Makandarasi wanaokiuka mikataba yao waonywa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
Mbega%20monica%281%29.jpg

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega.



[FONT=ArialMT, sans-serif]Serikali mkoani Kilimanjaro, imesema kamwe haitawavumilia makandarasi wanaokwenda kinyume na mkataba wa ujenzi wa barabara kwa kuchelewa kukamilisha kazi au kujenga chini ya kiwango.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Vile vile, imesisitiza azma yake ya kuchukua hatua za[/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]kisheria mara moja kwa makandarasi wababaishaji[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]wenye lengo la kujipatia fedha za walipa kodi bila kujenga barabara kwa kiwango kinachotakiwa na kwa mujibu wa mkataba kazi walizopewa.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Mkuu wa Mkoa huo, Monica Mbega, aliyasema hayo jana wakati wa uzinduzi wa ujenzi barabara nne za kiwango cha lami za Kwasadala-Masama, Kibosho-Sinde-Kwa Rafaeli-Internation School, Rau Madukani-Uru Njari na Kawawa–Nduoni-Marangu Mtoni katika wilaya za Hai na Moshi Vijijini ikiwa ni utekelezaji wa ahadi za Rais Jakaya Kikwete wakati wa kampeni za[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]uchaguzi mwaka 2005.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Alimuagiza Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) mkoani Kilimanjaro kushirikiana na mhandisi mshauri kufuatilia mara kwa mara ujenzi wa barabara hizo ili uwe wa kiwango na kuepusha gharama zisizo za msingi[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]kwani kuchelewesha au kubadili badili hakuvumiliki.[/FONT]

[FONT=ArialMT, sans-serif]Awali, katika taarifa yake, Meneja wa Tanroads mkoani Kilimanjaro, Tumaini Sarakikya, alisema barabara hizo zina urefu wa kilomita 80.1 na kwamba hadi sasa zimetumia zaidi ya Sh. milioni 497.8 kwa ajili ya usanifu kwa mwaka wafedha 2008/09.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Sarakikya alisema barabara ya Kibosho Shinde-Kwa[/FONT] [FONT=ArialMT, sans-serif]Raphael-Internation School (27.5), imejengwa kwa kiwango cha lami kwa kilomita nne kwa zaidi ya Sh. billion 1.9. [/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Hadi sasa zaidi ya Sh. billion 2.4 zimetumika.[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Alizitaja barabara zitakazojengwa kwa kiwango cha lami na idadi ya kilomita kwenye mabano kuwa ni Kwasadala-Masama (12.5).[/FONT]
[FONT=ArialMT, sans-serif]Nyingine ni Rau Madukani-Uru Njari (9.5) na Kawawa –Nduoni-Marangu Mtoni (30.6). [/FONT]



CHANZO: NIPASHE
 
Ufinyu wa kujua mikataba kwa pande zote, Serikali na wakandarasi kunachangia sana kufisha miradi mingi ya ujenzi.
Tatizo la watendaji wengi kutofahamu kwao matatizo ya miradi ya ujenzi kunachangia sana wao wenyewe kuwasingizia wakandarasi kwa kila kitu, ikiwa ndio njia rahisi ya kujikosha.
Tatizo la fani ya ujenzi inafikirika kuwa ni rahisi sana na kueleweka na kila mtu.Viongozi wengi, hata walio katika wizara zinazohusu ujenzi hawazifahamu taratibu za ujenzi wa kukandarasi.
Kama mradi unausimamizi mzuri wa kihandisi na kimradi(contract management) siyo rahisi mradi kufa.Wasimamizi wengi wa miradi(wahandisi na watoa fedha kiserikali) huwa hawana muda kutembelea miradi, hivyo matatizo kujilimbikiza na kuua mradi.
Tatizo la pili ni RUSHWA!!!
Siyo siri kuwa viongozi wengi wanashiriki katika kuomba KITU KIDOGO.
Hii inaua sana miradi maana hiyo KITU KIDOGO lazima ifidiwe kwenye kazi kwa kupunguza viwango vya ujenzi.Sasa hapo ndio tunawashangaa sana viongozi maana wanjua hilo linatendeka na wanajua jinsi ya kulitatua badala ya kulifanya issue kwenye majukwaa ya kisiasa.
 
Ufinyu wa kujua mikataba kwa pande zote, Serikali na wakandarasi kunachangia sana kufisha miradi mingi ya ujenzi.
Tatizo la watendaji wengi kutofahamu kwao matatizo ya miradi ya ujenzi kunachangia sana wao wenyewe kuwasingizia wakandarasi kwa kila kitu, ikiwa ndio njia rahisi ya kujikosha.
Tatizo la fani ya ujenzi inafikirika kuwa ni rahisi sana na kueleweka na kila mtu.Viongozi wengi, hata walio katika wizara zinazohusu ujenzi hawazifahamu taratibu za ujenzi wa kukandarasi.
Kama mradi unausimamizi mzuri wa kihandisi na kimradi(contract management) siyo rahisi mradi kufa.Wasimamizi wengi wa miradi(wahandisi na watoa fedha kiserikali) huwa hawana muda kutembelea miradi, hivyo matatizo kujilimbikiza na kuua mradi.
Tatizo la pili ni RUSHWA!!!
Siyo siri kuwa viongozi wengi wanashiriki katika kuomba KITU KIDOGO.
Hii inaua sana miradi maana hiyo KITU KIDOGO lazima ifidiwe kwenye kazi kwa kupunguza viwango vya ujenzi.
Sasa hapo ndio tunawashangaa sana viongozi maana wanjua hilo linatendeka na wanajua jinsi ya kulitatua badala ya kulifanya issue kwenye majukwaa ya kisiasa.

Ndio maana sasa wanaonywa
 
Fani nzima ya ujenzi na kandarasi za serikali imejaa usanii mtupu na hakuna asiyechukua rushwa katika vitengo hivyo wanaoshughulikia ugawaji wa tenda na kandarasi mbalimbali. Kifupi sana ndio sehemu ambazo humaliza pesa za serikali bila kazi iliyokusudiwa kufanyika. Hao wanasiasa nao wana matatizo yao, jukwaani wanaongea kitu kingine baadaye wenyewe wanaenda kudai rushwa na ikitokea mnafahamiana na ukamuuliza mbona majukwaani mnasema hivi simply atakujibu kwamba ile ni siasa we kata tumalizane!! Tanzania zaidi ya uijuavyo, kizazi cha viongozi wapenda nchi na wakweli kimekwenda na nyerere wake!!
 
Back
Top Bottom