaki manungaembe.

Mi naona utaratibu huu uendelee ila mh. Makonda achukue ushauri wangu hapo, hii itatusaidia sisi wanaume, kama ni muislamu kuna ruhusa ya kuoa wake wanne, kwahiyo mwanamke atajua anapambana yeye atakuwa wangapi, kama ni mkiristo na utaratibu wa dini ni kuwa na mwanamke mmoja ni kuangalia jinsi gani unaweza kuongeza kimila.......

Mila zetu za Kitanzania ata afrika sijawahi ona kuna ukomo wa kuoa kwahiyo kama umeoa na bado umependa mwingine tena, hakuna namna unaoa kimila maisha yataendelea.

Ahsante sana...nimefurahishwa na huu uzi..uangu ni hayo machache.
 
sasa ndio umeandika nini...? ebu muacheni makonda afanye kazi kwenye mkoa wake...
 
WANAWAKE HUENDEKEZA KUTAPELIWA.

Na, Robert Heriel.

Mtu anayefuata sheria na utaratibu kamwe hawezi kutapeliwa. Hasa sheria na amri za Mungu. Anayefuata mila na desturi kamwe hawezi kutapeliwa. Ukisikia mtu katapeliwa basi jua kuna sehemu amevunja sheria za dini au mila na desturi.

Moja ya Sababu ya mtu kutapeliwa ni tamaa na kutofuata taratibu za jambo husika. Ni ile tabia ya uasi na kufanya mambi kisiri siri.

Suala la mapenzi lisiwe suala la siri kwa vijana waliofikisha umri wa kuoa au kuolewa. Unakuta mtu anamiaka 20+ anaogopa kumuita kijana anayemchumbia nyumbani kwao ili wazungumze nyumbani.

Binti anamficha Mama yake kuhusu mambo ya mahusiano yake. Bado asitapeliwe thubutu. Mambo ya kimya kimya ndio huzaa utapeli.

Wewe binti kama umefikia umri wa kuolewa na kijana amekufuata na unampenda. Unashindwa kumuuliza kuwa je hajui utaratibu. Kama hajui mwambie utaratibu ukoje. Mwambie aandike barua iende kwa wazazi. Kisha taratibu zingine zifuate. Aje kwenu nawe uende kwao. Kisha mtangaze ndoa kwa siku kadhaa kuona kama kuna pingamizi. kama hakuna fungeni ndoa.

Sasa jitu linafanya mambo kimya kimya kwa nini lisitapeliwe. Mtu hataki hata kukuweka Profile picture wewe unachekelea tuu kama mwehu. Mtu anataka ndoa ifungwe kimya kimya hushtuki tuu kuwa kuna wizi unaendelea. Unakuja kuolewa baada ya miezi kadhaa unashangaa mke mwenzako anakuja kukutoa. Ati unalia. Pumbavu wewe ni wa kuchapa bakora. Unadanganywa kama mwehu.

Alafu shida nyingine ni kuwa vitoto vya siku hizi inajifanya inajua kila kitu. Haitaki ushauri kwa wazazi na wakubwa zao. Ati wameenda shule. Shule gani kama sio upuuzi. Mwishowe inakuja kusumbua watu.

Vijana nao kazi ujinga. Unahonga pesa kama kichaa. Ati ninasomesha. Mara ninamhudumia. Unamhudumia ni mke wako huyo. Akikuacha unaona watu wabaya wakati wewe ndio akili yako ni saa mbovu. Kutapeliwa ni kukiuka sheria za msingi. Mke ndio huhudumiwa hao wengine fukuza huko.

Mhe. Makonda hao unaowatetea kuwa wanatapeliwa ndio wanaoendekeza huo utapeli. Wao ndio wanataka watapeliwe. Ukiona mtu katapeliwa ujue yeye ndio chanzo cha huo utapeli.

Najua inakuumiza kuona Dada zetu wakilaghaiwa hali inayopelekea kupewa mimba na kutelekezwa. Hali inayopelekea Kuwatumikia wanaume kinyumba kwa miaka kadhaa alafu mwishowe hufukuzwa kama Paka shume. Ni kweli inauma lakini nakuhakikishia kuwa Chanzo kikubwa cha wao kulaghaiwa ni wao wenyewe kutaka.

Mwanamke aliyefunzwa akafunzika kamwe hawezi kulaghaiwa na mwanaume. Hawezi shindwa kujua yupi ni mwanaume mkweli na yupi ni mwanaume Muongo.

Mwanamke akitapeliwa ni wazi amejishusha viwango vya kuwa Mke mwema ndani ya nyumba. Ni wazi hatakuwa Mama Bora ingawa anaweza jifunza kutokana na makosa lakini ni wachache wanaojifunza kutokana na makosa.

Mhe. Makonda unaposema ndoa zisajiliwe sijajua unazungumzia nini. Mimi ninachojua ni kuwa ndoa ni lazima iwe imesajiliwa. Iwe ni ndoa ya kidini, Kimila au Ndoa ya serikali. Bahati nzuri ni kuwa mwenye mamlaka ya kusajili ndoa ni Serikali na ndio inayotoa vyeti. Sasa hizo ndoa unazosema zisajiliwe ni zipi.

Kama ni zile ndoa za kihuni za njoo tuishi pamoja hizo sio ndoa. Hizo ndizo huleta athari mbaya na hata kufikia watu kufanyiana utapeli.

Mhe. Makonda tamko lako lingetakiwa kusema Wale ambao hawajagunga ndoa ya aina yoyote lakini wanaishi pamoja waende mahala husika wakajisajili. Na ungependekeza bunge liunde sheria ya kuwa ni marufuku kwa mwanaume na mwanamke wasio na undugu kuishi pamoja bila kufunga ndoa. Kisha iwekwe adhabu kali kwa watakao kiuka.

Sheria hii ingekuwa na manufaa mengi. lakini faida kubwa ni kuwa na taifa lenye maadili ya kibinadamu na sio taifa la watu wanaoishi kama wanyama ambalo mtu akitaka kuishi na mwanamke/mwanaume anaishi tu bila wasi wasi. Hiyo ni desturi ya Wanyama.

Pia sheria hii itaongeza mapato ya taifa kwani Wanandoa watatoa pesa ya Vyeti au namna yoyote ile ya usajili.

Mhe. Makonda nature ipo wazi kabisa kuwa Mwanaume ndiye mtawala na ndiye muwindaji. Wakati mwanamke ni mtawaliwa na muwindwaji. Hao wanawake unaowatetea kuwa wanatapeliwa ni kutokana na kukiuka nature. Wanawake wanapaswa kutozurura zurura hovyo. Lakini wanawake wa siku hizi kutwa kiguu na njia tadhani wao ni wawindaji. Kutwa kwenye kumbi za starehe ilhali wao ni wawindwaji.

Wanawake wanapaswa kukaa ndani na kama watatoka iwe ni kwa sababu maalumu hasa hasa kazini. Lakini wanawake wa siku hizi ni kama wanaume kutwa kuzurura na hapo ndipo hukutana na wanaume mafisi na simba wala nyama. Jambo hili litokea ndipo kizaa zaa huzuka. Hata Hawa/Eva alianguka kwa Kuzurura hovyo bila mpango. Alisahau yeye ni muwindwaji.

Mhe. Makonda hao wanawake wa siku hizi wanaotapeliwa wanataka wenyewe kutapeliwa. Unakuta limwanamke halifanyi kazi. Livivu kutwa kuomba omba pesa kama omba omba asiye na miguu wala mikono. Wenyewe siku hizi wanaita kudanga. Hivi Mkuu Makonda kwa akili yako Mvuvi anapoweka Chambo kwenye ndoano unafikiri anadhumuni gani. Mvuvi anajua kuwa wapo samaki wenye uroho watabwia chambo kwa ulafi wao.

Wapo wanawake wengi siku hizi wenye uroho wa pesa. Na wanaume kama wawindaji kwa kujua jambo hili huweka pesa kama chambo kusubiri Wanawake wenye uroho. Hapo ndipo utapeli hutokea.

Ningefurahi kama ungepiga marufuku kwa wanaume wote kutoa pesa au mali yoyote kwa wanawake ikiwa sio wake zao au ndugu zao. Hapa ungecheza kama Ronaldo. Lakini unazuia upande mmoja alafu upande mwingine unaachia. Hata hivyo mambo haya ni mambo binafsi lakini kama umeamua kuyaingilia ni sawa. Usizuie upande mmoja zuia pande zote.

Mhe. Makonda najua huna lengo la Kupambana na jambo hili. Na kama unalengo basi nakusihi fuata ushauri wangu kama ifuatavyo;

1. ZUIA HAKUNA MWANAMKE KUOLEWA BILA BIKRA.
Zamani hapakuwa na utapeliwa kwani kulikuwa na sheria kali. Mwanamke alipaswa kujitunza na wazazi wa mwanamke walihakikisha aibu haiwapati. Walimtunza binti yao.

Ikiwa utatoa tamko kuwa mwanamke asiolewe bila bikra. Nakuhakikishia hutasikia habari za utapeli wa mapenzi. Hutasikia habari za wanawake wanaozaa kabla ya ndoa ambalo kwa sasa ni janga kubwa sana.

Hutasikia habari za Wanaume wenye vibamia. Hutasikia habari za Baba wa Kambo au mama wa kambo. Hutasikia mambo ya Ex wangu. Hutasikia hayo nakuhakikishia.

Bunge liunde sheria hiyo kama taifa linataka liwe sirius na masuala haya. Vinginevyo unapoteza muda wako.

Katika hili Natarajia changamoto kubwa kutoka kwa Wanawake wengi ambao wameshatoa bikra zao. Hilo lisiwe sababu hao wataolewa na wazee ambao wake zao wamefariki.

2. Dhibiti nyumba za Wageni na Nyumba za kupangisha.
Mwanamke na mwanaume wasiingie nyumba ya wageni ikiwa hawana vitambulisho vya ndoa. Hii itazuia zinaa na uasherati. Mmiliki wa Guest kama atakiuka sheria hii basi atafutiwa kibali cha kuendesha biashara hiyo

ingawa itafanya biashara ya Nyumba za wageni kuwa ngumu lakini itajenga maadili ya taifa.

Halikadhalika na upande wa Nyumba za kupangisha. Asipange mwanamke na mwanaume kwa pamoja kama sio wanandoa na kama hawana vitambulisho vya ndoa.

3. Mgawanyo wa Shule.
Pawepo na shule za Wasichana na shule za Wanaume pekee yao. Shule za wanawake wafundishe waalimu wa kike pekee. Halikadhalika na shule za wavulana wawepo waalimu wakiume tuu.
Miaka ya Shule za sekondari na shule ya msingi ipunguzwe angalau mwanafunzi amalize kidato cha sita akiwa na miaka kumi na sita

Chuoni pawe na mchanganyiko chini ya uangalizi mkali. Chuoni pawe ndio sehemu ya vijana kutafuta wachumba chini ya uangalizi wa Mshauri wa Wanafunzi.
Hii inachangamoto nyingi lakini sababu za huko juu zitaifanya ifanye kazi hasa mtoto wa kike kutokuolewa endapo hatakuwa na bikra.

4. Sheria na adhabu kali kwa Watakaokiuka.
Serikali iunde sheria kali kwa watakaokiuka amri hizo. Iwe ni mwanamke au mwanaume.

Kama binti atakutwa na kijana wakifanya mapenzi wapewe adhabu kali ikiwezekana kufungwa kifungo kisichopungua miezi sita kwa mwanamke. Na kisichopungua mwaka mmoja kwa mwanaume.

Miezi sita kwa mwanamke kwa kuwa yeye atakuwa kapoteza bikra na hataolewa na vijana bali wazee. Zaidi ya mwaka mmoja kwa Mwanaume kwa kuwa yeye hana alichopoteza na ataoa mwanamke amtakaye

5. Kifungo cha miaka thelasini kwa Mtu atakayechepuka ndani ya ndoa.
Hii iwe kama kwenye kesi ya ubakaji. Mwanaume au mwanamke atakayechepuka ndani ya ndoa afungwe miaka thelasini.

Uone kama taifa halitanyooka hili. Ukiona uovu unaenea kwa kasi ujue Watawala ni mawakala wa Shetani. Hivyo ndivyo ilivyo.

Ni hayo tuu kwa Leo.

Robert Heriel
Taikon Wa Fasihi
0693322300
Hongera kwa mawazo yako Chanya.....
Napenda na kuvutiwa na utangulizi ulioanza ila ukaja kuharibu kwenye Namba.

Kuanzia 1 mpaka ya mwisho hakuna uhalisia...mfano mdogo tu kwamba pamoja na sheria kalo ya ubakaji yenye adhabu kali lakini Bado watu wanabaka, na wengine pengine hawafungwi, aidha kwa sababu mbalimbali.

Umtajaye hatoweza kubalidi sheria wala yeye hahusiki moja kwa moja katika kuzitunga wala kuanzisha muswada wa sheria.

Hiyo namba 1 tu inakufanya ujikute umewatengenezea watu biashara ya kupata pesa SABABU WATAANZA KUUZA UNGA WA DAWA ZA KURUDISHA BIKRA tena kwa kunadi kama zinavonadiwa za NGUVU ZA kiume mara vumbi la kongo, mundende, super nini sijui.....n.k

Nyumba za kulala wageni sio ndio UWANJA WA MKP pekee ambapo mechi za uzinzi zinachezwa ila maeneo ni mengi na madanguro na vyumba vya short time vya wamiliki halali kabisa wanaouza vinafahamika na vingine ni siri kubwa labda ukiwa mteja.

Hitimisho.
Hoja yako ya msingi binafsi na wanavuoni wengine na wasio wanavuoni watakuwa wamekuelewa "KUWA WANAWAKE WAO WENYEWE NDIO WANAOCHUKUA NAFASI KUBWA KATIKA KUFANYA WATAPELIWE"

Naomba ibaki hivo Sababu kama mwanamke ataweka KUOLEWA KAMA NI FIRST DEMAND BASI MWANAUME ATAKUWA HANA BUDI....

Naomba kuchangia na kuwasilisha
Asanteni
 
Kwani Baba Keagan kaja na mpya ipi?

Maana jamaa huwa anaweza toa matamko hata kumi ndani ya mwezi...
 
Huezi kuwalazimisha watu kuishi pamoja,mnaona kwa kuwa watanzania ni hewala hewala kila mnalosema sasa mnataka kutuingilia hadi vyumbani
 
Back
Top Bottom