Wana JF,
Wote tunafahamukwamba tangu uhuru hakuna Spika wa Bunge Tanzania amezuiwa na chama kuingia kwenye kinyang'anyilo cha uchaguzi, wengine walikaa mpaka wakafa, hata mzee wetu Msekwa baada ya kutangaza kustaafu, na kulipwa maluplupu ikiwa pamoja na Benzi zito aliguka na kujitupa uwanjani ambako aliangushwa vibaya, lakini hukuzuiwa.
Affirmative kusaidia wanyonge kwenya jamii sawa, lakini kiti cha Spika si zawadi. Rejea mizengwe ilivyo kwenda. mzee wa vijisenti akasema yeye ni kiongozi safi anafaa kugombea, TAKURURU ikasema naaam, si wote tunamjua mkuu wa pale anakotoka, alikofanya kazi zama hizo na waliomweka alipo. Waingereza wakatia kitumbua mchanga, roho mbaya hawa, eti oh, mambo bado, mahakama uingereza hajatoa hukumu na kumfutia mashitaka Mzee wa vijisenti kama TAKURURU ilivyodai. Wajanja, soma mafisadi, wakasuka kikasukika, oh zamu wa wanawake, ebo, kwa nini Usipika, na siyo Katibu Mkuu wa Chama, Jaji Mkuu, Mkuu wa Polisi, Waziri Mkuu na hata rais!!!!!!!!!!!!1 Bwana Shibuda alipojotokeza kugombea uraisi kwa ticketi ya chama cha mapinduzi akaambia, bwana aliyeko Magogoni lazima amalize ngwe yake, na aliyeko mjengoni hana ngwe?
Jamani tusidanganywe huyu mama alibebwa si siri, kibaya zaidi ni kwamba alibebwa na wabaya wa Sitta, period.