Make America Great Again

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
98,112
Reaction score
143,524
Siasa ama kweli ni mchezo mchafu ulio wa kinafiki sana kiasi kwamba watu wakweli kama mimi ambao hatujui kuremba hatuuwezi.

Kwenye msimu huu wa uchaguzi mkuu wa Marekani, mgombea wa kiti hicho Bw. Donald Trump, kauli mbiu yake ni 'Make America Great Again'.

Kauli mbiu hiyo imepondwa na wapinzani wake wakuu ambao ni Hillary Clinton na chama chake cha Democrats.

Baadhi ya hao Democrats wamedokeza kwamba kauli mbiu hiyo ni ya kibaguzi.

Lakini eti ni ya kibaguzi sasa hivi kwa sababu tu inatumiwa na Donald Trump.

Wakati Bill Clinton alipoitumia mwaka 1991 na 1992 wakati anagombea urais, kauli hiyo haikuwa ya kibaguzi.

Hata mwaka 2008 wakati Hillary anagombea, huyo mumewe aliitumia tena hiyo kauli wakati akimpigia debe mkewe.

Situngi, sizushi, wala simsingizii mtu. Jioneeni wenyewe!




Halafu hebu ona hapa jinsi Hillary anavyosema eti hakubaliani na wanaosema make America great😀.


Huu kama siyo unafiki ni nini?

Akiba ya maneno.....anyone?
 
Ndiyo Siasa na Wanasiasa. Wanasiasa husema kulingana na hadhira na nyakati zilizopo. Siamini kama wale strategists wa vyama kwenye kampeni kama kazi yao ni kupanga mikakati ya kujenga Taifa kwa maana yenyewe hasa. Hapana.

Kazi yao ni kusoma akili za wapiga kura na kupanga namna ya kucheza nazo kwa manufaa ya wagombea wao.
 

Halafu utashangaa sasa wanazi wa Hillary watavyokana kuwa Bill hakuwahi kusema 'make America great again'.

Ndo yaleyale ya Lowassa....miaka nenda rudi watu wamemponda kuwa ni fisadi halafu mwisho wake ndo anakuja kuwa mgombea wao wa urais.
 
Umenena vizuri ila umeharibu hapo Chini kumuweka mh Lowassa maana hauna proof kua ni fisadi ndio maana umebakia kua wimbo mahakamani haendi, over!
 
Halafu utashangaa sasa wanazi wa Hillary watavyokana kuwa Bill hakuwahi kusema 'make America great again'.

Ndo yaleyale ya Lowassa....miaka nenda rudi watu wamemponda kuwa ni fisadi halafu mwisho wake ndo anakuja kuwa mgombea wao wa urais.
Wanasiasa wanafanana kwa mengi ila wanatofautiana kidogo.

Hata Wananchi nyakati za kampeni huwa kama wendawazimu kidogo. Kuna wananchi wanampa kura mgombea kwa sababu ya "u handsome", au uongeaji mzuri, utani, eneo analotoka mgombea, kabila, rangi, ubaguzi, ucheshi nk.

Na hao huwezi kuwaambia chochote cha kinyume kuhusu mgombea wao wakakuelewa. Kama ambavyo kuna majimbo Rep au Democratic wana uhakika wa kushinda hata bila kampeni ya nguvu.
 
"We wanna take our country back"

Of course, GOP wakisema hivyo wanaitwa racists.

Lakini Democrats wakisema....kunakuwepo na radio silence.

Check out this video in it's entirety.

John Kerry kawahi kusema...Howard Dean kawahi kusema...Joe Biden keshasema...Hillary Clinton keshasema...na Barack Obama keshasema.

 
Inategemea ametamka hayo maneno katika muktadha gani?Jinsi anavyotamka Trump ni kibaguzi zaidi.Sera za trump ni za kibaguzi zaidi.Trump akitoka kidedea itaashiria wamerekani wengi bado ni wabaguzi.
 
Inategemea ametamka hayo maneno katika muktadha gani?Jinsi anavyotamka Trump ni kibaguzi zaidi.Sera za trump ni za kibaguzi zaidi.Trump akitoka kidedea itaashiria wamerekani wengi bado ni wabaguzi.

Wamarekani walio wengi sio wabaguzi.

Ingekuwa ni wabaguzi Obama asingeshinda hata jimbo moja!
 
Wamarekani walio wengi sio wabaguzi.

Ingekuwa ni wabaguzi Obama asingeshinda hata jimbo moja!
Obama alishinda kwa sababu ya kura za walatino, weusi na wazungu wasio kuwa na ubaguzi wa waziwazi.
Trump amefanikiwa kuibua tena hulka na silika za kibaguzi kwa weupe wengi ata wale waliompigia kura Obama.
 
Obama alishinda kwa sababu ya kura za walatino, weusi na wazungu wasio kuwa na ubaguzi wa waziwazi.
Trump amefanikiwa kuibua tena hulka na silika za kibaguzi kwa weupe wengi ata wale waliompigia kura Obama.

Unajua jinsi rais wa Marekani anavyochaguliwa wewe?

Hapo chini ni baadhi ya majimbo aliyoshinda Obama. Haya twende kwa facts...niambie asilimia ya minorities na wazungu katika hayo majimbo....

Oregon kuna Walatino na weusi kiasi gani?

Washington state kuwa minorities kiasi gani?

Iowa kuna minorities kiasi gani?

Illinois kuna minorities kiasi gani?

Wisconsin kuna minorities kiasi gani?

Minnesota kuna minorities kiasi gani?

Virginia kuna minorities kiasi gani?

Michigan kuna minorities kiasi gani?

Maine kuna minorities kiasi gani?
 
Trump haandamwi kwa kauli yake ya make America great again kuwa ya kibaguzi Bali maneno yake ya kuwakejeli Hispanics kuwa wabakaji,wezi,wanachukua na kumiliki kazi nk, kuwasema blacks vby nk ,Ww unayemtetea Trump wkt akina McCain wanampinga trump kwa kauli zke ,..

Trump na Hillary wote candidates wabovu

Sanders,Rubio ndio walikuwa chaguo sahh ,
 

Akikujibu nishitue
 
Akikujibu nishitue

Kuna majimbo mengi tu ambayo Obama alishinda ambayo zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wake ni Wazungu.

Sasa kwenye hayo majimbo alishindaje kama Wazungu walio wengi hawakumpigia kura?

Iowa zaidi ya 90% ya watu wake ni Wazungu. Obama alishinda hilo jimbo chaguzi zote mbili.

Wisconsin zaidi ya 85% ya wakazi wake ni Wazungu. Obama alishinda chaguzi zote mbili tena ushindi mzuri tu.

Minnesota na yenyewe zaidi ya 80% ya wakazi wake ni Wazungu. Huko nako Obama alishinda ushindi mnono tu.

Illinois, huko anakotokea Obama zaidi ya 70% ya wakazi wake ni Wazungu. Obama alishinda kwa landslide.

Hiyo ni mifano michache tu ya majimbo yenye Wazungu wengi kuliko minorities wote combined lakini Obama alishinda.

Sasa alishinda shindaje huko bila kupigiwa kura na majority ya Wazungu wa huko?
 
Wewe nyani ngabu sema usemacho lakini majority of Republican, conservatives, Tea party, political right, southerners, anti immigrant etc wengi wao ni racists na wanaamini in social inequality na ndio supporter wakubwa wa Trump,what is the point for Trump to say Mexican wakija US wanaleta magonjwa na crime wangekuwa wazungu wenzake angesema hivyo? na akili ya kina Trump na wafuasi wake wanaamini welfare ni kwa minority tuu kumbe wazungu kwa millions nao wamo tuu,you don't need to be genius kuona ubaguzi wa Trump na watu wake maana ni wazi wazi kama wewe huoni lazima utakuwa na issues huko kichwani
 
Make America Great Again means America is not great at the moment. Now it feels racist if you consider what G. Bush did to the country compared to Obama. America is doing far better now than it was when Bush walked out of state house. Try to imagine if Obama na Bush switched places what would Trump have to say? It is hard to appreciate blackman's effort in this world, people just think it is a coincidence!

Brace yourself with a president who shoots and aims later. Trump is Bush version 2-the only difference is that the former is worse than latter.
 

You and your whale of a wife are both deplorable.
 
Eti Killery Clinton Anyway Vote For Donald Trump to [HASHTAG]#MakeAmericaGreatAgain[/HASHTAG]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…