Katika nchi zilizoendelea miji hujengwa na makampuni ya ujenzi.
Moja ya shughuli zao ni kununua ardhi wakajenga kitongoji/mji wa kisasa. Chukulia eneo lote la Tabata lingekuwa limejengwa na kampuni ya ujenzi. Nyumba za kisasa na za mpangilio.
Na baadae kampuni hiyo huuza nyumba za eneo hilo au kuzikabidhi kwa mwenye mradi wake (mwekezaji)
Hivyo ndivyo miji inavyojengwa. Hakutakuwa na mfumuko wa bei za nyumba za ajabu ajabu. Watu wanaweza kupewa mikopo ya nyumba. Ukishindwa kulipa unatolewa tu hela yako uliyokwisha lipa hurudishiwi na nyumba anauziwa mtu mwingine.
Yafuatayo ni makampuni kumi kati ya mengi yanayoshughulika na ujenzi wa makazi ya wananchi nchini Marekani.
1. D.R Horton Inc.
2. Pulte Group (2013
3. Lennar Corp
4. Toll brothers Inc
5. Taylor Morrison Home
6. Hovnanian Enterprises.
7. KB Home
8. Ryland Homes
9. Standard Pacific corp
10. Meritage Homes
Mtu anitajie makampuni kumi ya ujenzi wa makazi (sio ya nyumba moja moja) yaliyopo Tanzania.
Inasikitisha sana viongozi wanaposafiri nje wanauona utaratibu lakini wanashindwa kuutekeleza Tanzania.
Hata ikibidi kuleta wawekezaji wa ujenzi wa miji. Watakuwa ni wa maana kuliko Acacia. Kwa sababu mwisho wa siku wawekezaji wa hivi wanatuachia miji ya kisasa.
Uwekezaji wa hivi utatoa ajira nyingi sana kwenye sekta ya ujenzi na usafi wa miji. Wawekezaji sio Tigo na Voda tu ambao tunawashukuru kwa kurahisisha mawasiliano lakini kwa upande mwingine wamebwetesha sana watanzania. Umbea umetawala kwenye instagram na Facebook. Kazi hakuna na wananchi wananyonywa sana visenti vyao kwenye mabando yasiyochacha na yanayochacha.