kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,992
- 17,892
Natumai u bukheri wa siha njema mwanaJf mwenzangu...Nakusalimu kwa jina la jamhuri ya muungano wa Tanzania na jina la jamhuri ya kiislam ya Iran
Kwa muda wa miaka 40 sasa uwezo wa kijeshi wa Jamhuri ya kiislam ya Iran umewanyima usingizi na kuwatia kiwewe na jinamizi makhabithi wa kizayuni,madola ya kibeberu na vibaraka na matakthiri wa kieneo
Madola hayo ya kibeberu yenye kiburi yakiongozwa na utawala wa mjini Washington na London na lobi za wazayuni si tu zimekumbwa na wahka kuhusu statejia na uwezo mkubwa na irada ya wananchi wa Iran ya kiislam bali hata zimekua zikikhitilafiana namna ya kuingia katika satwa mpya au kujitumbukiza katika kinamasi cha vita na Iran ya kiislam
Madhali, utawala huo haramu wa israel kama kibaraka na mwana pendwa wa Washington na mshirika wa kisiri wa makhabithi wa kieneo umekua ukitoa dai eti kwamba wanaweza kuishambulia jamhuri ya kiislamu yenye nguvu na muqawama jambo ambalo utawala huo umekua ukiwa katika ngano hii ya ndoto kwa miaka takribani 40 sasa
Wazayuni hao waoga wanafahamu fika nguvu na irada ya muqawama wa wananchi wa iran na nguvu ya kimuqawama kuanzia iran,iraq,syria,lebanon na ghaza na kufahamu nguvu ya makombora ya jamhuri ya kiislam yenye uwezo wa kuusukumia utawala huo kharamu na katili katika bahari ya maangamizi
Kwa nukta hizi ni kwamba siku za utawala huu haramu zinahesabika huku madhalimu wengine wa kieneo na matakhiri siku zao za kusambaratika zikihesabika
Ala kulli..hali madhali muqawama unazidi kuongezeka basi wazayuni na mabeberu wajiandae kuonja joto la jiwe na kilichompata kanga manyoya siku za usoni
Nikiwambukushe tu ndugu wana Jf wenzangu kwamba mapinduzi ya kiislam sio tu yalizaa matunda ya irada, ruwaza ya uangavu kwa watia nia wote bali ilizaa mwamko mpya wa dunia dhidi ya kupingana na udhulumati,ukhabithi, kupigania haki duniani na kupambana na uistikibari wa madola ya kibeberu duniani pote
View attachment 1917928
View attachment 1917927
Kwa muda wa miaka 40 sasa uwezo wa kijeshi wa Jamhuri ya kiislam ya Iran umewanyima usingizi na kuwatia kiwewe na jinamizi makhabithi wa kizayuni,madola ya kibeberu na vibaraka na matakthiri wa kieneo
Madola hayo ya kibeberu yenye kiburi yakiongozwa na utawala wa mjini Washington na London na lobi za wazayuni si tu zimekumbwa na wahka kuhusu statejia na uwezo mkubwa na irada ya wananchi wa Iran ya kiislam bali hata zimekua zikikhitilafiana namna ya kuingia katika satwa mpya au kujitumbukiza katika kinamasi cha vita na Iran ya kiislam
Madhali, utawala huo haramu wa israel kama kibaraka na mwana pendwa wa Washington na mshirika wa kisiri wa makhabithi wa kieneo umekua ukitoa dai eti kwamba wanaweza kuishambulia jamhuri ya kiislamu yenye nguvu na muqawama jambo ambalo utawala huo umekua ukiwa katika ngano hii ya ndoto kwa miaka takribani 40 sasa
Wazayuni hao waoga wanafahamu fika nguvu na irada ya muqawama wa wananchi wa iran na nguvu ya kimuqawama kuanzia iran,iraq,syria,lebanon na ghaza na kufahamu nguvu ya makombora ya jamhuri ya kiislam yenye uwezo wa kuusukumia utawala huo kharamu na katili katika bahari ya maangamizi
Kwa nukta hizi ni kwamba siku za utawala huu haramu zinahesabika huku madhalimu wengine wa kieneo na matakhiri siku zao za kusambaratika zikihesabika
Ala kulli..hali madhali muqawama unazidi kuongezeka basi wazayuni na mabeberu wajiandae kuonja joto la jiwe na kilichompata kanga manyoya siku za usoni
Nikiwambukushe tu ndugu wana Jf wenzangu kwamba mapinduzi ya kiislam sio tu yalizaa matunda ya irada, ruwaza ya uangavu kwa watia nia wote bali ilizaa mwamko mpya wa dunia dhidi ya kupingana na udhulumati,ukhabithi, kupigania haki duniani na kupambana na uistikibari wa madola ya kibeberu duniani pote
View attachment 1917928