Makerere University kumuenzi Mkapa kwa uongozi bora

Kapwani

JF-Expert Member
Nov 17, 2009
672
110
Chuo Kikuu Makerere kumuenzi Mkapa kama kiongozi bora
broken-heart.jpg
Na Leon Bahati

"NABII hakubaliki nyumbani kwake". Ndivyo inavyojionyesha kwa rais wa serikali ya awamu ya tatu, Benjamin Mkapa ambaye leo atakuwa akitunukiwa shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa na Chuo Kikuu cha Makerere.

Nyumbani, Mkapa anakabiliwa na tuhuma nzito za kufanya biashara akiwa Ikulu, kujiuzia mgodi wa Kiwira kwa bei poa akiwa na waziri wake wa zamani, Daniel Yona, lakini leo, rais huyo wa awamu ya tatu ambaye alifanya kazi kubwa ya kuinua uchumi, atatunukiwa shahada hiyo kutokana na chuo hicho kubaini kuwa alikuwa kiongozi bora na ambaye anafaa kuigwa.

Mkapa, ambaye aliongoza nchi kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 akishughulika na ukusanyaji kodi uliosaidia nchi kufutiwa madeni, na ujenzi wa miundombinu, anaonekana na chuo hicho kuwa alifanikiwa kuimarisha demokrasia hapa nchini.

Vyombo mbalimbali vya habari nchini Uganda, likiwemo gazeti la Daily Monitor, jana viliripoti kwamba vikao vya juu vya maamuzi katika uongozi wa chuo hicho maarufu Afrika Mashariki, vilijadili kwa kina na kubaini kwamba rais huyo wa zamani wa Tanzania anastahili kupewa heshima hiyo.

Msemaji wa chuo hicho, Gilbert Kadilo alisema kwamba Mkapa, ambaye alisomea shahada yake ya kwanza chuoni hapo, atatunukiwa heshima hiyo leo kwenye sherehe maalumu ambazo pia amealikwa kuwa mgeni rasmi na ataangoza harambe ya kuchangia maboresho ya chuo hicho kikongwe.

Kadilo alisema kwamba jina la Mkapa lilipatikana baada ya mchakato mrefu uliohitimishwa uliofanywa na seneti na baraza la chuo hicho.

Mkuu wa chuo hicho, Profesa Mondo Kagonyera alisema kwamba Mkapa ni miongoni mwa viongozi wa Afrika, ambao walisoma chuoni hapo, akiwa amejiunga na chuo mwaka 1957 na kumaliza 1962 na kutunukiwa Shahada ya Fasihi na Lugha ya Kiingereza.

Profesa Kagonyera aliwataja viongozi wengine waliosoma kwenye chuo hicho chenye umri wa miaka 87 tangu kianzishwe kuwa ni rais wa kwanza wa Tanzania na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, rais wa Kenya, Mwai Kibaki, kiongozi wa Nigeria Hajj Shehu Shagarna na marais wanne wa zamani wa Uganda, Godfrey Binaisa, Milton Obote, Sir Edward Luwangula Muteesa II na Yusuf Lule.

Hapa nchini Mkapa anatuhumiwa kusajili kampuni ya ANBEN na kufanya biashara akiwa Ikulu, huku familia yake na Waziri wake wa Nishati na Madini, Daniel Yona zikitajwa kujitwalia mgodi wa Makaa ya Mawe Kiwira kinyume na taratibu, kwa bei poa ya Sh70 milioni.

Rais huyo mstaafu pia amekuwa akitajwa kutumia mamlaka yake kuandika barua na kuagiza nyongeza ya mkataba wa miaka kumi kwa kampuni ya International Container Terminal (TICTS), ambayo inaendesha kitengo cha makontena kwenye Bandari ya Dar es salaam. Pamoja na tuhuma hizo zote, Mkapa amekuwa hataki kuzizungumzia, lakini hivi karibuni alisema kwenye mkutano wa mfuko wa Mkapa kuwa "hawezi kuzuia masikio ya watu kusikia, lakini anaweza kuuzuia mdomo wake kusema", kauli iliyoonyesha kuwa ataendeleza msimamo wake wa kutojibu tuhuma zinazomkabili.


Imekaaje hii!
 
Chuo Kikuu Makerere kumuenzi Mkapa

Imekaaje hii!

Imekaa bomba sana! angekuwa gerezani kwa tuhuma zote mnazomsema angeenziwa na hiki chuo????

Suppose mtu leo anatoka mwezini , ukamweleza Mkapa mwizi, atakuuliza mbona yuko huru! utajibu nini??

Bado JK sijui atajigawia nini!!
 
Hongera sana Mh. B. W. Mkapa,

Mwenyezi Mungu akuongezee yote mema,

Akupe Maisha Marefu, Uwaone Vitukuu na Vining'ina wako. Amen.
 
Huko Uganda kuna museveni, Nae kaiba dhahabu nyingi sana huko DRC!!
Nafikiri kashinikiza ili akistaafu wafungue kampuni ya madini!!
 
Huko Uganda kuna museveni, Nae kaiba dhahabu nyingi sana huko DRC!!
Nafikiri kashinikiza ili akistaafu wafungue kampuni ya madini!!

Ndugu Kilemi,

Una uhakika na uliyo andika?

Angalia, Ijue Kweli nayo Kweli itakuweka huru.

Hongera sana Mzee B. W. Mkapa.
 
Ni vyema sana.

Mh. B. W. Mkapa anastahili,

Wabaya wake walie tu.
We ndugu unaishi sayari gani?

Hongera sana Mh. B. W. Mkapa,

Mwenyezi Mungu akuongezee yote mema,

Akupe Maisha Marefu, Uwaone Vitukuu na Vining'ina wako. Amen.
Amuongezee yote Mema!!!. Unamaanisha mgodi wa Kiwira hautoshi, aongezewe upi tena?
Ndugu Kilemi,

Una uhakika na uliyo andika?

Angalia, Ijue Kweli nayo Kweli itakuweka huru.

Hongera sana Mzee B. W. Mkapa.
Nani wa kuijua kweli between the two of you?

Ama kweli ukipenda, Chongo...!
Pole wee!
 
Imekaa bomba sana! angekuwa gerezani kwa tuhuma zote mnazomsema angeenziwa na hiki chuo????

Suppose mtu leo anatoka mwezini , ukamweleza Mkapa mwizi, atakuuliza mbona yuko huru! utajibu nini??

Bado JK sijui atajigawia nini!!

ni kweli usemayo waberoya ..mkapa anastrahiri kufunguliwa mashitaka lakini sijui sheria inasubiri nini kutendeka ??
 
endelea kupiga kimya BWM. husinene jambo lolote ili husije kujikwaa. Ukipokea shahada husisahau ukanena lisilo jema kwa WTZ
 
We ndugu unaishi sayari gani?


Amuongezee yote Mema!!!. Unamaanisha mgodi wa Kiwira hautoshi, aongezewe upi tena?

Nani wa kuijua kweli between the two of you?

Ama kweli ukipenda, Chongo...!
Pole wee!
PakaJimmy!
Kwanza nimsahihishe aliyeanzisha hii thread Makrere University na sio Makelele. Pili Mkapa alitokea Msumbiji na aktawala nchi kama mgeni na ndio aliwapendelea sana wahamiaji na watu wa kuja kama wahindi akina Rostam Aziz; akina Iddi Simba na ndugu zao wengi kutoka Uganda;Rwanda na kadhalika na ndio maana it makes a lot of sence kwa wafadhili na watu wa nje kumfagilia kwani si aliwafaa? For sure Modest ni mtu wa kja na is one of the big beneficiaries wa UHOVYO aliotutendea Jambazi kwa jina la Benjamini William Mkapa kumsifu is actually a blasphemy!!
 
thafi thana, tunukiwa baba
hata wafanyeje au wasemeje wewe ndo umeitoa nchi hii kichakani na imeheshimiwa dunian hata hawa wanaosafiri kila siku ziara ya siku kumi nje ya nchi bado wamesimama juu ya mabega yako.
 
PakaJimmy!
Kwanza nimsahihishe aliyeanzisha hii thread Makrere University na sio Makelele. Pili Mkapa alitokea Msumbiji na aktawala nchi kama mgeni na ndio aliwapendelea sana wahamiaji na watu wa kuja kama wahindi akina Rostam Aziz; akina Iddi Simba na ndugu zao wengi kutoka Uganda;Rwanda na kadhalika na ndio maana it makes a lot of sence kwa wafadhili na watu wa nje kumfagilia kwani si aliwafaa? For sure Modest ni mtu wa kja na is one of the big beneficiaries wa UHOVYO aliotutendea Jambazi kwa jina la Benjamini William Mkapa kumsifu is actually a blasphemy!!

Wewe PakaJimmy na Mkereme, Mliye tu.

Hongera Mzee B. W. Mkapa.
 
Makerere University ni chuo kinachoheshimika na kina watu wasomi na wenye akili zaidi ya wengi wetu tuliomo humu JF. Tuheshimu tu uamuzi wao huu.
 
Rais huyo mstaafu pia amekuwa akitajwa kutumia mamlaka yake kuandika barua na kuagiza nyongeza ya mkataba wa miaka kumi kwa kampuni ya International Container Terminal (TICTS), ambayo inaendesha kitengo cha makontena kwenye Bandari ya Dar es salaam. Pamoja na tuhuma hizo zote, Mkapa amekuwa hataki kuzizungumzia, lakini hivi karibuni alisema kwenye mkutano wa mfuko wa Mkapa kuwa "hawezi kuzuia masikio ya watu kusikia, lakini anaweza kuuzuia mdomo wake kusema", kauli iliyoonyesha kuwa ataendeleza msimamo wake wa kutojibu tuhuma zinazomkabili.

Imekaaje hii!

Anaamua kukaa kimya kwasababu tuhuma zote ni kweli atajibu nini!!!
 
hao ni marafiki zake tu, unajua chuo makini hakiwezi kumtunuku mtu mwenye mapungufu na hatia kadhaa za utumiaji mbaya wa madaraka yake kama mkapa, hizi tuzo za heshima zinatolewaje kwa mtu asie jiheshimu, mwenye kiburi ,asie staha, kama mkapa akitaka aombe ikulu imvue kinga aone heshima yake.
 
Back
Top Bottom