Makanisa Nchini Mjitafakari

Makanisa Nchini Mjitafakari

Ni Lini Watoto Wa Waumini wa Kanisa Walio Vijijini watasoma Katika Hizo Shule Zenu zinazofaulisha Division 1?

Wakati wakiwa Wanatoa Sadaka na Michango ya Shukurani, Na Harambee na Michango Mingine ya Kutegemeza Sijui nini wanaambiwa Inapelekwa Jimboni sijui inaenda Wapi. Sasa Mbona Mkishaanzisa Hizo shule Zenu mnakaribisha Matajiri na Wenye Pesa Ndio wakasome humo wakati waumini wenu Watoto wao Hawajiwezi na Wamekaa Bila Elimu Bora!
 
Ni Kama kuna ujumbe fulani Unataka kuufikisha lakini kwa andiko hili wengi watapoteza mwelekeo!

Mungu Katika Biblia ameagiza 'Nitoleeni Fungu la Kumi sababu hiyo ni haki yangu, na akaongeza nijaribuni Kwa njia hiyo Muone kama sitawafungulia madirisha ya Mbinguni.

Kuna sehemu ameagiza 'pandeni juu milimani mkalete miti mnijengee Kanisa.

Yote hayo ili Jina Lake Litukuzwe.

Ukitafakari Hayo Utagundua Michango na Sadaka kwa Mungu siyo Hiari ni Lazima.

Nafikiri shida yako mtoa Mada ni Baadhi wa wanaokusanya hiyo michango na Sadaka Hawatumii kwa Malengo Yaliyokusudiwa.

Ushauri : Wewe Hapo Ulipo Ukiona Sadaka zako Zinapigwa. Hama tu.
 
Viongozi wengi wa makanisa wanaishi maisha bombastic sana huku waumini wao, waleta sadaka, ni chokest mbaya sana.
Ndio mnatakiwa mjiulize kama Waumini mmepumbazwa vya Kutosha Maana Mlikuwa hamna Cha Kusimamia wala Kuhoji. Na Waliwaambia Ukihoji unamkufuru Mungu na Utalaaniwa wakijua Ndio Njia Nzuri ya Kuwateka Watu

Ni mipango yao Ili wamiliki hii Dunia ila Mungu wa Kweli atawaumbua Vibaya sana maana Watu wenye Akili timamu watakuja Kuwaumbua sana
 
Mengine yanafungua mabenki ya kibiashara, viongozi wa haya makanisa wamekuwa hawana aibu kubebesha waumini wao mizigo mizito wasiyoweza kubeba wao wenyewe, wanajenga mashule, vyuo na mahospitali ambayo waumini wao hawanufaiki kwa kutoa michango yao
 
Mtoa mada hama kanisa ulilomo.
Kumbukumbu la torati
Maagizo kuhusu fungu la kumi
22 Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika mavuno yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka. 23 Nawe utakula mbele za BWANA, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake, zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yako ya ng'ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha BWANA, Mungu wako, daima. 24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua BWANA, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia BWANA, Mungu wako; 25ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua BWANA, Mungu wako; 26na zile fedha zitumie kwa chochote itakachotamani roho yako, ng'ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako chochote; nawe utakula huko mbele za BWANA, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako; 27 na Mlawi aliye ndani ya malango yako usimwache, kwani hana fungu wala urithi pamoja nawe.

28 Kila mwaka wa tatu, mwisho wake, toa fungu la kumi lote la mavuno yako ya mwaka huo, uliweke ndani ya malango yako; 29 na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako, na waje wale na kushiba; ili kwamba BWANA, Mungu wako, akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.
 
Ni Kama Kuna ujumbe fulani Unataka kuufikisha lakini kwa andiko hili wengi watapoteza mwelekeo..!
Mungu Katika Biblia ameagiza 'Nitoleeni Fungu la Kumi sababu hiyo ni haki yangu, na akaongeza nijaribuni Kwa njia hiyo Muone kama sitawafungulia madirisha ya Mbinguni.!
Kuna sehemu ameagiza 'pandeni juu milimani mkalete miti mnijengee Kanisa...!
Yote hayo ili Jina Lake Litukuzwe.
Ukitafakari Hayo Utagundua Michango na Sadaka kwa Mungu siyo Hiari ni Lazima...!
Nafikiri shida yako mtoa Mada ni Baadhi wa wanaokusanya hiyo michango na Sadaka Hawatumii kwa Malengo Yaliyokusudiwa...!
Ushauri : Wewe Hapo Ulipo Ukiona Sadaka zako Zinapigwa ...Hama tu.
Mleta mada ameshauri fungu la kumi na shukurani zetu tuzipeleke moja kwa moja kwa wasio jiweza. Kanisani zinawanufaisha wenye uwezo kwa kufungua miradi isiyo na msaada kwa wenye uhitaji...

#tuamkekanisanitunapigwanakitukizitodeile
 
Nikawaza sana eti nitoe elfu 20 ya sadaka kanisani wakati ndugu yangu kule kijijini hali yake ngumu wengine wanasoma kwa tabu, nikasema alie juu anaona mpaka moyoni mwangu , basi nikatuma 18 kijijini elfu 2 ibaki kanisani na hii policy ni mpaka kesho nasaidia wenye uhitaji kwa hali na mali, Kanisani tupo wengi nisipotoa mimi atatoa mwingine.
 
Kama jehanamu ipo kweli ! Walio na Makanisa wataungua sanaaaaa. Makanisa ni Biashara za watu wenye kuwatumia maskini na matajiri kujiongezea kipato. Yapo Makanisa machache sana viongozi wao wataiona mbingu. Haya ya walokole hakuna hata moja litasalia yataungua kama mti mkavu.. kwani ni wachafu kuliko mnyama....hawana tofauti na waganga wa kienyeji..
 
Tukirudi kwenye fikira dini zote tulizo nazo ni dini za mchongo tuu ni vile tuu tumezaliwa na kukuta wakubwa wetu wanaabudu.

Fikiri kabla ya biashara ya utumwa watu walikua hawajui uislam africa.

Fikiri kabla ya kuja wazungu watu walikua hawajui ukristo africa.

Je walioishi kabla hukumu zao zikoje.

Jambo tafakarishi tunaomba kwa pamoja juu ya kinga fulani ila hilo hilo jambo lina kwenda tupata, mfano ufaulu, nafuu ya mgonjwa, ajari.

Kikubwa tuishi kwa kuwajari wenzetu, tutende yaliyo mema.
 
Kumbukumbu la torati
Maagizo kuhusu fungu la kumi
22 Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika mavuno yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka. 23 Nawe utakula mbele za BWANA, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake, zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yako ya ng'ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha BWANA, Mungu wako, daima. 24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua BWANA, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia BWANA, Mungu wako; 25ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua BWANA, Mungu wako; 26na zile fedha zitumie kwa chochote itakachotamani roho yako, ng'ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako chochote; nawe utakula huko mbele za BWANA, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako; 27 na Mlawi aliye ndani ya malango yako usimwache, kwani hana fungu wala urithi pamoja nawe.
28 Kila mwaka wa tatu, mwisho wake, toa fungu la kumi lote la mavuno yako ya mwaka huo, uliweke ndani ya malango yako; 29 na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako, na waje wale na kushiba; ili kwamba BWANA, Mungu wako, akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.
Kaa chini na Akili yako Mwenyewe Jiulize aliyeandika Hayo ni Nani! Kama Yameandikwa na Binadamu mwenzako basi Jua Umepigwa.

Na ukisoma.Mstari mpaka Mstari utajua Ni maandiko ya Kibinadamu mwenye Tamaa ya Mali mpaka anasema Mwenyewe kabisa huyo Mwandishi Kwamba hizo Sadaka kama Ni Nzito Basi Zibadili ziwe Pesa halafu zipeleke na Ukishazipeleka Yeye atatumia Kama Roho yake inavyo penda


Mungu hajawahi andika chochote kile wala Kumwambia Mtu aandike Kitu
 
Huu ujumbe uwafikie kina mwa. Nimewahi uliza hili vipi muumini masikini ananufaika vipi kiuchumi akijiunga na dhehubu lake. Inatakiwa madhehebu yaanzishe vyuo vya ujuzi kupitia sadaka na michango ya waumini kisha waumini masikini wasome wapate ujuzi Ili wazalishe kisha watoe sadaka. Nyumba za ibada zichunge watu kiroho na kiuchumi. Hata maandiko usema usiende nyumbani mwa Bwana mikono mitupu.
 
Back
Top Bottom