king kan
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 1,642
- 2,081
Spika wa Bunge, Anne Makinda ametoa ushauri wa bure kwa wabunge wa Viti Maalumu na kusema kwamba, badala ya kuendelea kubweteka katika nafasi hizo, wajinasue sasa na kwenda kugombea majimboni kwani nafasi hizo zinawapotezea heshima mbele ya jamii.
Spika anasema wabunge wa Viti Maalumu wanaonekana kuringa na kujisahau kabisa kwenda majimboni, huku akionya kwamba kitendo cha kuendelea kubweteka kitakuwa kimewaangusha wanawake wa Tanzania, ambao alisema wanategemea ushiriki wao katika chombo hicho muhimu cha kufanya maamuzi. Kwa tafsiri yoyote ile, hayo ni maneno makali ambayo pengine yatakuwa yameudhi baadhi ya wabunge hao kwa madai ya kudhalilishwa.
Source; Mwananchi
Spika anasema wabunge wa Viti Maalumu wanaonekana kuringa na kujisahau kabisa kwenda majimboni, huku akionya kwamba kitendo cha kuendelea kubweteka kitakuwa kimewaangusha wanawake wa Tanzania, ambao alisema wanategemea ushiriki wao katika chombo hicho muhimu cha kufanya maamuzi. Kwa tafsiri yoyote ile, hayo ni maneno makali ambayo pengine yatakuwa yameudhi baadhi ya wabunge hao kwa madai ya kudhalilishwa.
Source; Mwananchi